Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2019

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 01.10.2019: Martinez, Coman, Smalling, Brewster, Darmian, Kral

Picha
Wachezaji wa Barcelona walikuwa tayari ku saini mkataba na mshambuliaji wa PSG Neiymar ,27, msimu huu hali ya kwamba walikuwa tayari kuona mishahara yao ikipunguzwa kuhakikisha uhamisho huo unafanikiwa , kulingana na beki Gerrard Pique.  Manchester City ni miongoni mwa klabu zinazomnyatia mshambuliaji wa Steaua Bucharest raia wa Romania mwenye umri wa miaka 21 Florinel Coman.  Manchester United ina hamu ya mshambuliaji wa Inter Milan mwenye umri wa miaka 21 raia wa Argentina Lautaro Martinez - Mshambuliaji huyo atagharimu Yuro milioni 111.  Roma inataka kukamilisha uhamisho wa kudumu wa beki wa kati wa Uingereza Chris Smalling kwa dau la £18m. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 kutoka Man United yuko katika mkopo wa muda mrefu katika klabu hiyo ya serie A.  Liverpool inafikiria uwezekano wa kuchezesha timu mbili katika mashindano mawili tofauti yatakayofanyika siku moja , katika robo fainali ya kombe la Carabao dhidi ya Aston Villa huku timu hiyo pia ikishiriki katika kombe la nusu

Bilionea Mo Dewji azungumza kuhusu siku tisa za kutekwa na watu wasiojulikana Tanzania.

Picha
Bilionea kijana Afrika na mmiliki wa mojawapo ya klabu maarufu ya soka Afrika mashariki Simba SC - Mohammed Dewji amezungumza kwa mara ya kwanza kuhusu sakata lake la kutekwa nyara mwaka jana na namna alivyotishiwa maisha yake nchini Tanzania. Katika mahojiano maalum na ya kipekee Mo ameeleza kuwa kwa kipindi kizima, alihisi kwamba kuna uwezekano mkubwa hatoweza kutoka salama na kuwa mwisho wake wa maisha unakaribia. "Saa 24 za kwanza baada ya kutekwa zilikuwa kama mwezi. Imani ndio kitu kikubwa kilichonisaidia katika kipindi kizima." Katika kuikumbuka siku hiyo, Mo ameeleza: "Walinifunga macho, miguu na mikono kwa siku tisa. Tulikuwa hatuongei sana, walikuwa sio watu wa hapa. "Walikuwa wakinitisha na kuniweka bastola kwenye kichwa na kuniambia wataniua." ameeleza mfanyabiashara huyo. Mwaka jana mwezi Oktoba, Dewji alitekwana watu wasiojulikana mjini Dar es Salaam. Kufunga mlango (wa gari) tu, kugeuka nimekuta watu wanne ambao wamevaa mask nyeupe - wamefunika

China: Daraja la 'kuogofya' lililojengwa kwa kioo limefungwa

Picha
Daraja la kioo katika eneo la Zhangjiajie lilikuwa ndefu zaidi lilipofunguliwa Mkoa mmoja nchini China umefunga maeneo 32 ya kuvutia watalii yaliyojengwa kwa kioo - ikiwa ni pamoja na madaja, njia za kutembea kwa miguu na maeneo ya kujionea kwa umbali mandhari ya kupendeza - ili kutoa nafasi ya uchunguzi wa usalama wa maeneo hayo. Maeneo 24 yaliyojengwa kwa tumia kioo katika mkoa wa Hebei, yamefungwa tangu mwezi Machi mwaka 2018, kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha kitaifa CCTV. Hatua hiyo iliwahi kuripotiwa siku zilizopita. China imeshuhudia ongezeko la ujenzi wa kutumia kioo katika maeneo ya kuvutia watalii kote nchini- lakini ajali zimeripotiwa katika maeneo hayo huku watu wawili wakipoteza maisha. Inakadiriwa kuwa madaraja 2,300 ya vioo yamejengwa China. kwa mujibu wa chombo cha habari cha kitaifa ECNS. Ujenzi wa kutumia kioo katika maeneo ya kuwavutia watalii ni juhudi ya nchi hiyo kuvutia watalii wa ndani ili kuimarisha sekta hiyo ambayo imekuwa ikikua kwa kasi. Daraja la Zha

