Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2019

Tetesi za soka Ulaya Jumamosi tarehe 30.11.2019: Rodgers, Arteta, Vieira, Sancho, Willian, Richarlison

Arsenal wako tayari kuona kama wataweza kumshawishi Brendan Rodgers wa Leicester miongoni mwa watu waliowaorodhesha kuchukua nafasi ya Unai Emery.(Mirror) Leicester itahitaji fidia ya pauni milioni 14 kama klabu yoyote ya ligi kuu itajaribu kumchukua Rodgers. (Telegraph) Washika bunduki hao waliwasiliana na kocha wa zamani wa Valencia Marecelino ili awe meneja wao mpya ( Sun) Mauricio Pochettino, Nuno Espirito Santo, Massimiliano Allegri na Carlo Ancelotti wote ni miongoni wa wanaotamaniwa kujaza nafasi hiyo katika uwanja wa Emirate. (Telegraph) Wamiliki wa Wolves wanajiandaa kupambana kumbakisha Nuno, ambaye mkataba wake utakwisha mwishoni mwa msimu ujao. (Mail) Arsenal tena itapendekeza mchezaji wa zamani Mikel Arteta kujaza nafasi iliyoachwa na Emery. (Independent) Uamuzi wa kumtimua Emary ulifikiwa katika mkutano uluifanyika nchini Marekani siku ya Jumatatu.(Mirror) Aliyekuwa kipenzi cha Arsenal Patrick Vieira amefuilia mbali mpango wa kuondoka Nice- ingawa amekuwa akihusishwa na t

Siri ya Wole Soyinka kupona saratani

Mwandishi maarufu duniani, ambaye ni mshindi wa tuzo za Nobel Profesa Wole Soyinka alikutwa na saratani mwaka 2014. Sasa hali ya afya yake ni nzuri yaani hana saratani tena. Na kitu kikubwa ambacho profesa huyo alikuwa akikizingatia ni kujitunza vizuri na hakuwa anafanya mazoezi ya kukimbia. Soma zaidi:'Niliugua saratani ya kongosho, nikabeba ujauzito' 'Wazo lililonijia akilini lilikuwa ni kifo'

Bunge la Ulaya laidhinisha Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya

Picha
Bunge la Ulaya limeidhinisha wajumbe wapya wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, inayoshughulikia masuala ya kila siku ya uongozi wa umoja huo. Kwa kura hiyo, Ursula von der Leyen ataanza majukumu yake Jumapili ijayo. Kabla ya bunge la Ulaya mjini Strasbourg kuwapigia kura makamishna 27 aliowapendekeza, Ursula von der Leyenalikuwa ametoa ahadi ya kufanya mageuzi ambayo amesema yatafika katika kila kona ya jamii na ya uchumi wa Ulaya. Kura ilipopigwa, wabunge 461 waliunga mkono makamishna waliopendekezwa, huku 157 wakipiga kuwakataa, na 89 walijizuia. Karibu nusu ya makimishna hao 27, Von der Leyen akiwemo, ni wanawake, na hilo amesema inadhihirisha hatua iliyopigwa katika kuendeleza usawa wa jinsia, ingawa bado yapo mengi ya kufanya. Umoja kwa maslahi ya Ulaya Bi Ursula von der Leyen ambaye kabla ya kuchaguliwa katika wadhifa huu mpya alikuwa waziri wa ulinzi wa Ujerumani, amesema halmashauri anayoiongoza itafanya kazi kwa kuzingatia maslahi ya Umoja wa Ulaya. ''Kwa pamoja, tut

Watu 24 wauawa katika mkasa wa ndege Congo

Picha
Karibu watu 24 wameuwa  baada ya ndege ndogo kuanguka katika kitongoji chenye wakaazi wengi cha mji wa Goma, mashariki mwa Demokrasia ya Congo. Ndege hiyo iliyowabeba kiasi abiria 17 imeanguka leo wakati ikiruka kutoka mji wa Goma ulio mashariki ya Jamhuri ya Kidemkrasi ya Congo na kuwauwa abiria wote waliokuwemo. Jean Paul Lumbulumbu, makamu rais wa bunge la Kivu Kaskazini, amemsema miili 24 imepatikana kwenye vifusi ikiwemo ya watu kadhaa waliopigwa na vifusi vilivyokuwa vikianguka. Mfanyakazi wa uokozi ambaye hakutaka kutajwa jina amesema miili 26 imeptikana katika eneo la mkasa huo. Ndege hiyo ilianguka kwenye eneo la makaazi karibu na uwanja wa ndege wa mjini katika jimbo la kivu kaskazini na kuna wasiwasi kuwa imewauwa watu wengine waliokuwepo ajali ilipotokea. Hakujawa na taarifa yoyote kuhusu chanzo cha ajali hiyo. Taarifa ya awali iliyotolewa na gavana wa jimbo la kivu kaskazini imesema ajali ilitokea baada ya ndege hiyo mali ya kampuni binafsu ya Busy Bee iliyokuwa safarini k

