Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2019

Eric Kabendera: Mwandishi wa Tanzania kuendelea kuzuiliwa baada ya mahakama kuahirisha kesi dhidi yake

Picha
Mwandishi wa habari za uchunguzi , Erick Kabendera ataendelea kuzuiliwa jela baada ya Kesi ya uhujumu Uchumi inayomkabili ikuahirishwa hadi Septemba 12 mwaka huu. Hii ni baada ya upande wa Serikali kudai kuwa upelelezi wa Kesi hiyo bado haujakamilika.Wakili wake Jebra Kambole ameiambia Mahakama ya hakimu Mkaazi Kisutu, Dar es Salaam kuwa waleta mashtaka wanapaswa kuhimizwa wakamilishe upelelezi kwa Wakati na kuiomba Mahakama isisitize juu ya Hilo Wakili Kambole pia amesema kuwa afya ya Kabendera ianendelea kuzorota baada ya kupata tatizo la upumuaji inapofika usiku tangu Agosti 21 hali iliyomfanya kushindwa kutembea kwa siku mbili. Aidha ameiomba Mahakama hiyo iliamuru Jeshi la Magereza kumpeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili mtuhumiwa ili aweze kupatiwa vipimo. ''Kwa kuwa mteja wetu hajapata huduma ya matibabu tunaomba Mahakama ielekeze maafisa wa magereza kumpeleka katika hospitali yoyote ya serikali akapimwe '' alisema wakili huyo. Hata hivyo Wakili wa Serikali, Simon

Uganda ya andaa maonyesho ya picha ya Raisi wa zamani ya Field Marshal Idi Amin Dada

Picha
Serikali ya Uganda imeaandaa maonyesho ya picha kuhusu raisi wa zamani Field Marshal Idi Amin Dada ambaye anadhaniwa kuwa ni mmoja wa madikteta hatari duniani. Hata ivyo maonyesho haya yanalenga kuonesha taswira tofauti na kuangazia mazuri aliyoyafanya. Je ni nini mtazamo wako kuusu hatua hii iliyochukuliwa na Serikali ya Uganda? Toa maoni yako Kuhusu hilii

Je marufuku ya plastiki imefaulu Kenya?

Picha
Miaka miwili iliyopita, Kenya iliidhinisha marufuku dhidi ya matumizi ya mifuko ya plastiki nchini. Je imefanikiwa? Mamilioni ya ya plastiki ilitolewa katika maduka ya jumla kila mwaka nchini. Ilichafua mazingira na kuziba mashimo ya maji taka na kusababisha mafuriko wakati wa msimu wa mvua. Utafiti ulioungwa mkono na shirika la mazingira nchini (Nema) umebaini kuwa 50% ya ng'ombe walio karibu na maeneo ya mijini walipatikana na mifuko ya plastiki katika matumbo yao. Hivyo basi baada ya ahadi za miaka mingi kwamba  ingechukua hatua , serikai ilipiga marufuku utengenezaji, uuzaji na usambazaji wa mifuko ya plastiki nchini. Tangu marufuku hiyo, serikali inasema 80% ya idadi ya watu nchini wameacha kutumia mifuko ya plastiki. Licha ya kwamba hili linatia moyo, mifuko inayotumika mbadala imegunduliwa kuwa na madhara kwa mazingira. Yeyote anayepatikana kutengeneza, kuingiza nchini au kuuza mifuko ya plastiki anaweza kutozwa faini ya hadi $40,000 (£32,000) au akabiliwe na kifungo gerezan

Wakulima wa bangi Uganda kulifikia soko la kimataifa

Picha
Wakaguzi kutoka Umoja wa Ulaya (EU) wameidhinisha Uganda kutuma bidhaa za bangi barani Ulaya, gazeti la Daily Monitor linaripoti. Bangi itakayotumwa kwenye soko la Ulaya hata hivyo si kwa matumizi ya starehe kama uvutaji bali ni kwa ajili ya matibabu. Kwa mujibu wa Monitor mainspekta wa bidhaa za matibabu zitokanazo na bangi kutoka Uholanzi walikagua mashamba ya bangi kwenye wilaya za Hima na Kasese kati aya Julai 29 na Agosti 4. Maafisa hao kabla ya kuondoka Uganda waliikabidhi cheti cha kukidhi vigezo kampuni ya Industrial Globus Uganda Ltd kwa kipindi cha Agosti 6, 2019 mpaka Agosti 5, 2020. Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Benjamin Cadet amelithibitishia gazeti hilo kuwa EU wamewapa idhini ya kuasafirisha bangi Ulaya. "Baada ya EU kuthibitisha bidhaa zetu - usafirishwaji na mnyororo wote wa uzalishaji - kuanzia kupanda mpaka kuvuna kwa bangi utafanyika kikamilifu nchini Uganda na kupelekwa kwenye masoko ya Ulaya," Cadet amesema. Takribani kampuni 50 zimeomba kibali Wizara ya A

