Siku kama ya leo 2007 ni Kumbukumbu kwa hayati Lucky Philip Dude aliyepigwa risasi hadi kufa na wezi Wa magari Sifiso Mhlanga,Julio Shilindza na Mbuti Mabe.
Toa Hisia kwa nyimbo zake zilizosifika kwa kuandika na kushare kwenye comments na watu wote Duniani wanaotumia siku hii ya Leo kumkumbuka Mfalme Wa Reggae Afrika.
Viongozi wa nchi za Umoja wa Ulaya hatimaye Jumanne asubuhi walifikia makubaliano ya yuro bilioni 750 za kuufufua uchumi wao. Pesa hizi ni za kukabiliana na athari zilizotokana na janga la virusi vya corona. Viongozi hao walioonekana wenye uchovu wamekubaliana bajeti ya yuro trilioni 1.82 pia pamoja na hizo pesa za kufufua uchumi baada ya janga la virusi vya corona. Hatua hii imefikiwa kufuatia majadiliano ya siku nne ya usiku na mchana yaliyojawa na makabiliano na ubishi mkali kuhusiana na pesa na nguvu katika mojawapa ya mkutano wao mrefu zaidi wa kilele kuwahi kushuhudiwa. Hizo bilioni 750 zitatolewa kama mkopo kwa nchi zilizoathirika vibaya zaidi na janga hilo huku makubaliano yakiafikiwa pia kuhusiana na bajeti hiyo ya miaka saba ya zaidi ya trilioni moja. Mkutano ulitarajiwa kuisha Jumamosi Charles Michel ni mwenyekiti wa mkutano huo wa kilele. "Tumeonyesha imani kwa mustakabali wetu na makubaliano haya yanaonyesha kuwa Ulaya ni nguvu ya vitendo. Tumejadiliana
Serikali ya Uganda imeaandaa maonyesho ya picha kuhusu raisi wa zamani Field Marshal Idi Amin Dada ambaye anadhaniwa kuwa ni mmoja wa madikteta hatari duniani. Hata ivyo maonyesho haya yanalenga kuonesha taswira tofauti na kuangazia mazuri aliyoyafanya. Je ni nini mtazamo wako kuusu hatua hii iliyochukuliwa na Serikali ya Uganda? Toa maoni yako Kuhusu hilii
Uganda imesaini makubaliano na Urusi kuisaidia kujenga uwezo wake wa kutumia teknolojia ya nyuklia kwa matumizi ya kutengeneza nishati, dawa na matumizi mengine ya amani. Hatua hii inafuata kusainiwa kwa makubaliano mnamo mei mwaka jana baina ya serikali ya rais Yoweri Museveni na shirika la kitaifa la nyuklia China CNNC, kulisaidia taifa hilo la Afrika mashariki kuendeleza matumizi ya nishati ya nyuklia kwa madhumuni ya amani. Katika ujumbe rasmi wa wizara ya nishati Uganda, makubalinao hayo na Urusi yalisainiwa hapo jana Jumatano huko Vienna kati ya waziri Irene Muloni na naibu mkurugenzi mkuu wa shirika la kitaifa la nishati ya atomiki ROSATOM, Nikolai Spasskiy. Urusi itaisaidia Uganda kujenga miundo mbinu ya nyuklia kwa matumizi katika viwanda sekta ya afya na pia ukulima. "Spasskiy ameeleza uwajibikaji na utayari wa ROSATOM kuisaidia Uganda kuidhinisha matumizi ya amani ya nishati ya nyuklia hususan katika ujenzi wa kinu cha nishati ya nyuklia," taarifa imeeleza. Kwa muj
Maoni
Chapisha Maoni