Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2019

Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 01.10.2019:Sancho, Vertonghen, Mandzukic, Alderweireld, Wenger

Picha
Kocha wa zamani wa Arenal, Arsenal Arsene Wenger yupo kwenye orodha ya makocha wanaowaniwa na miamba ya Italia AC Milan kurithi mikoba ya kocha Marco Giampaolo.  Mshambuliaji wa Chelsea Tammy Abraham, 21, anatarajiwa kukataa ofay a kuchezea timu ya taifa ya Nigeria na badala yake kuelekeza nguvu zote kwa England iwapo ataitwa na kocha Gareth Southgate katika michezo ya kufuzu Euro 2020 dhidi ya Jamhuri ya Czech na Bulgaria.  Mkurugunzi wa michezo wa Borussia Dortmund amefichua kuwa hadhani kuwa nyota wao kinda Jadon Sancho, 19, akisalia klabuni hapo kwa muda mrefu. Sancho kutoka England alikuwa akihusishwa na Man United katika dirisha la usajili lililopita.  Beki wa Manchester United na timu ya taifa ya Ivory Coast Eric Bailly sasa kusalia nje ya uwanja mpaka mwezi Januari. Baily, 25, alipata majeraha ya goti kwenye mchezo wa kujiandaa na msimu dhidi ya Tottenham.  Beki wa Tottenham Jan Vertonghen, 32, ambaye makataba wake unaisha mwishoni mwa msimu amesema kuwa anaweza kusaini mkataba

Song Jiang, mhalifu wa Uchina aliyejificha pangoni kwa miaka 17

Picha
Polisi nchini Uchina wamemkamata mhalifu ambaye amekuwa akijificha kwa miaka 17, baada ya kutumia ndege zisizokuwa na rubani kubaini pango alimokuwa akijificha. Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 63 ,kwa kwa majina Song Jiang amekuwa akitafutwa na polisi baada ya kutoroka jela ambapo alifungwa kwa kufanya biashara haramu ya kuwasafirisha wanawake na watoto, lakini aliweza kutoroka kutoka kwenye kambi ya jela mwaka 2002. Amekuwa akiishi ndani ya pango dogo na kukata mawasiliano ya aina yoyote na binadamu kwa miaka mingi. Polisi katika mji wa Yongshan walipokea taarifa kuhusu ni wapi alipo Song mwezi Septemba , kulingana na maelezo yao katika akaunti yao ya mtandao wa kijamii wa WeChat. Taarifa hizo ziliwapeleka hadi katika eneo la milima iliyopo nyuma ya mji anakotoka katika jimbo la Yunnan lililopo kusini mashariki mwa Uchina. Baada ya kushindwa kumpata katika msako wa kawaida , maafisa walituma ndege zisizokuwa na rubani za ziada ili kuwasaidia maafisa katika msako huo. Hatimae ndege

Swahiliflix kunadi filamu za kiswahili kimataifa

Picha
Katika jitihada za kukuza soko la filamu nchini Tanzania, wasanii nchini humo wameanzisha programu tumishi inayojulikana kama Swahiliflix, ikiwalenga zaidi wapenzi wa filamu hizi walioko maeneo mbalimbali duniani. Waendeshaji wa programu hii tumishi wanahitaji filamu 14 kila juma lakini sasa wanapata fiilamu moja pekee yenye ubora. Na katika kuinua ufanisi wa kazi hiyo waendeshaji wanakiri kuwa changamoto bado ni kubwa lakini wameanza jitihada kadhaa kuzifanyia kazi. "Bado kuna changamoto katika uandaaji wa filamu za kiswahili lakini tuna mipango thabiti ya kuhakikisha kuwa na filamu zenye taswira zenye ubora zaidi na tuna uhakika baada ya muda mfupi swahiliflix itakuwa ni sehemu ambayo mtu akitaka kuangalia kitu chenye ubora wa juu anakuja kwetu"Maximilian Rioba ni mkurugenzi wa programu hiyo. Hadi sasa zaidi ya watu elfu kumi na tano wameanza kufaidi matunda ya mfumo huo wa lugha ya Kiswahili ikiwa ni chachu ya kueneza lugha ya kiswahili. Ni nani aliyeandika Kiswahili kibov

