Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2019

Unyonge wa Liverpool kwa miaka 30 EPL umefikia kikomo

Picha
Japo wenyewe hawasemi, ama yawezekana hawataki kunukuliwa wakisema, miaka 30 ya kushindwa kuchukua taji la Ligi ya Primia kwa Liverpool hatimaye inaelekea kufika kikomo. Hawawezi kusema hadharani, ama kuonesha furaha yao kwa sasa, kwa kuwa katika miaka hiyo 30 kumekuwa na vipindi ambavyo walikaribia kunyakua kombe lakini likawaponyoka. Lakini yaonekana mwaka huu hadithi ni tofauti, ubora wa kikosi ni wa hali ya juu, yawezekana ikawa sahihi kusema kikosi hiki cha sasa ndiyo bora zaidi kuliko vyote katika miongo mitatu iliyopita. Nuru ya ushindi iling'ara zaidi kwa vijana hao wanaonolewa na Mjerumani Jurgen Klopp baada ya kuichapa Leicester City inayoshika nafasi ya pili kwa goli 4-0 siku ya Boxing Day. Ushindi wa Liverpool uliambatana na kiwango safi cha umiliki wa kandanda, Leicester ambayo watu walikuwa wakiipigia chapuo la kuizuia Liverpool na kufanya maajabu ya kuchukua ubingwa kama mwaka 2016 walikuwa zaidi ya wanyonge katika mchezo huo uliopigwa dimbani kwao. Klopp:

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 27.12.2019: Xhaka, Rabiot, Draxler, Gueye, Volland, Sane, Hazard

Picha
Chelsea inamtaka winga a PSG na Julian Draxler, 26, na kiungo wa kati wa Senegal mwenye umri wa miaka 30 Idrissa Gueye. (Star) Ajenti wa kiungo wa kati wa Arsenal Xhaka nasema kwamba mchezaji huuyo mwenye umri wa miaka 27 raia wa Uswizi amekubali uhamisho wa kuelekea katika klabu ya Ujerumani ya Hertha Berlin. (Blick, via Mirror) Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta anataka kumsaini kiungo wa kati wa Adrien Rabiot, 24, kwa mkopo kutoka klabu ya ligi ya Seria A Juventus imwezi Januari. (Times - subscription required) Mkufunzi wa Chelsea Frank Lampard anasema kwamba winga wa Brazil Willian 31 ameanza mazungumzo na klabu hiyo kuhusu kuongeza kandarasi yake ambayo inakamilika mwisho wa msimu huu.. (Mail) Bayer Leverkusen itazuia jaribio lolote la Arsenal la kujaribu kumsaini winga wa Ujerumani Kevin Volland, 27, kutoka kwao. (Mail) Winga wa Manchester City Leroy Sane, 23, atasalia katika klabu hiyo hadi mwisho wa msimu huu lakini raia huyo wa Ujerumani anatarajiwa kuhamia Bayern Mun

Mzee aiba pesa na kuzitoa kama zawadi akisema 'Merry Christmas'

Picha
Bwana mmoja mwenye ndevu nyeupe alifanya u vamizi wa benki siku mbili kabla ya Krismasi na kuzirusha juu kwa furaha na kuwatakia kheri ya siku kuu wapita njia, mashuhuda wameeleza. Polisi wamethibitisha "mwanaume mzee wa kizungu" alivamia benki ya Academy mjini Colorado Springs, Marekani siku ya Jumatatu. "Aliiba pesa benki, akatoka nje na kuzitawanya kwa watu,"  shuhuda Dion Pascale alikiambia kituo cha Colorado's 11 News . "Alianza kurusha fedha kutoka kwenye begi na kisha akaanza kusema, 'Merry Christmas!'" Kwa mujibu wa mashuhuda, mtuhumiwa huyo akapiga hatua chache kutoka benki na kuketi mbele ya mkahawa wa Starbucks akisubiri kukamatwa. Katika hali ambayo inaweza kuwa ya kustaajabisha kwa wakazi wa Afrika Mashariki, wapita njia wanaripotiwa kuwa walichota fedha zote zilizozagaa na kuzirudisha benki. Polisi wamemtaja  mtuhumiwa huyo kwa jina la David Wayne Oliver, mwenye miaka 65 . Polisi hawadhani kuwa alikuwa na usaidi

Je, Chama cha upinzani kushinda uchaguzi ni ishara ya demokrasia?