Human Rights Watch: Yawasilisha malalmishi dhidi ya serikali ya Tanzania kuhusu wakimbizi wa Burundi

Picha
Maafisa wa serikali ya Tanzania walidaiwa kuwalazimisha zaidi ya wakimbizi 200 wanaotafuta hifadhi ambao hawakuwa wamesajiliwa, kurudi nchini Burundi mnamo tarehe 15 mwezi Oktoba mwaka huu Kulingana na shirika la Human Rights Watch maafisa wao walitishia kuwanyima uhalali wao wa kuwepo nchini Tanzania iwapo wangekataa. Hatahivyo mkimbizi mmoja kutoka Burundi anayeishi nchini Tanzania aliyehojiwa na Newsday Swahili na ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kwamba awali kulikuwa na taarifa hizo za kulazimishwa kuondoka lakini kwa sasa wakimbizi wamekuwa wakirudi nyumbani kwa hiari yao. lakini kwa mujibu wa taraifa hiyo ya HRW kurudishwa huko kwa lazima kunafuatia makubaliano ya mwezi Agosti 24 kati ya Tanzania na Burundi ambapo takriban wakimbizi 180,000 wa Burundi nchini Tanzania wanatarajiwa kurudi makwao kwa hiari ama kwa lazima kufikia tarehe 31 Disemba 2019. Shirika la Umoja wa mataifa kuhusu wakimbizi UNHCR lilitoa msaada wa kuwasajili wanaotafuta hifadhi nchini humo chini ya mp

Gumzo mtandaoni lahoji miundo mbinu gani ilipaswa kupewa kipaumbele Tanzania.

Picha
Wakati mvua zikiwa zinaendela kunyesha maeneo mbalimbali nchini Tanzania na kusabisha vifo na uharibifu wa miundombinu na kero kwa wananchi katika makazi yao. Mwishoni mwa wiki mvua hizo zimesababisha kukatika kwa barabara kubwa kadhaa na kusabisha watu kulala njiani kwa zaidi ya siku mbili. Kufikia siku ya jumatatu watu waliofariki kuanzia ijumaa wamefikia 15 mpaka hapo jana katika maeneo ya Tanga, kamanda mkuu wa polisi mjini Tanga amethibiti hilo. Licha ya kwamba maafa ya mafuriko katika taifa hilo sio jambo geni lakini mjadala umeibuka kwa baadhi ya watu kulalamikia juu ya ndege zinazonunuliwa huku barabara bado ni changamoto. Baadhi ya watu wameonekana wakibeza ujio wa ndege mpya wakati ambao watu wanahangaika katika usafiri wa barabara. Huku wengine wakiwa hawaoni umuhimu wa manunuzi ya ndege nyingi huku wananchi wengi wakiwa bado wanatumia usafiri wa barabara. Wengine wakihoji kama rais akiacha kuagiza ndege , je mafuriko hayatakuepo? Madai hayo yakitajwa kuwa mbinu za wapinzani

Abu Bakr al-Baghdadi: Tunachokijua kuhusu uvamizi wa Marekani na mauaji yake Syria

Picha
Rais Donald Trump ametangaza kwamba kiongozi aliyekuwa akijificha wa kundi la Islamic State , Abu Bakr al Baghdad alijiuwa mwenyewe wakati wa uvamizi wa kikosi maalum cha Marekani nchini Syria. Hiki ndicho tunachojua kuhusu operesheni hiyo. Ni wapi na lini ilitekelezwa? Katika tangazo la runinga , bwana Trump alitangaza kwamba gaidi huyo nambari moja duniani amefariki wakati wa uvamizi hatari wa usiku kaskazini magharibi mwa Syria na vikosi maalum vya Marekani. Rais alisema kwamba ndege aina ya helikopta iliokisafirisha kikosi hicho maalum iliondoka kutoka eneo ambalo halikutajwa baada mwendo wa saa kumi na moja saa za Marekani siku ya Jumamosi, wakati yeye na viongozi wengine walikusanyika katika chumba cha Ikulu ya Whitehouse. Ndege zilisafiri kwa muda wa saa moja na dakika 10 kutoka maeneo tofauti, hiuku opetresheni ya ardhini ikifanyika kwa muda wa saa mbili, aliongezea. Maafisa waliambia vyombo vya habari nchini Marekani kwamba mapema siku ya Jumapili nchini Syria, vikosi maalum v