Mpishi wa Italia akamatwa kwa kutumia bangi kama ‘kiungo cha kuongeza ladha mpya’

Picha
Mpishi mmoja amekamatwa kwa kutuhumiwa kwa ulanguzi wa madawa ya kulevya baada ya polisi kugundua bangi nyumbani kwake, vyombo vya habari Italia vinaripoti. Carmelo Chiaramonte ambaye ni mpishi anayeshiriki kipindi kwenye televisheni alipatikana na mimea miwili mikubwa ya bangi na kilo mmoja ya Indian hemp, polisi inasema. Mvinyo uliochanganywa na bangi, zaituni, kahawa, na samaki aina ya tuna pia vilikusanywa nyumbani mwake karibu na Catania huko Sicily mashariki. Inaarifiwa mpishi huyo aliwaeleza maafisa wapolisi kwamba alikuwa anajaribu 'viungo vipya vya upishi'. Chiaramonte amesema yeye ni mshauri wa vyakula asili kwa upishi wa kileo ", gazeti la Italia La Sicilia limeripoti. Mpishi huyo wa miaka 50, anayeishi katika kijiji cha Trecastagni, chini ya mlima Etna ameachiwa huru huku kesi ikisubiriwa kuwasilishwa. Chiaramonte ni mpishi katika hoteli ya Katane Palace huko Catania. Yeye hupika vyakula vya watu wa Meditarenia kwa mujibu wa maelezo kwenye mtandao wake. Alishir

Bomu la nyuklia la USSR lililoishangaza dunia

Picha
Mapema asubuhi, mnamo 30 Oktoba 1961, ndege ya kuangusha mabomu ya Muungano wa Usovieti aina ya Tu-95 ilipaa kutoka uwanja wa kambi ya ndege za kivita ya Olenya katika rasi ya Kola kaskazini mwa Urusi. Tu-95 ilikuwa ndege kubwa sana yenye injini nne ambayo iliundwa mahsusi kubeba mabomu. Katika mwongo mmoja uliotangulia, Muungano wa Usovieti ulikuwa umepiga hatua sana katika utafiti kuhusu nyuklia. Marekani na USSR zilikuwa zimejipata upande mmoja wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia lakini baada ya vita, kukatokea Vita Baridi. Wasovieti baada ya kujipata wanakabiliwa na taifa pekee lililokuwa na silaha za nyuklia, iliona njia pekee ya kushindana vyema na Marekani ilikuwa ni kuwa na silaha zake za aina hiyo. Tarehe 29 Agosti 1949, Wasovieti walikuwa wamefanyia majaribio silaha yake ya kwanza ya nyuklia kwa jina 'Joe-1' katika eneo ambalo sasa linapatikana Kazakhstan. Walitumia ujuzi uliopatikana kwa kuingia kisiri na kupata taarifa kuhusu mpango wa atomiki wa Marekani. Katik

Picha zinaonyesha sekunde kadhaa kabla ya ndege mbili kuponea kwa tundu la sindano kugongana