Picha
 mwandishi wetu,Mbelechi Msoshi Historia nyingine iliandikwa kwa taifa la Jamuhuri ya kidemokrasia ya kongo tarehe 29 Januari 2019. Kwa mara ya kwanza rais mpya kutoka chama cha upinzani ,Felix Tshisekedi aliapishwa mbele ya maelfu ya raia wa Kongo na rais mstaafu Joseph kabila. Katika tukio hilo rais mstaafu Joseph Kabila alimkabidhi Felix Tshikedi bendera ya taifa na nakala ya katiba. Maelfu ya wafuasi wa Tshisekedi, walisherehekea tukio hilo la kihistoria nje ya Ikulu ya Taifa, makaazi ya Rais, mjini Kinshasa. Baada ya miezi saba, serikali ya muungano ilioundwa, baina ya chama cha kabila na chama cha rais mpya Tshisekedi, vyama viwili ambavyo vilipingana kwa kipindi cha muda mrefu vilikubaliana kufanya kazi kwa pamoja, lakini baada ya siku chache tu mvutano ulianza kati ya vyama hivyo. Baadhi ya wafuasi wa chama cha Tshisekedi walianza kususia ushirikino huu, huku wakiwashutumu wafuasi wa chama cha kabila kumzuia rais mpya kutekeleza ahadi zake. "Kitu ninachotaka

Askari wa Umoja wa Mataifa kuendelea kulinda amani DRC

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa  leo hii limeidhinisha nyongeza ya mwaka mmoja wa kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Umoja wa Mataifa umepunguza idadi ya jeshi na kuongeza maafisa wa polisi. Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeidhinisha nyongeza ya mwaka mmoja wa kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wakati huo huo Umoja wa Mataifa umepunguza idadi ya jeshi na badala yake kuongeza maafisa wa polisi. Saumu Njama na taarifa zaidi Azimio lililowekwa katika rasimu ya Ufaransa, ambalo pia linaweka mkakati wa kuondoka nchini humo , lilikubaliwa kwa hiari na baraza la wanachama 15. Balozi wa Afrika Kusini Xolisa Mabhongo, akizungumza kwa niaba ya washirika watatu wa baraza la Afrika, alipongeza mpango huu na kwa kusema ni muhimu kujiondoa kwa MONUSCO kwa msingi wa mabadiliko baada ya kufikiwa mafanikio katika mkutano wao. Kwa upande wake, mwakilishi wa Kongo, Paul Empole Losoko Elambe, amesema, "wazo la kulenga vikosi vya MONU

Matamshi ya Mesut Ozil: Kiungo wa Arsenal afutwa kwenye mchezo wa video China

Picha
Kiungo wa Arsenal Mesut Ozil ameondoshwa kwenye mchezo wa video wa Pro Evolution Soccer (PES) 2020 toleo la Uchina baada ya kuikosoa nchi hiyo kwa kuwatesa jamii ya Waislamu ya Uighur. Ozil, 31, ambaye ni Muislamu, amewaita Wauighur (Wachina wa asili ya Kiislamu) "mashujaa wanaokabiliana na mateso". Pia ameukosoa utawala wa Uchina na ukimya wa Waislamu katika kuwatetea wenzao nchini humo. Kampuni ya NetEase, ambayo inatoa video za PES nchini China, imesema kiungo huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Ujerumani ameondolewa kwenye matoleo matatu yaliyopo nchini humo. "Ozil ametoa matamshi makali kuhusu Uchina kwenye mitandao ya kijamii," imesema kampuni hiyo kwenye taarifa yake. "Matamshi yake yameumiza hisia za mashabiki wa Kichina na kuvunja kanuni ya michezo ya amani na upendo. Hatuelewi, kukubali ama kusamehe jambo hili. Arsenal imesema kuwa klabu hiyo "si ya kisiasa" na wizara ya mambo ya nje ya Uchina imedai kuwa mchezaji huyo mwenye asi

Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 18.12.2019: Pogba, Haaland, Ancelotti, Ronaldo, Kante

