KOREA KUSINI: WAGONJWA 91 WALIOPONA COVID-19 WAPATA MAAMBUKIZI

Mamlaka za Korea Kusini zimeripoti kuwa takriban watu 91 waliopona Corona Virus wamepata maambukizi kwa mara ya pili

Mkurugenzi wa Kituo cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa nchini humo, Jeong Eun-kyeong amesema kuna uwezekano mkubwa virusi hivyo vilikuwa vimelala (dormant) na sio kwamba watu hao wameambukizwa upya

Aidha, Wataalamu wanasema huenda vipimo walivyofanyiwa watu hao vilionesha majibu ya uongo au baadhi ya virusi vilibaki mwilini ila havikuwa na madhara

Hata hivyo, Wataalamu wa Afya wa Korea Kusini bado hawajafahamu kinachosababisha hali hiyo na undani wa jambo hilo unaendelea kuchunguzwa

Hali ya wagonjwa wa Corona kupata maambukizi baada ya kupona ni suala ambalo linahofiwa kimataifa kwakuwa nchi nyingi zinatamani walioathirika watakuwa na kinga ya mwili ya kutosha itakayowazuia kuambukizwa tena

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?