Inaelezwa kuwa matumizi ya risasi za mpira ni hatari kwa waandamanaji.

Picha
Dunia imeshuhudia maandamano makubwa mitaani kwenye kipindi cha miezi michache iliyopita, kwa kiasi kikubwa na kusababisha, majeraha na hata vifo. Majeraha kama ya macho yaliyosababishwa na silaha za kudhibiti makundi kama vile risasi za mpira. Kwa mfano nchini Chile, wataalamu wa masuala ya afya na makundi ya haki za binaadamu wanakadiria kuwa takribani watu 220 wamepata majeraha ya macho kwa kipindi cha mwezi mmoja wa maandamano. Na ripoti mpya ya Shirika la Amnesty International, shirika ambalo lilifanya uchunguzi katika nchi hiyo ya kusini mwa Amerika, imeshutumu serikali ya Chile kuwadhuru waandamanaji makusudi. Madhara ya makusudi ''Nia ya vikosi vya usalama vya Chile iko wazi: kuwajeruhi wale wanaoandamana ili kuyapiga marufuku maandamano,'' Erika Guevara Rosas, Mkurugenzi wa shirika la Amnesty International Amerika, amesema kwenye taarifa yake aliyoitoa tarehe 21 mwezi Novemba. ''Mamlaka chini ya Rais Sebastian Pinera zimeendelea na sera ya adhabu kwa za

Kiongozi wa kijiji athibitisha tukio la mama kumuua na kumla mwanae.

Picha
Kumradhi baadhi yenu mnaweza kuona taarifa hii kuwa ya kuogofya Huenda likawa ni jambo lenye ukakasi kwenye masikio, lakini tukio la kushangaza limetokea katika mkoa wa Njombe Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania baada ya mwanamke mmoja kumchinja mwanae wa miaka minne na kisha kula baadhi ya viungo vyake huku vingine vikipotelea porini. Diwani wa kata ya Mavanga eneo la Ludewa mkoani Njombe, bwana Emmanuel Ngalalikwa anasimulia kile kilichotokea: "Baba wa familia ile alienda shambani kama kilomita kumi na mama ndiye alibaki peke yake nyumbani. Na ndio wakati ambao inadaiwa kuwa alimuua mwanae. Tukio hilo linadaiwa kufanyika kati ya siku ya Ijumaa au Jumamosi na liligundulika baada ya mume wake kurudi nyumbani kutoka shambani siku ya jumapili saa 12 jioni. Mume wake aliporejea nyumbani alimkuta mtoto mmoja tu nyumbani na alipomuuliza mke wake mtoto mwingine yuko wapi? akajibiwa kuwa anatakiwa kwenda kulipa mahari akiwa anamaanisha kupeleka ng'ombe na mbuzi kwao. Vilevile mke alida

Surua DR Congo: Takriban watoto 5,000 wafariki kutokana na mlipuko mbaya zaidi wa surua duniani

Picha
Ugonjwa wa ukambi ama Surua umewaua takriban watoto 5000 katika taifa la Jamhuri ya KidemokrasIa ya Congo mwaka 2019, kulingana na mamlaka baada ya ugonjwa huo kusambaa hadi mikoa yote. Takriban watoto 250,000 wameambukizwa mwaka huu pekee. Shirika la afya duniani WHO linasema kuwa ugonjwa huo ndio janga linalosambaa kwa kasi mno. Ugonjwa huo wa surua nchini DR Congo umeua idadi ilio mara mbili ya wagonjwa waliofariki kutokana na ugonjwa hatari wa Ebola katika kipindi cha miezi 15 iliopita. Serikali ya DRC kwa ushirikiano na shirika la afya duniani WHO imezindua chanjo ya dharura mwezi Septemba inayowalenga watoto 800,000. Lakini miundo msingi mibaya, mashambulizi dhidi ya vituo vya afya, mbali na ukosefu wa tiba za mara kwa mara zimekwamisha juhudi za kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo. Watoto milioni 4 tayari wamepewa chanjo, lakini wataalam wameonya kwamba idadi hiyo ni chini ya nusu ya jumla ya watoto nchini humo na kwamba chanjo zilizopo hazitoshi. Wengi ya wale walioathirika na ugon

Maandamano ya Iran: Umoja wa Mataifa umehofia watu kuuwawa.