Picha
Manchester United hawatamruhusu kiungo wao Mfaransa Paul Pogba, 26, kuihama klabu hiyo katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari. (Mail) United inaamini kuwa itamsajili mshambuliaji nyota wa Red Bull Salzburg na timu ya taifa ya Norway Erling Braut Haaland kwa kitita cha pauni milioni 76 mwezi Januari - na endapo wataruhusu mchezaji huyo asalie kwa mkopo Salzburg mpaka mwisho wa msimu. (Sun) Hata hivyo klabu ya Red Bull Leipzig pia wamempatia ofa mpya kwa minajili ya kumshawishi mshambuliaji huyo mwenye 19 kusalia klabuni hapo. (Kicker, via Mail) Carlo Ancelotti atambakiza kocha wa muda wa Everton Duncan Ferguson kama sehemu ya benchi la ufundi kama atateuliwa kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo. (Telegraph) Ajenti wa Cristiano Ronaldo, bwana Jorge Mendes amedokeza kuwa nyota huyo mwenye miaka 34 huenda akamaliza maisha yake ya kandanda katika klabu ya Juventus. (Sky Sports, via Goal) Manchester City wamewapiku Manchester United katika mbio za kutaka kumsajili beki kinda wa Bar

Boeing yatangaza kuacha kuzalisha kwa muda ndege za 737 Max kuanzia Januari

Picha
Kampuni ya Boeing itasimamisha kwa muda uzalishaji wa ndege zake zilizokumbwa na matatizo za 737 Max mwezi Januari. Utengenezaji wa ndege hizo ulikuwa ukiendelea licha ya ndege za chapa hiyo kuzuiwa kupaa kwa mezi tisa baada ya kuhusika katika ajali mbili zilizosababisha vifo vya mamia ya watu. Zaidi ya watu 300 walipoteza maisha wakati ndege mbili za 737 Max zilipoanguka katika nchi za Indonesia na Ethiopia baada ya kuripoti matatizo katika mfumo wake mpya. Boeing imekua ikitumaini kuwa ndege hizo zitarejea tena angani kufikia mwishoni mwa mwaka huu. Hata hivyo wasimamizi wa safari za anga nchini Marekani wamesema wazi kuwa ndege hizo hazitapewa kibali cha kurejea angani katika siku za hivi karibuni. Kampuni ya Boeing, yenye makao yake Seattle, Washington ni moja ya wauzaji wakubwa zaidi wa ndege duniani. Kampuni hiyo imesema katika taarifa yake kwamba haitawafuta kazi wafanyakazi wanaofanya kazi na 737 Max, lakini kusimamishwa kwa utengenezaji zake kunaweza kuwaathiri wa

Tetesi za soka Ulaya Jumatatu tarehe 16.12.2019: Ljungberg, Nuno, Pellegrini, White, Maja, Coutinho

Picha
Meneja wa muda Freddie Ljungberg amewataka wakuu wa Arsenal kuamua haraka mtu wanaemtaka kuwa wao meneja ajae. (Sun) Hatahivyo, Arsenal bado hawajawasiliana na Wolves kupata ruhusa ya kuzunguza na Nuno Espirito Santo juu ya kazi yao ya umeneja. (Express and Star) Akikabiliwa na shinikizo meneja Manuel Pellegrini anatarajiwa kuendelea kuiongoza  Ham kwa kemu yao ijayo  ya Crystal Palace itakayochezwa Alhamisi ya baada  Krismasi. (Guardian Chelsea wanaangalia uwezekano wa kumhamisha mshambuliaji wa Nigeria anayechezea klabu ya Ufaransa Bordeaux Josh Maja, mwenye umri wa miaka 20, zamani akiichezea Sunderland mwezi Januari. (90min.com) Chelsea pia wamemuweka mlizi wa Brighton Muingereza Ben White, mwenye umri wa miaka 22, ambaye amewafurahisha wengi akicheza kwa deni katika Leeds, katika orodha yao wachezaji watakaonunuliwa kwa pauni milioni 25 wakati dirisha la uhamisho wa wachezaji litakapofunguliwa Januari. (Sun) Wachezaji wa Bayern Munich wamewaomba wakuu wa klabu hiyo was

