Virusi vya corona: Tanzania imethibitisha wagonjwa wapya 196
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
Wagonjwa wa virusi vya Corona nchini Tanzania wafikia 480
Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa ametangaza ongezeko la wagonjwa 196 wa virusi vya corona nchini humo.
Idadi hiyo sasa ndio kubwa zaidi kushinda taifa lolote lile la Jumuiya ya Afrika mashariki.
Kati ya wagonjwa hao 174 wanatoka Tanzania Bara huku 22 wakitoka kisiwani Zanzibar (ambao tayari taarifa zao zilishatolewa na waziri wa Afya wa visiwa hivyo siku ya Jumanne).
Akizungumza na vyombo vya habari bwana Majaliwa pia ametangaza idadi ya vifo kufikia 16 ikiwa ni ongezeko la watu 6 zaidi.
Vilevile amekuwa na habari njema kwa Watanzania akisema kwamba idadi ya waliopona imeongezeka kutoka 48 hadi 167.
Tanzania kwa sasa inaongoza Afrika Mashariki kwa idadi ya wagonjwa ikifuatiwa na Kenya yenye wagonjwa 374, Rwanda 207, Uganda 79, Sudani Kusini 34 na Burundi 15.
Mji wa kibiashara wa Dar es salaam umetajwa kuongoza kwa idadi ya maambukizi nchini humo.
Licha ya mji huo kuwa kitovu cha maambukizi, Magufuli amesema jiji hilo la watu milioni sita ndio moyo wa mapato ya Tanzania.
"Wapo wengine wanatoa mawazo ya kuifunga Dar es Salaam, hili haliwezekani. Dar es salam ndio centre (sehemu) pekee ambapo collection (makusanyo) ya revenue (mapato) inapatikana kwa nchi yetu...Zaidi ya asilimia 80 ya mapato yanakusanywa Dar es Salaam," alisema Magufuli alipokutana na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hiyo.
Pia alisisitiza kuwa kutokana na wingi wa wakaazi wake, ilikuwa ni jambo la kutegemewa kitakwimu kwa jiji hilo kuwa na wagonjwa wengi zaidi.
WHO yaikosoa Tanzania
Hatua hiyo inajiri baada ya shirika la Afya Duniani WHO kuikosoa Tanzania kwa kuchelewa kuchukua hatua za mapema kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa huo.
Mkuu wa WHO wa bara la Afrika Bi Matshidiso Moeti alisema tarehe 24 Aprili kuwa kumekuwa na hofu juu ya kukua kwa kasi ya maambukizi katika taifa hilo la Afrika Mashariki.
"Kwa hakika tumeona kuwa watu kuacha kutangamana, pamoja na kupiga marufuku kwa mikusanyiko ya watu wengi kumechukua muda mrefu kufanyika na tunaamini kuwa hayo yanaweza kuwa ni moja ya mambo yaliyosababisha ongezeko la kasi la wagonjwa wa corona," alisema Dkt Moeti katika mkutano na wanahabari.
Hatuazilizochukuliwa kudhibiti maambukizi ni zipi?
Shule zote na vyuo vya elimu vimefungwa mpaka itakapotangazwa ili kuzuia kuenea kwa maambukizi ya corona nchini humo.
Pamoja na kuzuia mikusanyiko yote ya watu wengi yakiwemo matamasha ya muziki, mikutano ya hadhara mbalimbali ikiwemo ya kisiasa.
Magari ya usafiri wa umma hatayakiwi kujaza abiria, na wote lazima wawe wameketi vitini.
Ndege za abiria zimezuiwa kutua nchini humo.
Kuanzia Jumatatu ya Aprili 20 ni lazima kwa wakaazi wote wa Dar es Salaam kuvaa barakoa wanapokuwa maeneo ya umma.
Biashara zote za chakula jijini Dar es Salaam zinatakiwa kufunga bidhaa zao na kutoruhusu watu kula kwenye migahawa.
Ramani ya Coronavirus: Kasi ya kusambaa kwa virusi 22 Aprili 2020
Maelezo haya yanatokana na data za mara kwa mara kutoka Chuo kikuu cha Johns Hopkins na huenda yasiangazie hali halisi ya mambo yalivyo katika kila nchi.
