Burna Boy: 'Sikanyagi tena Afrika Kusini' asema msanii maarufu wa Nigeria:


Msanii Burna Boy wa miondoko ya Afrobeat nchini Nigeria ameapa hatawahi kukanyaga Afrika Kusini baada ya ghasia dhidi ya raia wa kigeni kuzuka upya nchini humo.

Katika post kadhaa za Twitter masanii huyo wa miaka 28- alisema hajawahi kuzuru nchi hiyo tangu mwaka 2017 lakini hatawahi kurudi tena hadi serikali ya Afrika Kusini itakaposhughulikia suala hilo.

Lakini serikali inatakiwa ''kufanya miujiza ila sijui jinsi itakavyoweza kutatau suala hili", aliongeza.

Tayari polisi nchini Afrika Kusini imewakamata zaidi ya watu miamoja waliowashambulia raia wa kigeni katika miji ya Johannesburg, Pretoria na maeneo mengine.
Msanii huyo ambaye alishinda tuzo ya kimataifa ya BET mwezi Juni, amesema mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni yanaenda kinyume na maadili - na kugusia jinsi bara la Afrika lilivyoisaidia nchi hiyo katika mapambano dhidi ya utawala wa wazungu walio wachache.

"Naelewa miaka mateso waliopitia miaka mingi iliopita imewafanya Waafrika Kusini kuchanganyikiwa kiasi cha kuwachukulia kama maadui watu waliowasaidia wakati wa utawala wa kibaguzi," Burna Boy alianginda katika Twitter yake.

Aliongeza kuna raia wa Afrika Kusini ni ''watu wazuri na wapenda maendeleo "… lakini kwa hili wamepotoka".

Raia wa Nigeria waliojawa na ghadhabu walivamia na kuharibu mali katika duka la jumla linalolimikiwa na raia wa Afrika jatika mji wa kibiashara wa Lagos.

Waziri wa Nigeria wa Habari na Utamaduni Alhaji Lai Mohammed, ameelezea kusikitishwa kwake na ripoti kwamba Wanageria wameanza kuvamia kampuni za nchi hiyo zinazoendesha shughuli zake Nigeria.

Msanii huyo ambaye alishinda tuzo ya kimataifa ya BET mwezi Juni, amesema mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni yanaenda kinyume na maadili - na kugusia jinsi bara la Afrika lilivyoisaidia nchi hiyo katika mapambano dhidi ya utawala wa wazungu walio wachache.

"Naelewa miaka mateso waliopitia miaka mingi iliopita imewafanya Waafrika Kusini kuchanganyikiwa kiasi cha kuwachukulia kama maadui watu waliowasaidia wakati wa utawala wa kibaguzi," Burna Boy alianginda katika Twitter yake.

Aliongeza kuna raia wa Afrika Kusini ni ''watu wazuri na wapenda maendeleo "… lakini kwa hili wamepotoka".

Raia wa Nigeria waliojawa na ghadhabu walivamia na kuharibu mali katika duka la jumla linalolimikiwa na raia wa Afrika jatika mji wa kibiashara wa Lagos.

Waziri wa Nigeria wa Habari na Utamaduni Alhaji Lai Mohammed, ameelezea kusikitishwa kwake na ripoti kwamba Wanageria wameanza kuvamia kampuni za nchi hiyo zinazoendesha shughuli zake Nigeria.

Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumanne Bw. Mohammed alisema hatua hiyo ni sawa na kujipiga mwenyewe.

''Wawekezaji wa MTN na Shoprite ni raia wa kigeni na wanaofanya kazi katika maduka hayo ni Wanigeria bila shaka kampuni hizo zikisitisha huduma zake kwa kuhofia kuvamiwa watakaoathirika ni watu wetu''aliongeza.

Alhaji Mohammed amewahakikishia Wanaigeria kuwa serikali inafanya kila iwezalo kukomesha mashambulio ya mara kwa mara dhi ya raia wake nchini Afrika Kusini.

Polisi wamepelekwa katika maeneo yote yaliokumbwa na vurugu na uporaji wa maduka huku sehemu zingine mali ya raia wa kigeni ikichomwa moto.

Wakenya pia ni miongoni mwa raia wa kigeni walioathiriwa na vurugu hizo. Balozi wa Kenya nchini Afrika Kusini Jean Kamau amethibitisha kuwa raia kadhaa wa nchi hiyo wameshambuliwa katika Mkoa wa Gauteng .

Watu 189 wamekamatwa kwa kujihusisha na ghasia, uharibifu wa mali na wizi katika maeneo tofauti tangu siku ya Jumapili.

Tamko la SADC

Jumuia ya Maendeleo Mataifa ya Kusini mwa Afrika SADC, imelaani vikali matukio ya vurugu na mashambulio dhidi ya raia wa kigeni.

Katibu mkuu wa SADC DK Stergomena Tax amendika katika Twitter yake akitoa wito wa kufikiwa kwa suluhisho la kudumu kuhusu suala hilo.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?