Picha
Watu kadhaa huenda wakawa wamepoteza maisha nchini Iran tangu siku ya Ijumaa wakati wa maandamano ya kupinga kupanda kwa gharama za mafuta ya petroli, Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia masuala ya haki za binaadamu. Msemaji wake amewataka maafisa usalama kutotumia nguvu kupita kiasi, ikiwemo kufyatua risasi, na ametaka mtandao wa intaneti urejeshwe. Shirika la Amnesty International limesema limepokea ripoti za kuaminika kuwa waandamanaji 106 katika miji 21 wamepoteza maisha. Haijulikani hali ikoje hivi sasa kwa sababu ya kufungiwa kwa huduma ya intaneti, kulikoanza Jumamosi jioni, lakini maandamano yameendelea kufanyika katika miji kadhaa mikubwa na midogo. Maandamano yalizuka siku ya Ijumaa baada ya serikali kutangaza kupanda kwa gharama za petroli kwa 50% hadi kufikia riali 15,000 kwa lita moja sawa na kuwa madereva watapaswa kununua lita 60 kila mwezi kabla ya gharama kupanda kufikia riali 30,000. Rais Hassan Rouhani amesema serikali inafanya hivyo kwa faida ya Umma na kuwa

Simulizi ya mwanamke aliyenusurika kuuawa na mumewe

Picha
Bi Diana Wanjiku Kamande kutoka nchini Kenya ni mama ya watoto wawili ,Anapokumbuka yaliyomkuta tarehe 13 mwezi Aprili 2013, hupatwa na hisia majonzi pamoja na furaha. Hii ni kutokana na tukio la siku hiyo ambapo alinusurika na mauaji ya mtu aliyempenda...mumewe, alimhadithia tukio hilo mwandishi wa Newsday Swahili: Alikutana vipi na mumewe? "Jina langu ninaitwa Diana Wanjiku ...nilikutana na mume wangu kwa jina, Richard Machio, mwaka wa 2003. Nilikuwa nasubiri basi la abiria (matatu) ili linipeleke katika shule niliyokuwa ninasomea. Alikuwa ni mwanaume mrefu wa miraba minne", anasema Diana. "Habari, jina langu ni Richard," alisema ."Mimi ni dereva wa matatu kisha akasita mara mmoja kana kwamba alikuwa hawezi kuzungumza tena "alijitambulisha Diana anasema kuwa moyo wake ulianza kumdunda dunda, na mara moja aligundua kuwa alikuwa amenaswa kwenye lindi la mapnezi na mtu yule. Tangu siku hiyo uhusiano wao wa kimapenzi uliiimarika kwa kasi sana, na tangu walip

Je Afrika inaweza kufanya nini kuwaepusha vijana na uhamiaji?

Mwanamuziki wa Kinyarwanda Mani Martin anawaasa vijana wa Afrika kuacha kufikiria kwamba matumaini yao yako ulaya au Marekani. Katika albumu yake mpya aliyoipa jina la ''Africa ndota'' yaani -Africa ninayoiota katika lugha ya Kiswahili, msanii huyo maarufu sana nchini Rwanda ameelezea namna anavyosikitishwa anasikitishwa na jinsi maelfu ya vijana wa Afrika wanavyofuja pesa wakitaka kwenda kutafuta rizki Ulaya na kupoteza maisha yao katika bahari ya Mediterranean badala ya kuwekeza pesa hizo katika mataifa yao ya Afrika. Mani Martin katika kibao chake ''Afrika Ndota''anaimba ndoto zake kwa bara la Afrika,namna anavyopendelea bara la Afrika kuwa, huku akipinga Waafrika wanaokimbilia barani Ulaya na Marekani wanakodhani watapata maisha bora. Kuhusu wanaokimbia vita na usalama mdogo katika nchi zao Bwana Marte alisema: "Viongozi wa Afrika lazima wafanye juhudi kubwa ili vijana waweze kupata maisha ya ndoto zao pasipo kufikiria kutoroka mataifa yao. Wana

Je vikwazo vya Marekani ndio sababu ya maandamano haya?

