Dawa za kupambana na Ebola zimeonesha ufanisi katika kuokoa maisha ya wagonjwa

Ugonjwa wa Ebola huenda punde ''ukadhibitiwa na kutibika'' baada ya majaribio ya dawa aina mbili zilizoonesha ufanisi.Wanasayansi wameeleza.

Dawa aina nne zilijaribiwa kwa wagonjwa nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambako kuna mlipuko mkubwa wa virusi hivyo.

Dawa aina mbili kati ya nne zimeonekana kufanya kazi vilivyo katika kutibu ugonjwa, utafiti umeeleza.

Dawa hizo sasa zitatumika kutibu wagonjwa wote wa Ebola nchini DR Congo, kwa mujibu wa maafisa wa afya wa nchi hiyo.

Taasisi ya taifa ya utafiti kuhusu uzio na maradhi ya kuambukiza ya nchini Marekani (NIAID), ambao ilidhamini majaribio hayo, imesema matokeo hayo ni ''habari njema'' katika mapambano dhidi ya Ebola.

Dawa hizo kwa jina REGN-EB3 na mAb114, zinafanya kazi ya kuvishambulia virusi vya Ebola kwa kuzipa nguvu chembe chembe za kinga za mwili zinazopambana na maradhi.

Ni ''dawa za kwanza, ambazo kisayansi zimeonesha kuwa muhimu katika kupunguza vifo'' vya wagonjwa wa Ebola, alisema Daktari, Anthony Fauci, Mkurugenzi wa NIAID.

Dawa nyingine aina mbili ZMapp na Remdesivir, zilishindwa kufanya vizuri kwenye majaribio hayo.

Matokeo ya majaribio yalikuwaje?
Majaribo, yaliyofanywa na taasisi ya utafiti na kuratibiwa na Shirika la afya duniani, WHO, yalianza mwezi Novemba mwaka jana.

Tangu wakati huo, dawa aina nne zilijaribiwa kwa wagonjwa 700, huku matokeo ya awali kutoka kwa watu 499 wa kwanza yakifahamika hivi sasa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?