Mgogoro wa Syria: Je Muungano mpya wa Urusi, Uturuki na Syria unaiweka wapi Marekani?

Picha
Rais wa Urusi Vladimir Putin alikutana na mwenzake wa Uturuki Reccep Tayyip Erdogan siku ya Jumanne ili kushinikiza jukumu la Moscow kama mdhamini aliyesalia wa uthabiti wa eneo la kaskazini mwa Syria. Mataifa yote mawili yataanza doria za pamoja ili kusaidia kuweka mpaka mpya unaojulikana kama eneo la usalama. Kwa upande mwingine magari ya vikosi vya jeshi la Marekani ambayo yalikuwa yakiondoka nchini Syria yanarushiwa mboga na uchafu yalipokuwa yakiondoka na kuwaacha washirika wake wa Kikurdi. Uvamizi wa Uturuki nchini Syria na kuondoka kwa wanajeshi wa Marekani kuna athari kubwa kwa Syria na eneo hilo kwa jumla. Baadhi ya athari hizo ni za moja kwa moja huku nyengine zikitarajiwa katika siku za baadaye. Je ni muungano utakaoibuka mshindi? Huo ni ushindi kwa Waturuki, kwa Urusi na serikali ya Syria. Kwanza Uturuki imepata kile ilichokuwa ikitaka: Inaendelea kuwaweka wanajeshi wake pamoja na washirika wake katika eneo hilo ambalo tayari inalidhibiti. Urusi na Syria zinaonekana kukubal

Boeing 787-800 Dreamliner: Tanzania yapokea ndege ya pili aina ya Dreamliner

Picha
Tanzania imepokea ndege nyengine kubwa aina ya Boeing 787 Dreamliner kutoka nchini Marekani. Ndege hiyo ilipokewa na rais John Pombe Magufuli aliyewaongoza mamia ya Watanziania katika uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere . Ndege hiyo ni ya saba kati ya 11 zinazotarajiwa kununuliwa na serikali kufikia mwaka 2022. Uwezo wa ndege ya Dreamliner 787 Inabeba uwezo wa kubeba jumla ya abiria 262 Ndege hiyo pia ina uwezo wa kubeba uzito wa tani 227. Uzito huo unajumuisha chombo, mizigo na mafuta. Sifa yake ni kwamba ina uwezo wa kuhimili hali nzito ya hewa ikiwa kwenye umbali mrefu kwenda juu. Inabeba Lita 101,000 za mafuta na ukubwa wa mita 56.72 sawa na nusu ya uwanja wa mpira wa miguu. Vilvile ndege hiyo ina uwezo wa kutembea kilomita 13620 sawa na saa zaidi 12 hewani bila ya kusimamia Akiwahutubia wananchi muda tu baada ya kutua kwa ndege hiyo , rais Magufuli ameelezea furaha yake ya kufanikiwa kwa mpango wa kuimarisha usafiri wa anga baada ya serikali hiyo ya awamu ya tano kununua ndege h

Waandamanaji 30 wauwawa nchini Iraq

Picha
Kiasi waandamanaji 30 wameuwawa jana Ijumaa wakati wa wimbi jipya la maandamano ya umma yaliyofanyika dhidi ya serikali nchini Iraq. Hayo ni kulingana na Mjumbe wa Kamisheni ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa, Faisal Abdullah, ambaye amesema vifo hivyo vilitokea wakati polisi ilipofyetua risasi za moto na gesi ya machozi kutawanya waandamanaji. Watu 8 waliuwawa kwenye mji mkuu Baghdad, wengine 18 katika miji ya Maysan na Dhi Qar, watatu mjini Basra na mtu mmoja aliuwawa kwenye jimbo la kusini la Muthanna. Kulingana na Abdullah watu wengine zaidi ya 2,300 walijeruhiwa huku takriban majengo 50 ya serikali na ofisi za vyama vya siasa yaliyochomwa moto katika baadhi ya majimbo nchini Iraq. Marufuku ya kutotoka nje imetangazwa kwenye majimbo ya  Dhi Qar, Basra, Muthanna na Wasit.

