KOREA KUSINI: WAGONJWA 91 WALIOPONA COVID-19 WAPATA MAAMBUKIZI
Mamlaka za Korea Kusini zimeripoti kuwa takriban watu 91 waliopona Corona Virus wamepata maambukizi kwa mara ya pili
Mkurugenzi wa Kituo cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa nchini humo, Jeong Eun-kyeong amesema kuna uwezekano mkubwa virusi hivyo vilikuwa vimelala (dormant) na sio kwamba watu hao wameambukizwa upya
Aidha, Wataalamu wanasema huenda vipimo walivyofanyiwa watu hao vilionesha majibu ya uongo au baadhi ya virusi vilibaki mwilini ila havikuwa na madhara
Hata hivyo, Wataalamu wa Afya wa Korea Kusini bado hawajafahamu kinachosababisha hali hiyo na undani wa jambo hilo unaendelea kuchunguzwa
Hali ya wagonjwa wa Corona kupata maambukizi baada ya kupona ni suala ambalo linahofiwa kimataifa kwakuwa nchi nyingi zinatamani walioathirika watakuwa na kinga ya mwili ya kutosha itakayowazuia kuambukizwa tena
Mkurugenzi wa Kituo cha Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa nchini humo, Jeong Eun-kyeong amesema kuna uwezekano mkubwa virusi hivyo vilikuwa vimelala (dormant) na sio kwamba watu hao wameambukizwa upya
Aidha, Wataalamu wanasema huenda vipimo walivyofanyiwa watu hao vilionesha majibu ya uongo au baadhi ya virusi vilibaki mwilini ila havikuwa na madhara
Hata hivyo, Wataalamu wa Afya wa Korea Kusini bado hawajafahamu kinachosababisha hali hiyo na undani wa jambo hilo unaendelea kuchunguzwa
Hali ya wagonjwa wa Corona kupata maambukizi baada ya kupona ni suala ambalo linahofiwa kimataifa kwakuwa nchi nyingi zinatamani walioathirika watakuwa na kinga ya mwili ya kutosha itakayowazuia kuambukizwa tena
Maoni
Chapisha Maoni