Picha
Maandamano yamezuka katika maeneo tofauti nchini Iran bada ya serikali kutangaza ghafla mpango wa kuuza mafuta kwa mgao na kuongeza bei ya bidhaa hiyo. Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la habari la kitaifa bei ya mafuta ilipanda kwa 50% siku ya Ijumaa. Mamlaka imepunguza ruzuku kubwa kwa bei ya petroli kukabiliana na athari ya vikwazo vya Marekani ambavyo vimeathiri vibaya uchumui wa Iran. Iran iliwekewa vikwazo vya kuuza mafuta yake nje ya nchi baada ya Marekani kujiondoa katika mkataba wa kimataifa wa nyuklia mwaka 2018. Shirika la habari la Iran IRNA limeripoti maandamano "makali" katika eneo la Sirjan, kati kati ya Iran, usiku wa Ijumaa huku watu "wakisjhambulia bohari ya kuhifadhi mafuta katika mji huo na kujaribu kuliteketeza moto". Mtu mmoja aliuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa, chombo kingine cha habari kisichokuwa rasmi ISNA kilimnukuu gavana wa jimbo la Sirjan. Maandamano pia yalizuka katika miji mingine kama vile Mashhad, Birjand, Ahvaz, Gachsaran, Abadan,

Jalala kubwa China lajaa kabla ya muda uliopangwa

Picha
Jalala kubwa kabisa la takataka nchini China linaelezwa kujaa, miaka 25 kabla ya muda uliopangwa. Jalala hilo lililo katika jimbo la Shaanxi, lenye ukubwa wa sawa na viwanja 100 vya mpira wa miguu, lilijengwa kupokea tani 2,500 kwa siku. Lakini badala yake lilikuwa likipokea tani 10,000 za takataka kwa siku, kiasi kikubwa kuliko jalala jingine lolote nchini humo. China ni moja ya nchi zinazofanya uchafuzi wa mazingira zaidi duniani, na imekuwa ikihangaika kwa muda mrefu kutatua changamoto zinazozalishwa na watu bilioni 1.4 wa nchini humo. Eneo la takataka lina ukubwa kiasi gani? Jalala kubwa la Jiangcungou lililo kwenye mji wa Xi'an lilijengwa mwaka 1994 kwa lengo la kufanya kazi mpaka mwaka 2044. Jalala hilo linawahudumia zaidi ya watu milioni nane.Lina ukubwa wa karibu mita za mraba 700,000, na kina cha mita 150 na uwezo wa mita za ujazo milioni 34. Mpaka hivi karibuni, Xi'an ni moja kati ya miji michache nchini China ambao kwa kiasi kikubwa inategemea jalala hilo kupokea uch

Kukatikakatika kwa umeme Zimbabwe kumefanya raia nchini humo kutumia nishati ya jua

Picha
Zimbabwe imepiga marufuku kuweka mashine za kupasha moto (heater) ikiwa ni jitihada ya kutunza umeme, Shirika la habari la uingereza Reuters limenukuu shirika la udhibiti wa nishati ya umeme nchini humo. Wasambazaji wa umeme hawataruhusiwa kuunga umeme kwenye maeneo mbalimbali bila kuunga mfumo wa solar kwa ajili ya mashine ya kupashia maji. Zimbabwe imekuwa gizani kwa muda mrefu umeme ukikatika mara kwa mara huku biashara nyingi zikifanyika nyakati za usiku, wakati umeme unapokuwa umewaka. Sababu nyingi zimetolewa kuhusu kukosekana kwa umeme.Kampuni ya serikali ya kusambaza umeme ,Zesa imesema wateja wakubwa hawajalipia huduma za umeme. Wakati huo huo ukame umepunguza kiasi cha maji kwenye bwawa la maji linalozalisha umeme. Kwanini Zimbabwe imefikia hali hii? Zimbabwe inategemea bwawa moja tu la Kariba la kuzalisha umeme lakini limeshindwa kusambaza umeme kama kawaida kwa sababu ya kushuka kwa kina cha maji kulikosababishwa na ukame. Zimbabwe inahitaji umeme wa Megawati 1,700 kila sik

Je, taifa hilo litaweza kupata takwimu sahihi ya watu wenye virusi vya ukimwi?