Hisia kali baada ya watu 8 kukamatwa kufuatia ajali ya gari la mafuta Kagera Tanzania

Picha
Kuna msemo wa kiswahili usemao "Binadamu ameumbwa kusahau" na kiuhalisia jambo hilo halipingiki hata kidogo. Na swali kubwa ni Je, huwa tunajifunza kutokana na makosa? Ni siku chache tu zimepita ambapo Tanzania ilipata janga kubwa la ajali ya moto huko mkoani Morogoro mara baada ya lori la mafuta kuanguka na kuuwa watu zaidi ya 100 na huku majeruhi wengine wakiendelea kupata tiba mpaka hii leo. Chanzo cha vifo hivyo kilitokana na watu kusogelea gari lililoanguka na kuchota mafuta. Na hapo jana ajali nyingine imetokea mkoani Kagera, ambapo lori la mafuta lilianguka wilayani Ngara wakati likiwa linatokea Rwanda kuelekea Dar es salaam na cha kushangaza watu walikimbilia tena kuchota mafuta bila uoga wowote. Kufuatia ajali hiyo ambayo imesababisha kifo cha dereva wa lori, jeshi la Polisi mkoani Kagera limewashikilia watu 8 kwa tuhuma za wizi wa mafuta na kukamata lita 300 za mafuta kutoka mikononi mwa wanakijiji katika wilaya ya Ngara.  Ni vyema tukajiepusha na matukio yoyote yal

Tundu Lissu: Mahakama Kuu Tanzania yakubali kusikiliza hoja za kupinga kuvuliwa ubunge

Picha
Mahakama Kuu nchini Tanzania imekubali kusikiliza hoja za mwanasiasa mwandamizi wa upinzani Tundu Lissu kupinga kuvuliwa ubunge. Lissu, kupitia kaka yake Alute Mughwai amefungua shauri Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam akipinga uamuzi wa Spika Job Ndugai kumfuta ubunge. Hata hivyo, mawakili wa serikali iliweka pingamizi wakitoa hoja nane wakitaka ombi la Lissu kutupiliwa mbali na mahakama. Shauri hilo lipo mbele ya Jaji Sirilius Matupa, ambaye hii leo ameamua kuendelea kusikiliza hoja za Lissu. Lissu alifutwa ubunge wa jimbo la Singida Mashariki Juni 28, 2019 baada ya Spika Job Ndugai kutoa maelezo kuwa hajulikani alipo na hakusaini fomu za maadili. Gazeti la Mwananchi linaripoti kuwa katika kesi hiyo serikali ya Tanzania ina mawakili mawakili 15 dhidi ya wanne wa Lissu. Huu ni mwanzo wa wa hoja na vita ya kisheria mahakamani ambapo upande wa Lissu utapigana kuthibitisha uhalali wake wa kuendelea kusalia na ubunge huku upande wa mawakili wa serikali kuonesha kuwa Spika Ndugai alikuwa s

Sensa Kenya: Kwa mara ya kwanza Afrika watu walio na jinsia mbili wasajiliwa

Picha
Kenya inaandikisha historia barani Afrika kwa kuwajumuisha huntha (watu wanaozaliwa na jinsia mbili) kwenye zoezi la kuhesabu Wakenya. James Karanja, ambaye alilelewa kama msichana hadi akiwa miaka 18, anaeleza masaibu yanayowakumba watu wanaozaliwa na hali kama yake.

