MAREKANI: CORONA VIRUS YAGHARIMU MAISHA YA WATU 2000 NDANI YA SIKU MOJA

Watu 2,018 wamefariki dunia kutokana COVID-19 ndani ya siku moja, idadi hiyo ya vifo ni kubwa zaidi kurekodiwa duniani

Huenda nchi ya Marekani yenye waathirika 503,177 na vifo 18,761 hadi sasa ikaipiku Italia ambayo imerekodi vifo 18,849 kufikia leo kwa kuwa na vifo vingi zaidi

Licha ya ongezeko hilo la vifo, Wataalamu wa Kikosi Kazi cha COVID-19 kutoka Ikulu wanasisitiza kuwa makali ya mlipuko huo yameanza kupungua

Rais Donald Trump naye amesema anatarajia kuona vifo vichache zaidi vikirekodiwa tofauti na makadirio yaliyotolewa awali

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?