Tetesi za Soka Ulaya Ijumaa 25.10.2019:Rodwell, Muller, Mourinho, Chilwell, Maddison, Sidibe

Picha
Kiungo wa kati wa Manchester City Jack Roderll,28 , yuko kwenye mazungumzo na Roma kuhusu kuhamia Serie A  Manchester United wanamtolea macho mshambuliaji wa Bayern Munich na Ujerumani Thomas Muller, 30.  Mkurugenzi wa michezo wa Borussia Dortmund Michael Zorc amekana uvumi kuwa kocha wa zamani wa Manchester United na Chelsea Jose Mourinho kuwa ataelekea kwenye klabu hiyo ya Ujerumani.  Manchester United haitarajii kuwasajili Ben Chilwell wa Leicester au James Maddison, 22, mwezi Januari. Monaco haiwezi kumuita tena mlinzi wa timu ya Ufaransa Djibril Sidibe, 27, kutoka Everton anakochezea kwa mkopo, kutokana na tetesi kuwa mfaransa huyo anahusishwa na kuelekea AC milan. Paul Scholes anaamini klabu yake ya zamani Manchester United ijaribu kumsajili mchezaji wa Arsenal Mesut Ozil,31, ili kutatua tatizo la safu ya ushambuliaji  Leicester wanahusishwa na taarifa kuwa wana mpango wa kumsajili kiungo Kerem Baykus,19.  Mkurugenzi wa Wolves sporting Kevin Thelwell anasema uhamisho wa mkopo hau

Tetesi za Soka Ulaya Ijumaa 25.10.2019:Rodwell, Muller, Mourinho, Chilwell, Maddison, Sidibe

Picha
Kiungo wa kati wa Manchester City Jack Roderll,28 , yuko kwenye mazungumzo na Roma kuhusu kuhamia Serie A  Manchester United wanamtolea macho mshambuliaji wa Bayern Munich na Ujerumani Thomas Muller, 30.  Mkurugenzi wa michezo wa Borussia Dortmund Michael Zorc amekana uvumi kuwa kocha wa zamani wa Manchester United na Chelsea Jose Mourinho kuwa ataelekea kwenye klabu hiyo ya Ujerumani.  Manchester United haitarajii kuwasajili Ben Chilwell wa Leicester au James Maddison, 22, mwezi Januari. Monaco haiwezi kumuita tena mlinzi wa timu ya Ufaransa Djibril Sidibe, 27, kutoka Everton anakochezea kwa mkopo, kutokana na tetesi kuwa mfaransa huyo anahusishwa na kuelekea AC milan. Paul Scholes anaamini klabu yake ya zamani Manchester United ijaribu kumsajili mchezaji wa Arsenal Mesut Ozil,31, ili kutatua tatizo la safu ya ushambuliaji  Leicester wanahusishwa na taarifa kuwa wana mpango wa kumsajili kiungo Kerem Baykus,19.  Mkurugenzi wa Wolves sporting Kevin Thelwell anasema uhamisho wa mkopo hau

Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 23.10.2019: Sancho, Alena, Mandzukic, Ibrahimovic, Morelos, Diaz