Mbwana Samatta ailiza Anderlecht ya Vincent Kompany

Picha
Mabingwa wa ligi ya Ubelgiji Genk waliilaza timu inayoongozwa na mchezaji wa zamani wa Manchester City Vincent Kompany - Anderlecht 1-0 katika siku ya tano ya ligi hiyo ya Jupiler Pro. Baada ya timu hizo mbili kukabiliana , Genk hatimaye ilikuwa kifua mbele katika dakika ya 55. Kiungo wa kati wa klabu hiyo Junya Ito alimpatia pasi murua mshambuliaji wa Genk raia wa Tanzania Mbwana Samatta ambaye hakupoteza wakati na kucheka na wavu. Anderlecht ilijaribu kutafuta bao la kusawazisha , lakini walipata pigo baada ya mchezaji wao Phillip Sandler kuondolewa kunako dakika ya 68 kabla ya nahodha Vincent Kompany pia naye kupandishwa katika machela kunako dakika ya 74 na jeraha. Siku ya Alhamisi, Kompany aliwachilia kazi yake ya ukufunzi wakati wa siku za mechi ili kucheza na badala yake ameamua kuchukua unahodha wa timu hiyo. Klabu hiyo ya Ubelgiji imechukua pointi mbili pekee kati ya 15 katika mechi zake tano za kwanza na hivyobasi kuongeza msururu wao mbaya katika miaka 21. Miongoni mwa wache

Air Tanzania: Mjadala waibuka baada ya ndege ya Tanzania kuzuiliwa Afrika Kusini:

Picha
Hatua ya Mahakama kuu ya nchini Afrika Kusini kuzuilia kuruka ndege ya Air Tanzania imeendelea kuzua mjadala kuhusu chanzo chake. Mpaka sasa Mamlaka nchini Afrika Kusini haijatoa tamko lolote kuhusiana na hatua hiyo. Ndege hiyo ilikuwa inatoka Afrika Kusini kwenda jijini Dar es Salaam. Lakini Kwa mujibu wa balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ndege hiyo imezuiliwa kwa amri ya Mahakama Kuu ya mjini Johannesburg. Ripoti ya baadhi za vyombo vya habari nchini Tanzania zinaashiria kuwa abiria waliokuwa ndani ya ndege ya Air Tanzania iliyozuiliwa kuondoka katika uwanja wa ndege wa Oliver Tambo mjini Johannesburg wametafutiwa usafiri mbadala katika nmashirika mengine ya ndege. Gazeti la Mwananchi linaripoti kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) Ladislaus Matindi amesema ''Kuna safari nyingi zitakazoathiriwa kutokana na kushikiliwa kwa ndege hiyo aina ya Air Bus A220-300'' Bwa. Matindi ameliambia Mwananchi kuwa abiria waliokata tiketi wataarifiwa iwapo kut

Wakazi wa Dar es Salaam wazua gumzo mtandaoni vumbi la Makongo Juu nchini Tanzania

Picha
Mjadala mkali umeibuka katika mitandao ya kijamii nchini Tanzania juu ya wakaazi wa mtaa mmoja jijini Dar es salaam kuhusu vumbi ambalo wakazi hao wanadaiwa kuingia nalo mjini. Picha mbalimbali, maneno, kejeli na mizaha wikii hii vimetawala kwenye mitandao ya kijamii kama vile Twitter na Whatsapp zikionyesha namna wakaazi wa mtaa huo wanavyoonekana wakiwa na vumbi. Ukiwa Dar waweza jua daladala ni ya njia ipi kwa kuangalia tu abiria wanaoshuka au kupanda. Ukiona daladala abiria wengi wamevaa madela na baraghashia nyingi na wanaongea sana hiyo daladala ni ya kuelekea Temeke.Ukiona daladala wengi wanaopanda ni weupe weupe na wana meno ya rangirangi kama gold ni daladala ya kwenda Kimara & maeneo Mbezi mwisho .... Ila ukiona daladala .. wanaoshuka wamechafuka VUMBI kila sehemu usipate taabu... hizo ni daladala za MAKONGO JUU"... ni miongoni mwa ujumbe ambao umekuwa ukisambazwa katika mtandao wa Whatsapp Tanzania Wakaazi wa eneo hilo wanadai kushangazwa kwa kufanywa wao ndio mada