UN - COP 25: Mazungumzo ya hali ya hewa yagonga mwamba

Mataifa ya ulimwengu yamegawanyika katika matabaka ya matajiri na masikini kuhusiana na ufadhili wa mabadiliko ya hali ya hewa na sheria za ushirikiano wa kimataifa. Marekani, India, China na Brazil zimelaumiwa kwa kukosa muelekeo katika mapambano dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa.  Mkutano wa mazingira wa COP 25 wa Umoja wa Mtaifa uliofanyika mjini Madrid, Uhispania na uliotarajiwa kumalizika jana Ijumaa, umeongezewa muda hadi leo Jumamosi ili kujadili zaidi masuala ya mabadiliko ya hali ya hewa. Wawakilishi kutoka mataifa 200 wanakutana mjini Madrid kumalizia muongozo wa kuhusu hali ya hewa kwa mujibu wa mkataba wa Paris ea mwaka 2015, ambao unapendekeza upunguzaji wa joto la dunia hadikufikia kiwango cha chini ya digrii 2 Celsius. Umoja wa Mataifa umesema ili kulipunguza joto kwa nyuzi 1.5 ulimwengu unahitaji kupunguza uzalishaji wa gesi chafu kwa zaidi ya asilimia 7% kila mwaka hadi kufikia 2030. Wanasayansi wameonya kwamba dunia inakabiliwa na kasi isiyoweza kuzuilika ya

Matokeo ya uchaguzi 2019: Conservative chanyakua viti vya Leba katika ushindi wa kihistoria

Picha
Kiongozi wa chama cha Conservative Boris Johnson amewashukuru wapiga kura wa Uingereza kwa kushiriki kwa wingi katika uchaguzi wa Disemba. Akizungumza na vyombo vya habari muda mfupi baada ya chama chake kushinda zaidi ya viti 326, Boris Jonhson amesema kwamba hatua hiyo inaipatia serikali mpya fursa ya kuheshimu maamuzi ya kidemokrasia ya raia wa Uingereza ili kuliimarisha taifa hilo. Chama cha Boris Johsnon kilihitaji kujipatia viti 326 ili kutangazwa kuwa mshindi lakini kufikia sasa kimepitisha idadi hiyo na kufikia viti 363. Waziri huyo mkuu amesema kwamba uamuzi huo unampatia jukumu la kufanikisha Brexit na kuiondoa Uingereza katika muungano wa Ulaya. ''Zaidi ya yote nataka kuwashukuru watu wa taifa hili kwa kujitokeza kupiga kura ya Disemba ambayo imebadilika na kuwa ya kihistoria, ambayo inatupatia sisi kama serikali mpya fursa ya kuheshimu uamuzi wa kidemokarsia wa raia wa kulibadilisha taifa hili na kuonyesha uwezo wa raia wa taifa hili''. Johnson am

Je juhudi za upatikanaji wa pedi zinazaa matunda A. Mashariki?

Picha
Serikali ya Rwanda imetangaza kuondoa ushuru wa nyongeza ya thamani (VAT) kwa taulo za hedhi katika hatua ya kusaidia wanawake na wasichana kupata vifaa hivyo kwa urahisi. Mashirika ya kusaidia wanawake nchini humo yamekuwa yakipaaza sauti kutaka serikali kutoa taulo za hedhi hata kwa bure. Hatua ya kuondoa ushuru wa nyongeza ya thamani kwa taulo zinazotumiwa na wanawake wakiwa katika hedhi imetangazwa na wizara ya maendeleo ya wanawake na usawa wa jinsia kwenye ukurasa wake wa Twitter Wizara imesema kwamba ni uaamzi unaolenga kurahisishia akinamama kupata taulo hizo. Lakini je hii ni suluhu ya tatizo? Kwa kawaida maduka katika mji mkuu wa Rwanda Kigali na kwengineko nchini, bei ya paketi moja ya sodo(vitaambaa vya hedhi) huuzwa kati ya franga za Rwanda mia 900 na elfu moja, ambayo ni kama nusu ya dola 1, ukiondoa ushuru wa nyongeza ya thamani sokoni tofauti itakuwa ya franga chini ya 200. Kwa mwananchi wa kipato cha chini, bei ya franga 700 bado ni ya juu: ''Kwa ma

Jane Kiarie: ''Mama alijaribu kuniua lakini alitoka akilia''