Picha
Mchezaji wa zamani wa Liverpool wa safu ya kati Dietmar Hamann anasema kuwa amepata fununu kwamba Reds "wanahamu sana" ya kumsajili winga wa Borussia Dortmund na England Jadon Sancho, 19.  Mancheter United huenda ikaongeza juhudi ya kumsajili Mario Mandzukic, 30, baada ya mshambuliaji wa Juventus na Croatia kupunguza masharti ya marupu rupu yake.  Real Madrid imemwambia kiungo wa kati wa zamani wa Manchester City Brahim Diaz, 20, kwamba inataka kumuuza kama sehemu ya kuondokeana nae kabisa.  Mchezaji wa safu ya kati ya Real Isco, 27, amekubali kuwa mmoja wa wachezaji watakaoondoka klabu hiyo mwezi January mwakani.  Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Paris St-Germain na Juventus, Zlatan Ibrahimovic,38, anataka kurejea katika ligi kuu ya Italia, Serie A. Mkataba wa mchezaji huyo wa kimataifa wa zamani wa Uswidi katika klabu ya LA Galaxy unakamilika mwisho wa mwaka huu.  Barcelona imepinga madai kuwa imeilipa Atletico Madrid euro milioni 15 kumaliza mzozo kati yake na

Sochi 2019: Mkutano wa kwanza unaidhinisha kurudi kwa ushawishi wa Urusi Afrika.

Picha
Katika miaka michache iliyopita, Urusi imerudi upya kama nguvu ya kutambuliwa katika bara la Afrika. Ushirikiano mwingi uliokuwepo katika enzi za uliokuwa muungano wa Sovieti ulikatizwa baada ya kuanguka kwa Muungano huo, lakini wakati uhusiano na magharibi ukififia kwa mara nyingine, Kremlin imeidhinisha uhusiano wa kutosha kiuchumi, kiusalama na kisiasa na Afrika. Moscow itajaribu kuimarisha zaidi uhusiano huu wakati wa mkutano wa kwanza baina ya Urusi na Afrika unaofanyika mjini Sochi kuanzia leo tarehe 23 hadi kesho Oktoba 24. ratiba ya mkutano huo ni kujadili nishati, madini na ushirikiano wa kijeshi. Kufikia 2018, biashara ya Urusi na bara la Afrika ilikuwa na thamani ya dola bilioni 20.4, iliyoongezeka mara nne zaidi ya ilivyokuwa 2010. Kumekuwa na tuhuma nyingi kuhusu Urusi kupanua kwa siri uwepo wake kijeshi kwa kuwatumia mamluki katika baadhi ya mataifa ya Afrika na pia kuwatuma wawakilishi na kusambaza taarifa zisizo sahihi katika kampeni ya kushawishi siasa za dai ya nchi.

Zimbabwe: Tembo 55 wafa kwa kukosa maji ya kunywa:

Picha
Tembo 55 wamekufa njaa katika mbuga ya kitaifa ya Hwange, nchini Zimbabwe kutokana na ukame mkali uliokithiri kwa zaidi ya miezi miwili. "Hali ni mbaya," Msemaji wa mbuga hiyo Tinashe Farawo, anasema. "Tembo wanakufa kutokana na ukame na hili ni tatizo kubwa." Ukame umepunguza kwa kiwango kikubwa viwango vya mimea nchini Zimbabwe. Theluthi moja ya watu nchini humo wameripotiwa kukabiliwa na uhaba wa chakula wakati mgogoro wa kiuchumi ukiendelea nchini humo. Mwezi Agosti, ripoti ya Shirika la Chakula Duniani ilisema kuwa watu milioni mbili wako katika hatari ya kukabiliwa na baa la njaa nchini Zimbabwe. Baadhi ya tembo walipatikana katika eneo la mita 50 (yadi) ya maji -kuashiria kuwa walitembea mwendo mrefu bila maji na hatimaye kufa muda mfupi kabla ya kuyafikia. Tembo hao wamesababisha "uharibifu mkubwa" wa mimea katika mbuga ya Hwange, Bw. Farawo alisema. Mbuga hiyo inawahifadhi karibu tembo 15,000 lakini kwa sasa kuna zaidi ya tembo 50,000. Mbuga ya Hw

Utafiti: wanasayansi wanachunguza jinsi saratani 'inavyozaliwa'