Kufungwa kwa maeneo ya burudani wakati wa sensa kwazua mjadala Kenya

Picha
Raia nchini Kenya wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kuelezea kutoridhishwa kwao na hatua ya kufunga maeneo ya burudani ili kufanikisha mpango wa kitaifa wa kuhesabu watu. Waziri wa usalama wa ndani Fred Matiang amezua gumzo nchini humo baada ya kutangaza mabaa na kumbi za burudani kufungwa kwa ajili ya shughuli ya kuhesabu watu maarufu sensa. Kwa mujibu wa Bw. Matiang'i maeneo ya burudani yatafungwa kuanzia saa kumi na moja jioni Jumamosi na Jumapili ili kuhakikisha wahudumu wa maeneo hayo wote wako nyumbani kufikia saa kumi na mbili jioni wakati ambapo maafisa wa kuhesabu watu wataanza kazi yao. "Tutafunga maeneo yote ya burudani hususana baa kuanzia saa kumi na moja jioni ili kukupatia muda wa kuwa nyumbani kabla ya maafisa wa kuhesabu watu kufika nyumbani kwako kuanzia saa kumi na mbili jioni," alisema waziri huyo siku ya Jumatano akitoa agizo hilo. Waziri huyo amewahakikishia Wakenya kuwa hali ya usalama utaimarishwa na maafisa wote wa usalama wamezuiliwa kwenda

Ubaguzi dhidi ya Pogba: Wito watolewa wachezaji kususia mitandao ya kijamii

Picha
Mkufunzi wa timu ya soka upande wa akina dada nchini England Phil Neville amesema kuwa wachezaji wanapaswa kususia mitandao ya kijamii ili kutuma ujumbe mzito kwamba ubaguzi wa rangi hautakubaliwa. Matamshi ya Neville yanajiri baada ya kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba kupokea machapisho ya ubaguzi wa rangi mitandaoni kufuatai hatua yake ya kukosa penalti wakati wa mechi iliotoka sare ya 1-1 dhidi ya Wolves siku ya Jumatatu. ''Lazima tuchukue hatua mwafaka sasa kama jamii ya kandanda. Tumeona na wachezaji wangu katika mitandao ya kijamii, ligi ya Premia na mabingwa wameona'' , alisema Neville. ''Sijui kama jamii ya soka tunafaa kususia mitandao ya kijamii , kwa sababu Twitter haitachukua hatua yoyote, instagram haitafanya lolote - wanakutumia barua pepe wakisema kwamba watachunguza lakini hakuna kinachofanyika''. Nimepoteza imani na yeyote anayeendesha idara za mitandao hii, hivyobasi tutume ujumbe mzito. Tususie mitandao ya kijamii kwa miez

Vita vya wenyewe kwa wenyewe Syria: 'Watu watatu' wauawa katika shambulio la msafara wa magari ya kijeshi ya Uturuki

Picha
Shambulio la angani la serikali ya Syria uliolenga msafara wa kijeshi wa Uturuki uliokuwa ukielekea katika eneo linalotawaliwa na waasi kaskazini mwa Syria limesababisha vifo vya raia watatu, Uturuki imedai. Watu wengine 12 walijeruhiwa katika shambulio hilo katika mkoa wa Idlib siku ya Jumatatu kulingana na wizara ya ulinzi ya Uturuki. Idlib ambayo ni mojawapo ya maeneo machache yasiodhibitiwa na serikali, ilitarajiwa kulindwa na kuwa eneo huru linalotenganisha majeshi pinzani lililoafikiwa na Uturuki inayowaunga mkono waasi mwaka uliopita. Lakini mashambulizi ya serikali yamekuwa yakiongezeka tangu mwezi Aprili. Mamia ya raia wameuawa kutokana na hilo na kuna hofu kwamba wengi watafariki iwapo hali itaendelea kuwa mbaya. ''Hii ndio hatari inayotukabili kwa sasa'', alisema Jan Egeland kutoka baraza la wakimbizi la Norway akizungumza na BBC. Kwa miaka kadhaa sasa tumeonya kuhusu hatari inayoikabilia Idlib , ambapo hakuna mahala pa kutorokea kwa raia milioni 3. Kuna wapi

