Rais wa Sierra Leone atangaza kujitenga baada ya mlinzi wake kuthibitishwa kuwa na Coronavirus

Mlinzi wa Rais wa Sierra Leone Julius Maada Bio ameambukizwa virusi vya corona.

Rais wa nchi hiyo alitangaza siku ya Jumatatu usiku kuwa ana afya njema ingawa mfanya kazi wake ana maambukizi.

Amesema pia familia yake yote iko salama na hakuna aliyeonesha dalili za kuwa na maambukizi ya virusi vya corona.

Rais Bio atakaa karantini kwa siku 14 kwasababu alikuwa karibu na mlinzi wake, kwa mujibu wa mwandishi wa Newsday Swahili

Sierra Leone mpaka sasa ina wagonjwa 43 wa virusi vya corona.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Kwanini Somaliland ina matumaini na ujio wa Trump?

Rwanda bila misaada: Je, inaweza kujitegemea?

Ubalozi wa Marekani: Hatutasita kuwachukulia hatua watakaovuruga au kukwaza demokrasia Tanzania