Picha
Bunge la Tanzania limepitisha muswada wa mabadiliko ya sheria itakayomwezesha mtu kujipima mwenyewe virusi vya ukimwi na pia kushusha umri wa vijana kuweza kupima virusi vya ukimwi bila ya ridhaa ya mzazi, hadi kufikia miaka 15. Naibu Waziri wa Afya Dokta Faustine Ndugulile amesema Tanzania ni moja ya nchi ambazo zimekubali na kuridhia malengo ya dunia yanayojulikana kama 90-90-90, ikimaanisha kwamba asilimia 90 ya Watanzania wanaoishi na virisi vya ukimwi kuweza kupimwa na kutambua hali yao ya maambukizi. Asilimia 90 ya wale waliopimwa waweze kufikiwa na kupata dawa, asilimia 90 ya wale watakaopata dawa kuweza kufubaza virusi vya ukimwi. Hata hivyo amesema yote hayo kuweza kufanikiwa kikamilifu inategemea na asilimia 90 ya kwanza ya watu kupima na kujitambua afya zao. Naibu Waziri wa Afya ameeleza kuwa mabadiliko hayo ya sheria kuhusu ukimwi yamekuja pia kutokana na changamoto zilizopo za upimaji wa virusi vya ugonjwa huo. ''... Changamoto imekuwa wanaume wengi hawajitokezi ku

Victoire Ingebire: Kiongozi wa chama cha upinzani FDU Inkingi nchini Rwanda atangaza kuanzisha chama kingine cha upinzani

Picha
Mwanasiasa wa upinzani nchini Rwanda, Bi. Victoire Ingabire amejiuzulu kuwa mkuu wa chama cha FDU na kuanzisha chama kipya cha kisiasa, chama cha maendeleo na uhuru kwa wote-''DALFA-UMURINZI''(Development And Liberty For All). Ingabire ameeleza sababu zilizompelekea kuchukua hatua hiyo ni kutokana na chama cha FDU kuwa nje ya Rwanda hivyo kinakuwa hakihusiani na hali halisi nchini Rwanda. Katika mazungumzo na waandishi wa habari mjini Kigali, Bi. Victoire Ingabire ameeleza pia kuwa amechoka kuendelea kuongoza chama kwenye mtandao kwa sababu wafuasi wake wengi na wakuu wengine wa chama hicho wako nje ya nchi na kwamba wakati umewadia kuwa na chama kinachobainisha matatizo kikiwa ndani ya nchi. Ingabire ameondoa wasiwasi wa kwamba amekisaliti FDU kwa manufaa ya chama tawala RPF. ''Kuna waliosema kwamba ninakwenda kuwa mpambe wa chama tawala RPF, sio kweli. Ni vizuri watu wafahamu kwamba siasa lazima ipige hatua. Haingewezekana kuendelea kuongoza chama kupitia mtan

Shambulio la kigaidi lauwa watu 38, lajeruhi 63 Burkina Faso

Picha
Waziri wa Ulinzi wa Burkina Faso Moumina Cherif Sy anasema idadi ya waliouliwa kutokana na shambuliao la kigaidi karibu na mgodi wa dhahabu imefikia 38 na wengine 63 wamejeruhiwa. Waziri Sy aliyetembelea eneo shambulio lilitokea katika jimbo la mashariki ya mji mkuu wa Wagadougou anasema maafisa wa uokozi wangali wanawatafuta wachimba migodi wengine ambao bado hawajulikani walipo. Kampuni ya Canada ya Semafo inayosimamia kazi za mgodi huo imeeleza Ijumaa kwamba mabasi yake matano yaliyo kuwa yanawasafirisha wafanyakazi kuelekea kazini yalishambuliwa na wanamgambo wasiojulikana wa makundi ya wafuasi wa itikadi kali za Kiislamu yanayoendesha shughuli zake kaskazini na mashariki ya Burkina Faso. Taifa hilo la Afrika Magharibi linalofahamika kwa utulivu wake limekuwa likipambana na mashambulizi ya kigaidi yaliyowasababisha maelfu ya watu kukimbia makazi yao tangu mwanzoni mwa mwaka huu kulingana na mashirika ya kimataifa ya huduma za dharura.