Wanasayansi wa Uingereza wamegundua mti mrefu zaidi duniani

Picha
Wanasayansi nchini Uingereza na Malaysia wanasema kuwa wamegundua mti mrefu zaidi duniani wenye urefu wa zaidi ya mita 100. Mti huo wa kitropiki aina ya meranti ulipatikana katika msitu wa Borneo na kundi moja kutoka chuo kikuu cha Nottingham mwaka uliopita. Watafiti kutoka katika chuo kikuu cha Oxford walifanya utafiti huo kwa kutumia kamera zisizokuwa na rubani kuthibitisha rekodi hio. Mti huo uliopatikana katika eneo la uhifadhi la Danum Valley huko Sabah umepewa jina Menara ambalo linamaanisha jumba refu. Mkweaji miti kutoka eneo hilo, jami ambaye aliupima mti huo kwa kutumia kamba alisema alliogopa kuupanda mti huo ''Lakini kwa kweli picha kutoka juu ilikuwa nzuri mno. Sijui cha kusema isipokuwa tu ulikuwa uzoefu mzuri sana'', liongezea. Daktari Doreen Boyd, kutoka chuo kikuu cha Nottingham, alisema kuwa ugunduzi huo ulikuwa muhimu kwa kuwa ni sayansi inayosema miti kama hii inapatikana , ni mirefu hali ya kwamba hatukuwahi kudhania na huenda kuna miti mirefu zaidi

Watalii wa Ufaransa kukabiliana na hukumu ya wizi wa mchanga

Picha
Wapenzi kutoka Ufaransa wamekamatwa na kilo 40 za mchanga wa Sardinian katika gari lao na wanaweza kukabiliana na kifungo cha miaka 6 jela. Walisema kuwa walitaka kuondoka na mchanga nyumbani kwao na hawakujua kama wamefanya makosa. Ni kosa la jinai kwa mtu kuhamisha mchanga kutoka katika kisiwa cha Sardinia, kwa sababu mchanga unatambulika kama mali ya umma. Kwa miaka mingi, wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakilalamikia wizi wa mali asili ikiwa ni pamoja na mchanga. Wapenzi hao wanaweza kuhukumiwa kati ya mwaka mmoja jela mpaka miaka sita kwa kosa la wizi wa mali ya umma. Chini ya sheria ya mwaka 2017, biashara ya mchanga na mapambo ya bahari ni kunyume cha sheria, na faini ya yuro 3000. Polisi walikuta mchanga umewekwa kwenye chupa 14 ambazo zilitoka katika ufukwe wa Chia , kusini mwa Sardinia katika buti ya gari la wapenzi hao. Mwaka 1994, ufukwe uliopo kisiwa cha Budeli kaskazini mashariki mwa Sardinia uliwekewa zuio kwa ajili ya siku siku za mbeleni. Mamlaka ina hofu ya tani kadhaa z

Tetesi za soka jumatatu Barani Ulaya:

Picha
Paris St-Germain wamemtaka beki wa Real Madrid na Ufaransa Raphael Varane, 26, pamoja na mshambuliaji wa Brazil Vinicius Junior, 19, katika mpango wa kubadilishana wachezaji iwapo wanamuitaji mshambuliaji wa Brazil mwenye umri wa miaka 27 Neymar. 

Watu 73 washikiliwa na polisi mkoani Shinyanga kwa Uhalifu:

Picha
Jeshi la polisi mkoani Shinyanga limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne wa matukio ya mauaji ya watu wawili wa familia moja na wengine zaidi ya 70 waliokamatwa wakijihusisha na uhalifu mbalimbali ikiwemo kusafirisha dawa za kulevya,utekaji,wizi na utengenezaji wa pombe haramu ya moshi. Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga ACP Richard Abwao amewataja watuhumiwa wanne kati ya 73 wanaoshikiliwa kwa tukio la kufanya mauaji ya mwanamke mmoja kwa kumfungia mawe shingoni na miguuni na kumtumbukiza kwenye lambo la maji kwa lengo la kupoteza ushahidi huku wakiwa wamemteka mtoto wake na kusafiri naye hadi wilayani Mpanda mkoani Katavi kumuua na kutelekeza mwili wake porini ambapo uliliwa na fisi na kubakizwa mabaki tukio ambalo linadaiwa chanzo chake ni kuwania mali.   Aidha kamanda Richard Abwao amesema katika kipindi cha mwezi mmoja jeshi la polisi mkoani Shinyanga limefanikiwa kukamata watuhumiwa waliokuwa wamepora pikipiki na kuwaua madereva wake huku wakikamata vifaa vya kuvunjia m

Nusu ya dhahabu inayonunuliwa kwa wachimbaji wadogo Chunya inatoroshwa:

Picha
Zaidi ya nusu ya dhahabu inayonunuliwa na wanunuzi wa kati maarufu kama Brokers kutoka kwa wachimbaji wadogo wadogo wilayani Chunya  inatoroshwa badala ya kupelekwa kuuzwa kwenye soko kuu la dhahabu lililofunguliwa na serikali wilayani humo. Licha ya serikali kufungua soko la madini wilayani Chunya kwa ajili ya kuwawezesha wachimbaji na wanunuzi wa dhahabu kufanya biashara hiyo kwa njia halali na serikali kupata mapato yake, imebainika kuwa madini ya dhahabu hasa yanayonunuliwa kutoka kwa wachimbaji wadogo hayafikishwi sokoni hapo na badala yake yanatoroshwa  na kwenda kuuzwa nje ya wilaya na hata kusafirishwa nje ya nchi kinyemela. Mkuu wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa wilaya ya Chunya, Luitufyo Mwambungu amesema utoroshaji huo wa dhahabu una harufu ya kuambatana na vitendo vya rushwa na kuwataka wananchi kutoa taarifa za vitendo hivyo, huku Meneja wa mamlaka ya mapato Tanzania, TRA, wilaya ya Chunya, Osaund Mbilinyi akidai kuwa ipo changamoto ya wanunuzi na wachimbaji wa m

Ajali yasababisha vifo vya watu watano Morogoro:

Picha
Watu watano wamefariki na wengine 26 wamejeruhiwa baada ya basi la abiria la Safari njema kugongana uso kwa uso na lori aina ya tata mali ya kiwanda cha Tumbaku cha Alliance One katika eneo la Nanenane manispaa ya Morogoro. Ajali hiyo imetokea majira ya saa saba usiku ambapo majeruhi 26 akiwemo mtoto mdogo wameshakimbizwa katika hospitali ya rufaa ya Manispaa ya Morogoro na wanaendelea na matibabu.

Mbwana Samatta afunga hat-trick Ubelgiji na kuisadia KRC Genk kupata ushindi mkubwa

Picha
Mshambuliaji na nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta anayeichezea klabu ya KRC Genk nchini Ubelgiji siku ya Jumamosi aligonga vichwa vya habari baada ya kuisaidia timu yake kufunga hat-trick katika mechi ya ligi ya Ubelgiji dhidi ya klabu ya Waasland-Beveren. Samatta alifiunga magoli hayo katika mechi ilioipatia timu yake ushindi mkubwa ugenini. Mshambuliaji huyo alifunga goli lake la kwanza katika dakika ya 52 baada ya mchezaji mwenza Paintisil kuiweka kifua mbele KRC Genk kunako dakika ya 21. Baadaye mshambuliaji huyo alifongeza goli la pili na la tatu kwa jumla katika dakika ya 66. katika ukurasa wake wa instagram Samatta aliandika: Ni Furaha kupanta pinti tatu muhimu leo nje ya nyumbani. Timu ilkicheza vizuri. Na tunawashukuru mashabiki waliosafiri kutupa sapoti.Pia nina furaha kufunga hat-trick yangu ya kwanza msimu huu na nina imani nyingi zitakuja. Ruka ujumbe wa Instagram wa samagoal77 Mwisho wa ujumbe wa Instagram wa samagoal77 Lakini hakusita hapo kwani muda wa

Tetesi za soka jumapili barani Ulaya:

Picha
Mshambuliaji wa Manchester United na Chile Alexis Sanchez, 30, amekataa uhamisho wa kuelekea Roma, licha ya klabu hiyo ya Old Traford kukubali kulipa kitita kikubwa cha mshahara wake wa £560k kwa wiki. Hata hivyo Sanchez huenda akaelekea katika ligi ya serie A baada ya Man United kumruhusu kufanya mazungumzo na Inter Milan, ambapo huenda akakubali kupunguza mshahara wake.

Tetesi za soka barani Ulaya:

Picha
Monaco wanamtaka mshambuliaji wa Uingereza Daniel Sturridge, 29, ambaye yuko huru baada ya kuondoka Liverpool. 