Picha
Jane Kiarie alitelekezwa na mama yake mzazi punde tu baada ya kuzaliwa. Mama yake kijana ambaye kulingana na yeye hakuwa tayari kupata mtoto, akipata ujauzito wa Kiarie alikuwa na umri wa miaka 17 pekee yaani bado kijana na wakati huohuo, alikuwa akifanyakazi kama yaya. Alibeba ujauzito wa Kiarie hadi miezi minane lakini mambo yalimzidi na hapo akaamua kuavya mimba hiyo akiwa peke yakk e katika nyumba ya dadake alimokuwa anaishi. Baada ya kuona mtoto aliyemuavya ametoka akiwa mzima na analia, akaamua kukimbia na kumuacha mtoto alipoangukia. Dada yake aliporudi jioni baada ya pilk apilka za siku akakutana na mtoto nyumbani kwake akiwa peke yake, na alichoamua kufanya ni kumpeleka kwa bibi yake. Masaibu ya Kiarie hayakuishia hapo kwa sababu mama yake mzazi alirejea tena miaka minne baadaye wakati huo akiwa na miaka 21 na mtoto mwengine wa kike mgongoni. Safari hii mama alionekana kuwa na mpango madhubuti na watoto wake kwasababu mara kwa mara aliwatembelea na kuwaletea viatu,

Tetesi za soka Ulaya Jumanne 10.12.2019: McTominay, Solskjaer, Eriksen, Emery

Picha
Mkufunzi wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer ameambiwa kwamba kazi yake ipo salama na mmiliki wa klabu hiyo na kwamba hawatamuajiri aliyekuwa mkufunzi wa Tottenham Mauricio Pochettino.. (Mail) Manchester United wana mpango wa kumpatia kiungo wa kati wa Uskochi mwenye umri wa miaka 23 Scott McTominay mkataba mpya wa £60,000 kwa wiki . (Sun) Everton iliwasiliiana na mkufunzi wa zamani wa Arsenal Unai Emery kuhusu pengo la mkufunzi katika klabu hiyo ya Goodison Park. (Sky Sports) Rasi wa Barcelona Josep Maria Bartomeu anasema kwamba mlango upo wazi kila mara iwapo mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola atahitaji kurudi katika klabu hiyo.. (La Repubblica, via Goal) Arsenal inakabiliwa na upinzani kutoka kwa Inter Milan na Juventus kwa saini ya beki wa Manchester United Chris Smalling, 30, ambaye yuko kwa mkopo katika klabu ya Roma. (Mirror) Newcastle na Bournemouth zinamchunguza mshambuliaji wa Hull City mwenye umri wa miaka 22 Jarrod Bowen. (90min) Bologna wamewasiliana na

Korea Kaskazini imesema (08.12.2019) imefanya jaribio la roketi ya masafa marefu, ikieleza kwamba litakua matokeo muhimu katika eneo lake la kimkakati.

Picha
Shirika la Habari la Korea CNA limesema jaribio hilo limefanywa katika eneo la maalumu la kufanyia majaribio la Sohae. Na kuongeza kwamba matokeo ya jaribio husika yameripotiwa kamati kuu ya chama tawala cha taifa hilo. Hata hivyo ripoti haikuisema jaribio lenyewe lilikuwaje hasa. Lakini vyombo vya habari vimesemea  picha mpya ya satellite inaonesha Korea Kaskazini inaweza kuwa inajiandaa kuanzisha upya mtambo ambao unatumika kusukuma satellite katika eneo hilo. Ripoti za jaribio hilo zinatolewa katika kipindi ambacho Korea Kaskazini imeongeza shinikizo kwa Marekani kuonesha jitihada za wazi katika katika mazungumz yaliokwama ya nyuklia. Marufuku ya Umoja wa Mataifa kwa Korea Kaskazini Umoja wa Mataifa uliipiga Marufuku Korea Kaskazini kurusha satellite kwa sababu, inalichukulia jambo hilo kama jaribio la jaribio la makombora ya masafa marefu. Baada ya kufanya majaribio kadhaa yalioshindwa, Korea Kaskazini ilifanikiwa kuifikisha satellite yake katika mzunguko wa dunia mwaka 2016. Katik