Picha
Ndege mbili za abiria zimepigwa picha sekundi tano tu kabla ya ajali kuweza kutokea ambayo imezuiwa kwa kikosi cha maafisa wa uangalizi wa ndege , uchunguzi umebaini. Ajali hiyo ambayo nusra ingetokea ilikuwa ni kati ya ndege aina ya Cessna 208 mnamo Aprili na iliweza kuepukika kwa "tundu la sindano", bodi ya Airprox imesema. Mojawpao ya ndege hizo ilikuwa imetoka kumshusha jamaa aliyeshuka kwa parashuti huko Sibson Aerodrome, karibu na Peterborough nchini Uingereza, huku ndege ya pili ilikuwa ikipelekwa na mwanafunzi aliyekuwa na mwalimu wake. Maafisa wa Kituo cha uangalizi wa ndege waliiambia ndege iliyokuwa juu izunguke eneo hilo mara moja kabla ya kutua. Bodi ya Airprox, inayochunguza matukio ya ajali ambazo huenda zingetokea imegundua kwamba ndege iliyomshusha jamaa kwenye parashuti ilikuwa inakaribia kutua mita 15 juu ya ndege hiyoya pili. Mwalimu wa mwanafunzi rubani huyo alisikia kelele, akaona kivuli cha ndege iliyokuwa juu yao na kuchukua udhibiti wa usukani kutoka

Manchester United: Ole Gunnar Solskjaer amesema kwamba klabu yake 'inaimarika'

Picha
Mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer anasema kwamba kikosi chake chenye wachezaji wa umri mdogo kinaimarika kila uchao ikilinganishwa na vile walivyoanza msimu. United imeshinda mara moja katika mechi zake tano za ligi ya Uingereza na ilihitaji penalti kuishinda klabu ya daraja la kwanza ya Rochdale katika michuano ya Carabao siku ya Jumatano. ''Sijasema kwamba itakuwa rahisi msimu huu'' , alisema mkufunzi huyo wa Man United. Kutakuwa na changamoto. Tunaposhindwa mechi lazima tujiamini na kile tunachofanya''. Kikosi hicho cha Solkjaer ambacho kilishindwa 2-0 na West Ham wikendi iliopita , kitachuana na Arsenal katika uwanja wa Old Trafford siku ya Jumatatu usiku. ''Utamaduni upo, hatuna tatizo na jinsi wachezaji wanachukulia kila mechi, na viwango'' , aliongezea. ''Unaweza kuona dhidi ya Astana na Rochdale, wanataka kucheza vizuri na mara nyengine wanaharakisha mashambulizi yao''. Siku ya Jumanne, klabu hiyo ilitanga

Tetesi za soka Ulaya Alhamis tarehe 26.09.2019: Eriksen, Pochettino, Mandzukic, Kane, Ibrahimovic, Haaland

Picha
Real Madrid inamtaka kiungo wa kati wa Tottenham raia wa Denmark Christian Eriksen, mwenye umri wa miaka 27, kusaini mkataba wa awali mwezi Januari - na baadae atahamia Spurs kwa meneja Mauricio Pochettino.  Tottenham wanahofia Eriksen atakataa mapendekezo ya kumuuza mwezi Januari , hii ikimanisha kuwa anawza kuondoka kwa uhamisho usio na malipo msimu ujao.  Mshambuliaji wa timu ya Juventus Mario Mandzukic alikataa euro milioni 7 alizopewa kwa mwaka kuichezea timu ya Qatar kwa hiyo Mcroatia huyo mwenye umri wa miaka 33 ana fursa ya kujiunga na Manchester United mwezi Januari mwaka ujao. 

Mwanajeshi wa Marekani akamatwa kwa kutoa mafunzo kuhusu namna ya kutengeneza bomu mtandaoni:

Picha
Shirika la FBI limemkamata mwanajeshi wa Marekani kwa kutuhumiwa kusambaza taarifa kupitia mitandao ya kijamii ya namna ya kutengeneza mabomu. Jarrett William Smith anatuhumiwakupendekeza kutumia bomu la kwenye gari kushambulia kituo kikubwa cha habari Marekani. Mwanajeshi huyo mwenye miaka 24 aliandika katika mtandao wa kijamii kwamba angetaka kulipigania kundi la wafuasi wa mrengo wa kulia nchini Ukraine wanedehsa mashtaka wamesema. Alipendekeza kuwa angewaua wafuasi wa kundi la mrengo wa kushoto Antifa, linasema FBI. Alikamatwa mwishoni mwa juma na kushtakiwa kwa kusambaza taarifa zinaozhusiana na silaha za kuangamiza umma. Kwa mujibu wa nyaraka za mahakamani, Smith aliwasiliana tangu 2016 na raia mwingine wa Marekani aliyesafiri kwenda Ukraine kupigana na kundi la utaifa, the Right Sector. Inaarifiwa kuwa Smith alijadiliana na Lang kwenye Facebook kuhusu namna ya kuunda mabomu. "Ni kweli nilipata elimu kuhusu mabomu ya IED kwa siku kadhaa," amesema Smith katika mawasilian

Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 25.09.2019: Mandzukic, Dembele, Tonali, Gerrard, Zaha, Lopes

Picha
Mcroatia Mario Mandzukic Manchester United inapania kumsajili mshambulizi wa Juventus wa miaka 33 Mcroatia Mario Mandzukic na kiungo wa kimataifa wa Ufaransa na Barcelona Ousmane Dembele, 22, Januari Mwakani. (The Independent) Maafisa wa matibabu wa mshambuliaji wa Newcastle na England Andy Carroll, 30, wanahofia mchezaji huyo huenda isiingie uwanjani hadi baada ya Krismasi japo anaendelea kupata nafuu kufuatia jaraha la mguu alilopata. (Telegraph) Mapato ya Man United yaimarika, ina maana gani?Tetesi za soka Ulaya Jumanne tarehe 24.0.2019Ujumbe wa Silva kwa Mendy unachunguzwa Manchester United inafuatilia mchezo wa kiungo wa kati wa Italia wa miaka 19 Sandro Tonali atashiriki mechi ya Brescia dhidi ya Juventus siku ya Jumanne. (Mail) Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amesema meneja wa sasa wa Rangers na nahodha wa zamani wa Reds Steven Gerrard ndiye atakayemrithi atakapiamua kuondoka Anfield. (FourFourTwo)

Wanafunzi 7 wafariki baada kuangukiwa na paa la darasa Kenya:

Picha
Wanafunzi saba wamethibishwa kufariki na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya darasa la shule yao kuporomoka mapema Jumatatu asubuhi viungani mwa jiji la Nairobi nchini Kenya. Jengo la mbao la shule ya msingi ya Precious Talent liliporomoka muda mfupi kabla ya masomo ya siku kuanza. Wanafunzi 50 wamelazwa hospitali kwa ajili ya matibabu katika mji mkuu wa Nairobi, kulingana na msemaji wa serikali Cyrus Oguna. Kituo cha televisheni nchini Kenya NTV kimetuma picha ya ujume wa Bwana Oguna kupitia Twitter akizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio ambapo jengo liliporomoka, akiwahakikishia wazazi kwamba serikali italipia garama ya matibabu ya wanafunzi waliojeruhiwa: Wakati huo huo wanafunzi kadhaa bado wamekwama ndani ya jengo hilo na maafisa wa shirika la msalaba mwekundu wanaendelea na shughuli za uokozi . Mafisa wa zima moto wa Baraza la jiji la Nairobi kwa ushirikiano na Shirika la Msalaba mwekundu wanasaidiana wenyeji kuwaokua watoto waliokwama chini ya jengo hilo. Kamanda

Kipindi cha radio kilichowarudisha nyumbani watoto walionusurika mauaji ya kimbari Rwanda:

Picha
Kutokana na wazo hilo iliamuliwa hatua ya kuanzisha kipindi cha dakika ambacho kitakua kikipeperushwa hewani na Newsday Swahili kikiwalenga wasikilizaji wa Rwanda na mataifa yalio karibu. Kipindi hicho kilianza kwa Taarifa ya Habari na kufuatiwa na sauti za watu wanaowatafuta jamaa zao. Ukweli ni kwamba haikua rahisi kutayarisha kipindi hicho lakini kwa ushirikiano na mashirika yasiokua ya kiserikali kama vile Shirika la Msalaba Mwekundu, Save the Children na Umoja wa Mataifa sauti zilizorekodiwa kutoka kwa wahasiriwa ziliwasilishwa katika studio za Newsday Swahili "Tulipeperusha hewani sauti za watu kutoka kambi hizo za wakimbizi ," anaeleza Mugenzi, ambaye pia alikua mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho kilichokua kikiendeshwa na watangazaji wawili. Hatimaye tulipewa jina la Gahuzamiryango, likimaanisha "muunganishi wa familia" na mara ya kwanza ilitangazwa kwa mara ya kwanza miaka 25 iliyopita. Kipindi hicho kilitarajiwa kumalizika baada ya miezi mitatu. Lakini

Tetesi za soka Ulaya Jumatatu tarehe 23.09.2019: Xavi, Keane, Mourinho, Balotelli, Sottil, Hysaj

Picha
Kiungo wa kati wa zamani wa Barcelona Xavi, ambaye ni meneja wa timu ya Qatari ya Al-Sadd, anasema kuwa itakuwa ni tatizo kwake kuwaongoza wachezaji wenzake wa zamani kama vile Lionel Messi, Luis Suarez na Sergio Busquets katika Nou Camp.  Kaeni nje ya Ghuba, Iran yaonya vikosi vya kigeniPicha: 'Sekunde kadhaa kabla ya ajali ya ndege'WHO lalalamika ukosefu wa ushirikiano kutoka Tanzania kuhusu Ebola Tottenham imetuma ujumbe kumchukunguza mchezaji wa kimataifa wa timu ya vijana waliochini ya miaka 21 wa Italia winga wa Fiorentina Riccardo Sottil ambaye ni mchezaji wa kiwango cha juu huku wakionyesha nia ya kumchukua kijana huyo mwenye umri wa miaka 20 .  Matumaini ya Chelsea ya kusaini mkataba na mchezaji wa Napoli Elseid Hysaj msimu ujao yanaweza kugonga mwamba huku klabu hiyo ya Italia ikiwa tayari kurefusha mkataba na kijana huyo kutoka Albania mwenye umri wa amiaka 25. (Express) Meneja wa Everton Marco Silva ameutuma ujumbe umchunguze zaidi mshambuliaji wa timu ya RB Leipzig

Abiria 2 Waislamu wasio na hatia 'wasababisha' kukatizwa kwa safari ya ndege Marekani:

Picha
Wanaume wawili Waislamu nchini Marekani wametaka uchunguzi kufanywa baada ya kusema kwamba walibaguliwa kidini katika ndege moja iliokuwa ikielekea mjini Dallas. Abderraoof Alkhawaldeh na Issam Abdallah wamedai kwamba safari yao ilifutiliwa mbali kwa kuwa abiria hawakufurahia kusafiri na wanaume hao. ''Ilikuwa aibu kubwa katika maisha yangu'' , bwana Abdalla aliambia maripota. Taarifa ya kampuni hiyo ya ndege ilisema kuwa wasiwasi uliowakabili abiria wa ndege hiyo ulisababisha kufutiliwa mbali kwa safari ya wawili hao. 'Marekani na washirika wake wote wana jukumu la kutilia maanani usalama na wasiwasi wa kiusalama wa wafanyakazi na abiria'' , ilisema katika taarifa. Ni nini kilichotokea katika ndege? Bwana Alkhawaldeh na bwana Abdallah walitoa madai hayo katika mkutano na vyombo vya habari ulioandaliwa na baraza la uhusiano wa Waislamu wa Marekani na kutangazwa katika mtandao wa Facebook. Mnamo tarehe 14 mwezi Septemba, wanaume wote wawili waliorodheshwa mio

Fatma Karume aapa kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa kumvua uwakili:

Picha
Wakili wa Tanzania fatma karukme aliyevuliwa uwakili siku ya Ijumaa ameapa kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo alioutaja kua kinyume na sheria. Akizungumza kwa njia ya simu na Newsday Swahili Bi karume alisema kwamba Jaji wa mahakama aliyetoa uamuzi huo hakufuata taratibu yoyote kabla ya uamuzi huo huo. Alisema kwamba pia atakwenda katika kamati ya mawakili ili kutoa malalamishi yake kuhusu uamuzi huo ambao anasema kwamba unakiuka haki zake za kisheria. Hakunipa haki yangu ya kusikilizwa , hakunipa notisi yoyote ili kusikiliza malalamishi kuhusu wakili wangu , amevuruga kabisa sheria, alisema bi karume ambaye ni ,mtetezi wa haki za kibinaadamu mbali na kuwa wakili wa kikatiba. ''Eti pia kaamua kwamba Ado Shaibu amlipe fidia rais Magufuli inawezekanaje hiyo ilihali rais anatetewa na wakili mkuu ambaye analipwa na kodi ya mwananchi''. Hatahhivyo wakilki huyo amesema kwamba hashangazwi na uamuzi uliotolewa kwa kua hata aliyekuwa mbunge wa singida mashariki Tundu Lissu hakupat

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?

Picha
Uganda imesaini makubaliano na Urusi kuisaidia kujenga uwezo wake wa kutumia teknolojia ya nyuklia kwa matumizi ya kutengeneza nishati, dawa na matumizi mengine ya amani. Hatua hii inafuata kusainiwa kwa makubaliano mnamo mei mwaka jana baina ya serikali ya rais Yoweri Museveni na shirika la kitaifa la nyuklia China CNNC, kulisaidia taifa hilo la Afrika mashariki kuendeleza matumizi ya nishati ya nyuklia kwa madhumuni ya amani. Katika ujumbe rasmi wa wizara ya nishati Uganda, makubalinao hayo na Urusi yalisainiwa hapo jana Jumatano huko Vienna kati ya waziri Irene Muloni na naibu mkurugenzi mkuu wa shirika la kitaifa la nishati ya atomiki ROSATOM, Nikolai Spasskiy. Urusi itaisaidia Uganda kujenga miundo mbinu ya nyuklia kwa matumizi katika viwanda sekta ya afya na pia ukulima. "Spasskiy ameeleza uwajibikaji na utayari wa ROSATOM kuisaidia Uganda kuidhinisha matumizi ya amani ya nishati ya nyuklia hususan katika ujenzi wa kinu cha nishati ya nyuklia," taarifa imeeleza. Kwa muj

Tetesi za soka alhamisi barani ulaya:

Picha
Manchester United inatumai kumshawishi mchezaji wa kiungo cha kati mwenye umri wa miaka 26 Paul Pogba kusaini mkataba mpya. Mchezaji wa kiungo cha kati wa England Jesse Lingard, mwenye umri wa miaka 26, na mchezaji wa kiungo cha mbele wa miaka 17 anayeichezea timu ya taifa ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21 Mason Greenwood pia wameorodheshwa kwa mikataba mipya.  Mashabiki wenye hasira wa Real Madrid wametaka Zinedine Zidane afutwe kazi kama meneja wa timu hyo baada ya Paris St-Germain kuitandika kichapo katika mechi ya ligi ya mabingwa  Juventus imekataa fursa ya kumsajili Dani Alves msimu huu wa joto kabla ya mlinzi huyo mwenye miaka 36 kujiunga na Sao Paulo katika uhamisho wa bure. 

Majaliwa amsimamisha mhandisi Morogoro, ampa maagizo RC:

Picha
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kasimu Majaliwa leo Jumatano anakamilisha ziara ya siku tano mkoani Morogoro. Tangu alipoanza hadi leo amekwisha kuwasimamisha watumishi 15 wa Halmashauri ya Kilombero, Mji Ifaraka na Ulanga pamoja na Mhandisi wa Ujenzi wa wilaya ya Morogoro.