Rais wa Tanzania John Magufuli ndiye mwenyekiti mpya wa SADC

Picha
Rais wa Tanzania, John Magufuli ndiye mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, SADC. Bw. Magufuli ambaye amekabidhiwa uwenyekiti huo na Rais wa Namibia, Dk Hage Geingob ataongoza Jumuiya hiyo kwa mwaka mmoja. Akipokea uwenyekiti huo Rais Magufuli amesema:''Tunaahidi kushirikiana na nchi zote Wanachama wa SADC kuhakikisha kupitia mkutao huu ndoto na mawazo ya Baba wetu wa Taifa pamoja na viongozi wengine waanzilishi wa Jumuiya hii yanaendelea kutekelezwa kwa vitendo'' Tayari mwenyekiti huo mpya ameomba rasmi Jamii ya Kimataifa kuiondolea Zimbabwe vikwazo vya kiuchumu akiongezea kuwa vikwazo hivyo vimelemaza uchumi wa taifa hilo Kwa mujibu wa Bw. Magufuli vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Zimbabwe vinaathiri pia ushirikiano wake katika Jumuiya ya Sadc na kuomba nchi hiyo ipewe nafasi ya pili kwa sababu ina utawala mpya. Rais wa nchi hiyo Emerson Mnangagwa pia yuko nchini Tanzania kuhudhuria mkutano huo wa siku mbili. Zimbabwe iliwekewa vikwazo hivyo na matai

Gareth Bale: Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane 'kumtegemea' mshambuliaji wa Wales

Picha
Mkufunzi wa klabu ya ya Real Madrid Zinedine Zidane amesema sasa "anamtegemea" mshambuliaji Gareth Bale licha ya kauli alizozitoa awali kwamba nyota huyo wa kimataifa wa Wales huenda akahama klabu hiyo. Bale alitarajiwa kujiunga na klabu ya Jiangsu Suning inayoshiriki Super League ya Uchina mwezi Julai. Zidane wakati huo alisema kuondoka kwake kutakuwa vyema kwa kila mtu. Mchezaji Eden Hazard aliyesajiliwa hivi karibuni aliumia paja siku ya Ijumaa akiwa mazoezini sasa Bale huenda akategemewa katika mechi ya ufunguzi wa La Liga dhidi ya Celta Vigo Jumamosi ya leo. "Ilionekana kama ataondoka lakini kwa kuwa hakufanya hivyo nitamtegemea sawa na wachezaji wengine katika kikosi," alisema Zidane. "Ana mkataba, na ni mchezaji muhimu, na kila mchezaji ananipatia wakati mgumu kuamua nani ajumuishwe katika kikosi cha kwanza au la." Hazard, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa kati ya wiki tatu mpaka nne, huku Real ikiendelea kumudu bila uwepo wa muda mrefu wa Marco As

Meno ya bandia yakwama kooni kwa wiki moja

Picha
Mgonjwa mmoja nchini Uingereza amejikuta katika maumivu makali baada ya meno yake ya bandia kunasa kooni kwa wiki moja. Mgonjwa huyo mwenye miaka 72 alikuwa akilalamika kupata maumivu makali wakati wa kumeza vitu na kukohoa damu katika kipindi chote hicho. Bwana huyo, alimeza meno hayo wakati akifanyiwa upasuaji wa tumbo. Undani wa tukio hilo umechapishwa kwenye jarida la kisayansi la BMJ ambapo watunzi wake wamewataka madaktari kuhakikisha wagonjwa wao wanaondoa meno ya bandia kabla ya upasuaji. Siku sita tu baada ya upasuaji huo uliofanyika mwaka 2018, bwana huyo alienda kwa daktari na kulalamika kuwa nanashindwa kumeza vyakula vizito. Madaktari awali waliamini kuwa hiyo ni athari ya kuwekewa mpira kwenye kinywa wakati wa upasuaji, na kumpatia dawa za kukabiliana na maumivu na maambukizi ya koo. Lakini baada ya bwana huyo kurudi tena baada ya siku mbili akiwa na malalamiko zaidi, madaktari ikabidi wamfanyie uchunguzi zaidi wa koo. Vipimo vya miale ya X-Ray vikaonesha kuwa kuna meno y

Wabunge wa Marekani wapigwa marufuku Israel

Picha
Israel imeamua kuwawekea vikwazo vya usafiri wabunge wawili wa chama cha Democratic nchini Marekani baada ya Rais Trump kuiomba nchi hiyo kuwapiga marufuku Bwana Trump alisema "itaonesha udhaifu mkubwa" ikiwa Israel itawaruhusu Ilhan Omar na Rashida Tlaib kuzuru taifa hilo. Hatua hiyo inakuja baada ya tamko la balozi wa Israel nchini Marekani mwezi uliopita kuwa wawili hao wataruhusiwa kuingia nchi hiyo. Israel imekua ikiwapiga marufuku wafuasi wa vugu vugu linalosusia taifa hilo, kitu ambacho viongozi hao wawili wanaunga mkono. Hatua huyo imethibitishwa katika taarifa iliyotolewa na wazara ya mambo ya ndani ya Israeli, ambayo imesema "haielewi kwa nini watu wanaopinga taifa la Israel waruhusiwe kulizuru". Mwezi uliopita balozi wa Israeli nchini Marekani, Ron Dermer alisema wabunge hao wawili wa Democratic wataruhusiwa kuingia nchini humo "kwa heshima ya bunge la Marekani na uhusiano uliopo kati ya nchi hiyo na Israel". Rais Trump, ambaye ana uhusiano wa k

