Ndege ya Urusi yalazimika kutua kwa dharura baada ya kugongana kundi la ndege

Ndege ya abiria ya Urusi imelazimika kutua kwa dharura kwenye shamba la mahindi karibu na jiji la Moscow baada ya kugonga kundi la ndege.
Watu ishirini na watatu wamejeruhiwa katika tukio hilo, ambalo limesababisha ndege kutua huku injini yake ikiwa imezima na gia yake kutua ikirudi nyuma, wamesema maafisa wa afya.
Ndege hiyo Ural Airlines Airbus 321 ilikuwa ikisafiri kuelekea katika eneo la Simferopol Crimea ilipogonga kundi la ndege muda mfupi baada ya kuondoka uwanjani , hali iliyovuruga utendaji wa injini yake.
Vyombo vya habari vya taifa la Urusi vimetaja kutua kwa ndege hiyo kama "muujiza wa eneo la Ramensk".
Maafisa wa ndege hiyo wamesema ndege imeharibika sana na haiwezi kupaa tena. Uchunguzi rasmi juu ya ajali hiyo unaendelea.
Ndege hiyo ilikwa na abiria 233 na wahudumu ndani yake wakati ndege waliporipotiwa kuingia ndani ya injini na rubani wake akaamua kutua mara moja.
Abiria mmoja ambaye hakutajwa jina lake ameiambia televisheni ya taifa kuwa ndege ilianza kuyumba kwa hali ilisiyo ya kawaida baada ya kuondoka uwanjani.
"Sekunde tano baadae, taa za upande wa kulia za ndege zikaanza kuwaka na kuzima na kulikuwa na harufu ya kuungua. halafu tukatua na kila mtu akatimua mbio kwenda mbali ," alisema.

Wasafiri na wahudumu wa ndege waliondoshwa haraka kutoka eneo la tukio baada ya ndege kutua kwa dharura
Shirika la usafiri wa ndege la Rosaviatsia limesema kuwa ndege hiyo ilitua katika sahamba la mahindi yapata kilomita moja (maili 0.62 ) kutoka kwenye njia yake kwenye uwanja wa kimataifa Zhukovsky , huku injini yake ikiwa imezima na breki zake za kutua zikiwa zimerudi nyuma.
Wasafiri walitolewa kutoka kwenye ndege, huku baadhi wakipelekwa hospitalini kwa matibabu na wengine wakiongozwa kuelekea kwenye uwanja wa ndege.
Wizara ya afya imesema kuwa watoto watano walikuwa miongoni mwa wasafiri waliolazwa kufuatia ajali hiyo.. Wale waliojeruhiwa katika mkasa huo walichukuliwa kama watu wenye "hali mbaya na hali ya kawaida ",imesema.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya ndege ya Ural Airlines Kirill Skuratov amewaambia waandishi wa habari kuwa wasafiri waliotaka kuendelea na safari yao watawekwa kwenye ndege mbadala baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.
Watu zaidi ya 100 wafariki ajali ya ndege Cuba
Kuna uwezekano wa kunusurika ajali ya ndege?
Waethiopia waomboleza waliokufa kwenye ajali ya ndege
Vyombo vya habari vya Urusi vimelinganisha tukio hilo na tukio la safari ya ndege ya Marekani-US Airways iliyolazimika kutua kwa dharura katika mto Hudson muda mfupi baada ya kupaa mnamo mwaka 2009.
Migongano baina ya ndege na ndege ni jambo la kawaida katika safari za anga , huku maelfu ya ajali hizo zikitokea nchini Marekani pekee. Hata hivyo, ni nadra kusababisha ajali au kusababisha uharibifu kwenye ndege

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?