Je ni kweli taasisi ya haki miliki ya muziki Kenya haiwalipi wasanii?

Taasisi ya haki miliki ya muziki nchini Kenya inakabiliwa na shutuma kali kutoka kwa wasanii wa muziki wanaodai limekuwa haliwalipi pesa zao kulingana na kazi yao.

Taasisi hiyo -Music Copyright Society of Kenya ina jukumu la kuwalipa wasanii wa muziki kwa kazi yao, lakini kwa miaka wasanii wa Kenya wamekuwa wakilalamika kuwa haliwalipi ili hali miziki yao inachezwa kwenye redio na televisheni.

Tulipe Pesa zetu, Tafadhali. Yamekuwa ni maneno yanayorudia mara kwa mara kila mara wanamuziki wanapokutana kwa mikutano yao na katika maandamano ya mitaani yanayolenga kupinga kutolipwa na taasisi hiyo. Hata hivyo bado hawajawahi kusikilizwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?