Erick Kabendera: Mwandishi anayeshikiliwa Tanzania afanyiwa vipimo:

Picha
Mwandishi wa habari za uchunguzi nchini Tanzania, Erick Kabendera, anayetuhumiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi, ameieleza mahakama nchini humo kuwa ameanza kupelekwa hospitali. Kabendera alionekana akiuvuta mguu wake, na kuwa kwenye maumivu wakati alipopandishwa kizimbani Septemba 12, na mawakili wake kuiambia mahakama kuwa mteja wao ana matatizo ya kupooza mguu wa kulia na pia kupumua kwa shida. Hii leo kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, Kabendera amethibitisha kuwa jana Jumanne Septemba 17, 2019 alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Amana na amefanyiwa kipimo cha X Ray kwenye mgongo pamoja na kipimo cha damu. Nashukuru jana nilifanikiwa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Amana na nilifanyiwa kipimo cha X Ray kwenye mgongo wangu na majibu yametoka," amedai Kabendera. Kabendera amedai alikuchukuliwa kipimo cha damu na majibu yake bado hajapewa, na yanasubiriwa ilia aanze matibabu. Pia ameieleza mahakama kuwa bado ana maumivu makali katika mguu wake. Upande wa mashataka umedai kuwa bado haujak

Tetesi za soka jumanne barani Ulaya:

Picha
Klabu ya Celtic ya Uskochi inaweza kujaribu kumsajili kiungo wa klabu ya Tottenham na Kenya Victor Wanyama, 28, mwezi Januari, kwa mujibu wa kocha wa klabu hiyo Neil Lennon. Wanyama aliwika na Celtic kabla ya kutimkia England, na sasa kocha wa Tottenham ameshaeleza kuwa hana haja naye. Winga wa Chelsea na Brazil Willian anataka kusalia kwenye uga wa Stamford Bridge, lakini klabu hiyo hata hivyo bado haijampatia nyota huyo mwenye miaka 32 mkataba mpya.  Beki wa Ajax na Uholanzi Joel Veltman, 27, amebainisha kuwa alitaka kujiunga na klabu ya West Ham United ya England katika dirisha la usajili lililopita lakini mabingwa hao wa Uholanzi hawakumruhusu kuindoka.

America: Wezi waiba choo cha dhahabu

Picha
Choo cha dhahabu chenye karati 18 kimeibwa katika wizi wa mabavu usiku wa kuamkia leo katika Jumba la Blenheim Genge moja lilivunja na kuingia katika kasri la Oxfordshire na kuiba kiti hicho , kulingana na maafisa wa polisi wa Thames Valley. Kiti hicho kwa jina America , ambacho wageni wameombwa kukitumia hakijapatikana lakini mzee mmoja mwenye umri wa miaka 66 amekamatwa Wizi huo ulisababisha uharibifu mkubwa kwa kuwa choo hicho kilikuwa kimejengwa kushikana na msingi wa nyumba hiyo, polisi walisema. Kilikuwa miongoni mwa vitu vya maonyesho ya msanii mmoja wa Itali Maurizio Cattelan yaliofunguliwa siku ya Alhamisi. Jumba hilo ni la karne ya kumi na nane na eneo alilozaliwa Sir Winston Churchill. Kwa sasa limefumngwa huku uchunguzi ukiendelea. Akizungumza mwezi uliopita nduguye wa kambo wa Churchil , Edward Spencer alisema kwamba hakuwa na shaka kuhusu usalama wa choo hicho. ''Sio kitu cha rahisi kufikiria'' Wageni katika jumba hilo la maonyesho walikuwa huru kutumia vi

Mambo matano ya kujifunza katika Safari ya Papa barani Afrika:

Picha
Papa Francis ameongoza mamia ya watu ya mataifa matatu alipotembelea Afrika ikiwa ni ishara ya kukua kwa kanisa Katoliki barani humo. Hii ilikuwa ni ziara yake ya nne tangu alikuwa papa mwaka 2013. Mtangulizi wake Papa Benedict wa XVI alizuru mara mbili Afrika katika kipindi cha uongozi wake wa kanisa hilo. Mhariri wa dini wa Newsday Swahili aliambatana na Papa Francis katika ziara yake nchini Msumbiji, Madagaska na Mauritius. 1) Upendo kwa maskini Hii ilikuwa fursa ya Papa kubadilisha mawazo na kupumzika. Kwani mwaka huu umekuwa wa matukio mengi ambayo yalihatarisha mienendo ya viongozi wa kanisa hilo tangu mwezi Februari. Hii ilifuatia shutuma za uzalilishaji wa kingono ambazo zimemkabili kadinali George Pell ambaye pia alikutwa na hatia. Pell ameshitakiwa kifungo cha miaka sita jela kutokana na kukutwa na hatia. Safari yake Papa barani Afrika , lengo ni kusaidia wahitaji. Shirika la chakula la umoja wa mataifa linasema 80% ya raia wanaoishi nchini Msumbiji hawawezi kukidhi mahitaji

Ebola: Tanzania yasema wanaoeneza uvumi kuchukuliwa hatua:

Picha
Serikali ya Tanzania imefutilia mbali uvumi kwamba kuna visa vya ugonjwa wa Ebola nchini humo. Waziri wa afya nchini humo bi Ummy Mwalimu aliambia mkutano na wanahabari mapema leo kwamba hakuna kisa hata kimoja cha ebola katika taifa hilo. Kumekuwa na tahadhari na madai ya kuwepo kwa kisa cha ebola nchini humo. Washinda tuzo Shirika la Afya Duniani WHO lilituma kundi la wataalamu kuchunguza kisa cha ugonjwa usiojulikana na ubalozi wa Marekani ulifuatilia hatua hiyo kwa kutoa tahadhari . Hatua hiyo ilisababisha uvumi katika mitandao ya kijamii kwamba ugonjwa huo hatari umeingia nchini Tanzania. Alisema kwamba taifa hilo limejiandaa kukabiliana na mlipuko wowote wa ugonjwa na tayari limefanya majarabio ili kujua jinsi ilivyojiandaa huku ikiweka tayari vituo vya kuwatenga waathiriwa. Waziri huyo pia alionya kwamba wale ambao wataendelea kusambaza uvumi huo wa uwongo kuhusu kisa hicho watachukuliwa hatua kali za kisheria kupitia sheria ya uhalifu wa mtandaoni. Uvumi wa visa vya ebola nchin

Ebola: Tanzania yasema wanaoeneza uvumi kuchukuliwa hatua

Picha
Serikali ya Tanzania imefutilia mbali uvumi kwamba kuna visa vya ugonjwa wa Ebola nchini humo. Waziri wa afya nchini humo bi Ummy Mwalimu aliambia mkutano na wanahabari mapema leo kwamba hakuna kisa hata kimoja cha ebola katika taifa hilo. Kumekuwa na tahadhari na madai ya kuwepo kwa kisa cha ebola nchini  Washinda tuzo Shirika la Afya Duniani WHO lilituma kundi la wataalamu kuchunguza kisa cha ugonjwa usiojulikana na ubalozi wa Marekani ulifuatilia hatua hiyo kwa kutoa tahadhari . Hatua hiyo ilisababisha uvumi katika mitandao ya kijamii kwamba ugonjwa huo hatari umeingia nchini Tanzania. Utambuzi wa watu ambao mgonjwa aliwasiliana nao umekwisharipotiwa kwa njia isiyo rasmi na "wamewekewa karantini." Hakuna taarifa za ziada zilizopo. Mahali ambapo mgonjwa alibainika kukutana na watu wengine hakujajulikana . Shirika hilo la afya dunianin linasema kuwa tarehe 11 Septemba 2019, WHO lilipokea ripoti ambazo hazikuwa rasmi kuhusu mfanyabiashara kutoka Mwanza ambaye alikuwa na dalil