Picha
Wanasayansi wa Uingereza na Marekani wameungana kutafuta dalili za mapema za ugonjwa wa saratani katika juhudi za kugundua na kutibu kabla ijitokeze. Wanapanga "kuzalisha" saratani katika maabara ili kubaini muonekano wake "siku ya kwanza". Hii ni moja wa tafiti zinazopewa kipaumbele na muungano huo wa kimataifa wa wanasaya wanaofanya shughuli za ugunduzi wa mapema wa saratani. Kufanya kazi pamoja katika mradi huo kunamaanisha watu wanaougua saratani watafaidika zaidi, unasema muungano huo. Kupiga hatua Kwa pamoja wanasayansi hao wanalenga kufanya uchunguzi kama vile wa damu, pumzi na kupima mkojo ili kuwabaini wagonjwa walio katika hatari zaidi, kuimarisha mbinu ya ugunduzi wa mapema wa saratani na kuangazia kwa jumla dalili zisizonekana za ugonjwa huo. Lakini wamekiri kuwa hatua hiyo "ni kama kutafuta sindani gizani" na huenda ikachukua miaka 30. "Tatizo la msingi ni kwamba hatujawahi kuona jinsi saratani inavyozaliwa katika mwili wa binadamu,"

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 21.10.2019: Sancho, Haaland, Werner, Meunier, Koeman

Picha
Real Madrid inawafuatilia winga wa Borussia Dortmund na England Jadon Sancho, 19 na mshambuliaji wa Norway wa miaka 19- Erling Braut Haaland, anayechezea Red Bull Salzburg.  Meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer anataka kumsajili mshambuliaji wa Ujerumani na RB Leipzig Timo Werner,23 ambaye aliwahi kuhusishwa na tetesi za kujiunga na Liverpool.  Manchester United inajiandaa kumpatia mkataba mpya kiungo wa kati wa Uingereza Angel Gomes, 19, licha ya tetesi kuwa Barcelona inamtaka.  Newcastle United inamfuatilia mshambuliaji wa Lille na Nigeria wa miaka 20 Victor Osimhen.  Meneja wa Chelsea Frank Lampard anataka mshamsmbuliaji wa Ufaransa wa miaka 33, Olivier Giroud, ambaye hajafurahishwa na hatua ya kutojumuishwa katika kikosi cha kwanza aendelee kusalia Stamford Bridge.  Chelsea imemuongeza aongeza mchezaji wa safu ya kati wa Atalanta na Ukraine Ruslan Malinovskyi, 26, katika orodha ya wachezaji amabao huenda wakahamia klabu hiyo msimu ujao wa joto.  Beki wa Paris St-Germain

Rais John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko serikalini

Picha
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi kadhaa serikalini huku akiwapiga kalamu viongozi wengine. Kulingana na taarifa iliotoka katika Ikulu ya Tanzania na kutiwa saini na Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Ikulu ya rais, walioteuliwa ni Mathias Kabunduguru ambaye sasa ndiye mtendaji mkuu wa mahakama ya Tanzania, akichukua nafasi ya Hussein Katanga aliyeteuliwa kuwa balozi. Wengine walioteuliwa ni Godfrey Mweli kuwa naibu katibu mkuu Tamisemi anayeshughulikia elimu. Kabla ya uteuzi huo Mweli alihudumu kama mkurugenzi wa mipango katika wizara ya katiba na Sheria. Hashim Abdallah Komba naye ameteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Nachingwea. Kabla ya Uteuzi huo Komba Komba alikuwa akihudumu kama katibu tawala mkoa wa Iringa. Anachukua nafasi ilioachwa na Rukia Muwango ambaye uteuzi wake umetenguliwa. Vilevile kiongozi huyo wa taifa amemteua Hassan Abbas Rungwa kuwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Nachingwea. Anachukua mahala pake bakari Mohammed Bakari ambaye ameon

Robert Kyagulani maarufu Bobi Wine asema Museveni anaongoza 'kwa mtutu wa bunduki'