CHANZO CHA PICHA, AFP Maelezo kuhusu taarifa Author, Watu wengi huko Somaliland wanaamini kwamba Marekani, chini ya rais ajaye Donald Trump, itakuwa nchi ya kwanza duniani kuitambua jamhuri hiyo iliyojitangazia uhuru wake. Eneo hilo lilijitangazia uhuru miaka 33 iliyopita baada ya Somalia kutumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. "Donald ni mwokozi wetu. Ni mtu mwenye hekima. Mungu ibariki Marekani," anasema mwanafunzi wa chuo kikuu Aisha Ismail. Anazungumza nami kutoka Hargeisa, mji mkuu wa Somaliland - jiji lililo umbali wa kilomita 850 (maili 530) kaskazini mwa Mogadishu, Somalia. Kwa wale walio Mogadishu, Somaliland ni sehemu ya Somalia. "Nina shaka kwamba Donald Trump anaijua Somaliland ni nini, au iko wapi," anasema Abdi Mohamud, mchambuzi huko Mogadishu. Pia unaweza kusoma Wakuu wa jeshi la Ethiopia-Somaliland wakutana huku kukiwa na mvutano wa kikanda 9 Januari 2024 Makubaliano ya Ethiopia na Somaliland yatikisa diplomasia katika Pembe ya Afrika 9 Janu...
Michezo Imepakiwa mnamo 11:37 PSG v Man City: Je Messi kumaliza zimwi la ukame wa magoli dhidi ya kikosi cha Pep Guardiola leo? Ulikuwa ni uhusiano wenye mafanikio makubwa zaidi wa kocha na mchezaji wake katika nyakati za soka la sasa. Tetesi za soka Ulaya Jumanne 28.09.2021: Phillips, Rice, Porro, Kessie, Isco, Jovic, Davies, De Ligt CHANZO CHA PICHA, JUSTIN TALLIS/GETTY IMAGES Manchester United imeamua kuelekeza nguvu zake kwa kiungo wa Leeds United Kalvin Phillips, 25, baada ya kuachana na mipango yao ya kumsajili kiungo mwenzake wa England Declan Rice, 22, kutoka West Ham. (Star) West Ham ina mpango wa kumuuza Rice kwa dau la £90m ikijiandaa na dau la kumpata mrithi wake. (Football Insider) Real Madrid wanafikiria kupeleka ofa kwa ajili ya mlinzi wa pembeni wa Hispania Pedro Porro, 22, ambaye yuko kwa mkopo Sporting Lisbon akitokea klabu ya Manchester City. (O Jogo - in Portuguese) Follow us on Facebook Follow us on Instagram Follow...
CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES Hivi karibuni nchi za Ulaya, Marekani na Canada zimekuwa zikitangaza hatua ya kukata misaada dhidi ya Rwanda, kufuatia kile kinachoelezwa na nchi hizo za Magharibi kwamba inaunga mkono kundi la M23 liloteka maeneo ya mashariki mwa DRC, ikiwemo miji ya Goma na Bukavu. Nchi hizo zinaituhumu Rwanda kuchochea ghasia katika eneo la Mashariki mwa DRC kwa kuwaunga mkono waasi wa kitutsi wa Congo wa kundi la M23, tuhuma zinazokanushwa vikali na Rwanda. Lakini je, Rwanda inaweza kujitegemea bila misaada? Kujibu swali hili ni vyema kuelewa ni kwa namna gani Rwanda inategemea misaada kutoka mataifa ya kigeni kwa ajili ya kuendesha uchumi wake. Kulingana na takwimu za Benki ya Dunia, Rwanda ilikadiriwa kutegemea kwa kiasi kikubwa misaada ya kigeni mnamo 2024, huku makadirio yakionyesha kuwa misaada na mikopo kutoka nje inaweza kuchangia na karibu 27% ya jumla ya bajeti ya taifa hilo. Inakadiriwa kuwa Rwanda inapokea zaidi ya dola bilioni 1 ya msaada wa kigeni Pia una...
Maoni
Chapisha Maoni