Ndege ya Urusi yalazimika kutua kwa dharura baada ya kugongana kundi la ndege

Picha
Ndege ya abiria ya Urusi imelazimika kutua kwa dharura kwenye shamba la mahindi karibu na jiji la Moscow baada ya kugonga kundi la ndege. Watu ishirini na watatu wamejeruhiwa katika tukio hilo, ambalo limesababisha ndege kutua huku injini yake ikiwa imezima na gia yake kutua ikirudi nyuma, wamesema maafisa wa afya. Ndege hiyo Ural Airlines Airbus 321 ilikuwa ikisafiri kuelekea katika eneo la Simferopol Crimea ilipogonga kundi la ndege muda mfupi baada ya kuondoka uwanjani , hali iliyovuruga utendaji wa injini yake. Vyombo vya habari vya taifa la Urusi vimetaja kutua kwa ndege hiyo kama "muujiza wa eneo la Ramensk". Maafisa wa ndege hiyo wamesema ndege imeharibika sana na haiwezi kupaa tena. Uchunguzi rasmi juu ya ajali hiyo unaendelea. Ndege hiyo ilikwa na abiria 233 na wahudumu ndani yake wakati ndege waliporipotiwa kuingia ndani ya injini na rubani wake akaamua kutua mara moja. Abiria mmoja ambaye hakutajwa jina lake ameiambia televisheni ya taifa kuwa ndege ilianza kuyumba

Facebook kuhakiki maudhui yanayochapishwa kwa lugha za kiafrika kupambana na taarifa za urongo

Picha
Mtandao wa kijamii wa Facebook, kwa ushirikiano na shirika la kuhakiki taarifa la Africa Check, umeanza mpango wa kufuatilia taarifa bandia zinazochapishwa katika mtandao huo kwa kutumia lugha za kiasili za kiafrika. Mpango huo uliozinduliwa mwaka jana katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara barani Afrika, sasa utajumuisha uhakiki wa lugha za Yoruba, Igbo, Swahili, Wolof, Afrikaans, Zulu, Setswana na Sotho. Taarifa zitakazosadikiwa kuwa ghushi zitadhibitiwa hali ambayo itahakikisha haziwafikii watumiaji wengu wa mtandao huo ili zisisambazwe kwa urahisi. Facebook inasema kuwa inategemea mrejesho kutoka kwa watumiaji wake kudhibiti taarifa bandia inapochambua uhalisia wa taarifa husika. Mtandao huo wa kijamii wa umekuwa ukilamiwa vikali wa kusambaza taarika ghushi na kauli za uchochezi na chuki. Facebook imekuwa ikilaumiwa kutodhibiti mitandao yao, sasa wajipanga kuchukua hatua Barani Afrika pekee zaidi ya watu milioni 130 wanatumia mtandao wa Facebook. Hivi karibuni Facebook iliunda

Je ni kweli taasisi ya haki miliki ya muziki Kenya haiwalipi wasanii?

Picha
Taasisi ya haki miliki ya muziki nchini Kenya inakabiliwa na shutuma kali kutoka kwa wasanii wa muziki wanaodai limekuwa haliwalipi pesa zao kulingana na kazi yao. Taasisi hiyo -Music Copyright Society of Kenya ina jukumu la kuwalipa wasanii wa muziki kwa kazi yao, lakini kwa miaka wasanii wa Kenya wamekuwa wakilalamika kuwa haliwalipi ili hali miziki yao inachezwa kwenye redio na televisheni. Tulipe Pesa zetu, Tafadhali. Yamekuwa ni maneno yanayorudia mara kwa mara kila mara wanamuziki wanapokutana kwa mikutano yao na katika maandamano ya mitaani yanayolenga kupinga kutolipwa na taasisi hiyo. Hata hivyo bado hawajawahi kusikilizwa.