Tetesi za soka Ulaya Jumamosi 07.12.2019: Pogba, Van de Beek, Dembele, Cavani, Zaha

Picha
Kiungo wa kati wa Man United Paul Pogba yuko tayari kuondoka katika klabu hiyo katika dirisha la uhamisho la mwezi Januari , huku klabu ya Real Madrid ikiwa na matumaini ya kuanzisha mazungumzo ya kupunguza bei ya Man United ya £126.4m ili kumuuza mchezaji huyo wa Ufaransa huku akiingia miezi 12 ya mwisho katika kandarasi yake. (L'Equipe via AS) Tottenham imeendeleza hamu yake ya kutaka kumnunua mchezaji wa Ajax Donny van de Beek , lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 na raia wa Uholanzi anataka kuhamia Real Madrid, ambao wanajiandaa kutoa dau la £46.2m (De Telegraaf via FourFourTwo) Manchester City na Chelsea wamekuwa na mazungumzo na wawakilishi wa mchezaji wa Barcelona Ousmanne Dembele mwenye umri wa miaka 22 (Eldesmarque via Sun) Mkufunzi wa Chelsea Frank Lampard anaweza kupata zaidi ya £150m kutumia baada ya marufuku ya uhamisho ya klabu hiyo kupunguzwa huku ikiwalenga winga wa Crystal Palace na Ivory Coast Wilfried Zaha, 27, pamoja na beki wa kushoto wa Leicester City

Wajir Kenya: Watu sita wauawa na wapiganaji wa al-Shabab

Picha
Takriban watu sita wamefariki katika kaunti ya Wajir kaskazini mashariki mwa Kenya siku ya Ijumaa baada ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa kundi al-Shabab kushambulia basi walilokuwa wakisafiri. Walioshuhudia waliambia Newsday Swahili  kwamba wapiganaji kadhaa waliokuwa wamejihami walishambulia basi hilo lililokuwa likielekea Mandera na kuwalenga watu wasiotoka katika eneo hilo baada ya kuwatenga kutoka kwa abiria wengine. Kisa hicho kinadaiwa kufanyika kati ya miji ya Wargadadud na Kutulo . Kulingana na gazeti la Daily Nation nchini Kenya kamanda wa polisi katika kaunti hiyo Stephen Ngetich amethibitisha tukio hilo lakini hakuweza kutoa idadi kamili ya walioathiriwa. Bwana Ngetich amesema kwamba kikosi cha maafisa maalum tayari kimetumwa katika eneo hilo. ''Naweza kuthibitisha kwamba kundi moja la watu waliojihami walishambulia basi ambalo lilikuwa linaelekea Mandera siku ya Ijumaa jioni ijapokuwa bado hatujapata habari kamili kuhusu idadi ya waliouawa'', alinukul

Mvua Afrika Mashariki: Vimbunga pacha kupiga Alhamisi, Ijumaa

Picha
Vimbunga viwili vinatarajiwa kutua katika pwani ya Afrika Mashariki usiku wa leo Alhamisi na kesho Ijuamaa, mamlaka za hali ya hewa zinaripoti. Eneo la Puntland nchini Somalia ndilo linalotarajiwa kuathirika zaidi na tufani hiyo. Kwa mujibu wa wataalamu wa hali ya hewa, mgandamizo wa hali ya hewa ambao ulikuwa ukitengeneza vimbunga hivyo pacha umesababisha mvua kubwa katika nchi tisa za ukanda wa Afrika Mashariki. Zaidi ya watu 130 wamepoteza maisha kutokana na mafuriko na maporomoko ya udongo nchini Kenya na Uganda. Sehemu kubwa ya Somalia ni kame kwa muda mrefu, lakini toka mwezi Septemba, mvua kubwa ya zaidi ya mara mbili ya wastani wa kawaida zimekuwa zikinyesha sehemu kadhaa za nchi hiyo. Mpaka kufikia mwezi Novemba, zaidi ya watu 270,00 walilazimika kuhama makazi yao nchini humo. Kwa ujumla mvua zisizo za kawaida zinanyesha katika baadhi ya maeneo ya Kusini mwa Ethiopia, Tanzania, Djibouti, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini. Hata hivyo, mvua hizo zinatarajiwa kupungua kasi mara ba