Picha
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Bobi Wine amemjibu rais Yoweri Museveni ambaye katika mahojiano na Newsday Swahili alimtaja kuwa adui wa maendeleo nchini humo. Bobi Wine ambaye jina lake kamili ni Robert Kyagulani , hivi majuzi alitangaza kwamba atamkabili bwana Museveni mwenye umri wa miaka 75 katika kinyanganyiro cha urais katika uchaguzi wa 2021. Rais huyo wa Uganda amekuwa madarakani tangu 1986. Bobi Wine atangaza azma yake ya kuwania urais UgandaMwandani wa Bobi Wine afariki Uganda Katika ujumbe wake wa twitter Bobi Wine alimtaja rais huyo kuwa adui wa Uganda ambaye anaongoza kupitia 'mtutu wa bunduki'. Katika mahojiano hayo ya Newsday Swahili , bwana Museveni alidai kwamba msanii huyo wa muziki alikuwa amesema katika ziara yake Marekani kwamba watu hawafai kwenda Uganda na kuwekeza. Lakini mgombea huyo wa urais alisema kwamba Museveni huenda amekuwa akiota ndoto kwa kuwa hajawahi kutoa matamshi kama hayo. Katika taarifa ambayo alisema huenda rais huyo alikuwa akizungum

As Roma kuzungumza na Waswahili kupitia Twitter:

Picha
Klabu ya mpira ya 'As Roma' nchini Italia imekuwa klabu kubwa ya kwanza kutoka barani Ulaya kuanzisha ukurasa wake katika mtandao wa Twitter. Kurasa hiyo ya As Roma itakuwa ikiandika habari zake kwa lugha adhimu ya kiswahili. Ukurasa huo wa lugha ya kiswahili ulizinduliwa rasmi jana, na inaaminika lengo kuu la 'As Roma' ni kuwafikia mamilion ya watu wanatumia lugha ya kiswahili. Akaunti hiyo ya Twitter imezinduliwa siku ya jumatano kwa video yenye maneno ya utani ya kiswahili. Akaunti hiyo imepokelewa vizuri na wasomaji wa kiswahili wa Tanzania na Kenya. Wengi wakiona kuwa ni ubunifu mzuri ambao unaonesha kuwajali mashabiki wanaoongea lugha ya Kiswahili. Idadi kubwa ya watu wameanza kufuatilia kurasa hiyo na kujibu kwa kiswahili. Rais wa klabu hiyo Jim Pallotta ametumia kurasa yake binafsi ya tweeter kuthibitisha kuwa kurasa hiyo imefunguliwa. "Tuna furaha kuzindua kurasa ya kiswahili ya AS Roma", mkuu wa mipango Paul Rogers alieleza. Uzinduzi huo umekuja mara

HPV: Kenya yazindua chanjo dhidi ya saratani ya shingo ya kizazi, ina umuhimu gani?

Picha
Kenya imezindua kampeni ya kitaifa kuwachanja wasichana dhidi ya HPV, kirusi kinachohusishwa kusababisha baadhi ya saratani ikiwemo ya shingo ya uzazi. Ni taifa la 16 barani Afrika kuidhinisha mpango huu wa chanjo dhidi ya HPV. Chanjo hiyo inatolewa kwa watoto wenye umri wa miaka 10 na maafisa wanatumai kuwafikia watoto laki nane katika mwaka wa kwanza wa uzinduzi. Rais Uhuru Kenyatta ameizindua rasmi kampeni hiyo leo katika mji wa Mombasa pwani ya Kenya huku akitoa wito kwa raia kushikilia usukani wa afya zao kwa kuhakikisha wanafanyiwa ukaguzi wa mara kwa mara wa saratani. Kwanini chanjo ya HPV ni muhimu? Saratani ya shingo ya uzazi huwaathiri zaidi ya wanawake nusu milioni kila mwaka na husababisha vifo vya wanawake laki mbili na nusu kwa mujibu wa shirika la afya duniani WHO. Ni mojawapo ya saratani inayowashika wengi hii leo lakini pia ni mojawapo ya saratani inayoweza kuzuilika. Chanjo dhidi ya HPV hulinda usalama dhidi ya maambukizi yanayohusishwa kwa karibu na saratani hiyo, na