Aacha kazi ya benki kuwa mpishi

Picha
Pamela Oduor ni muanzilishi wa kundi la Lets Cook nchini Kenya ambalo linaangazia mapishi ya jamii tofauti. Alianza kundi hilo miaka mitatu iliyopita baada ya kuamua kuacha kazi ya benki ili kuangazia kitu anachopenda, upishi. Bi Pamela alikua miongoni mwa majina 100 ya watu walio na mashabiki wengi katika mtandao wa kijamii wa Facebook mwaka jana.

Mfichua siri atilia shaka mfumo wa oksijeni wa ndege ya Boeing 787

Picha
Mfichua siri wa Boeing amedai kuwa abiria katika ndege ya 787 Dreamliner huenda wakaachwa bila hewa ya oksijeni ndege hiyo ikipata ghafla hitilafu ya kiufundi. John Barnett anasema uchunguzi umebaini kuwa hadi robo ya mfumo wa oksijeni una hitilafu na kwamba huenda ikakosa kufanya itakapohitajika. Pia anadai kuwa vipuri vya ndege vilivyo na kasoro vimewekwa wakati ndege hiyo ilipokuwa ikiundwa katika kiwanda cha Boeing. Boeing imepinga madai hayo ikisema kuwa ndege zake zote zinaundwa kwa kuzingatia viwango vy usalama vya hali ya juu. Kampuni hiyo imejikuta mashakani siku za hivi karibuni baada ya ajali mbili mbaya zilizohusisha ndege yake ya 737 Max -iliyokuwa ya shirika la ndege la Ethiopia na kupata ajali mwezi Machi na ajali ya Lion Air ya Indonesia mwaka jana. Bwana Barnett, ni injinia wa zamani wa udhibiti wa ubora, aliyefanya kazi na Boeing kwa miaka 32, hadi alipostaafu kwa misingi ya afya yake mwezi March mwaka 2017. Kutoka mwaka 2010 aliajiriwa kama meneja anayesimamamia masu

Mshambuliaji kinara wa Tanzania Mbwana Samatta afunga bao la kufutia machozi Genk ikilazwa 2-1 na Liverpool.

Picha
Mshambuliaji kinara wa klabu bingwa ya Ubelgiji KRC Genk na nahodha wa Tanzania, Mbwana Samatta, hatimaye amepachika goli dhidi ya vigogo wa England klabu ya Liverpool jana usiku. Goli hilo lilikuwa likisubiriwa kwa hamu na mashabiki wa mpira wa miguu nchini Tanzania. Hata hivyo, matokeo ya mwisho ya mchezo huo wa Klabu Bingwa Ulaya yalikuwa mabaya kwa Genk kwa kulazwa kwa goli 2-1. Samatta, aliunganisha kwa kichwa mpira wa kona mpaka wavuni katika dakika ya 40 ya mchezo. Mshambuliaji huyo ambaye ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kucheza michuano hiyo mikubwa zaidi ya vilabu barani Ulaya tayari ameshapachika magoli mawili katika mechi nne. Katika mechi ya mkondo wa kwanza dhidi ya Liverpool, Samatta pia alipachika bao la kichwa ambalo hata hivyo lilikataliwa baada ya kumchezea rafu mchezaji wa Liverpool kabla ya kupachika bao. Goli la kwanza la Liverpool katika mchezo huo lilifungwa na Georginio Wijnaldum katika dakika ya 14 baada ya safu ya ulinzi ya Genk kufanya uzembe wa ku

Wabunge wa Tanzania waanza kutumia Tablet, je zina manufaa gani?

Picha
Wabunge nchini Tanzania wataanza kutumia tablet kwa ajili ya kazi za bunge, huku bunge hilo likiondokana na matumizi ya karatasi. Wabunge walikabidhiwa vifaa hivyo Jumatatu kabla ya kuanza kwa vikao Jumanne mchana katika mji mkuu wa nchi hiyo Dodoma. Katika akaunti ya rasmi ya Twitter ya bunge zilitumwa picha za wabunge wakipokea Tablet na ujumbe uliosema wanalenga kuachana na matumizi ya karatasi : Katibu wa Bunge Stephen Kigaigai alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kuhifadhi pesa ambazo serikali imekuwa ikizitumia kuchapisha na kunakili nyaraka za serikali. " Hata hivyo tumeziomba wizara husika kuja na baadhi ya nyaraka kwa ajili ya kuweka rekodi yake. Kwa mfano kwa matumizi katika maktaba," alisema. Bwana Kigaigai anasema imekuwa ikichapisha nakala 500 za nyaraka za kutumiwa katika shughuli za bunge kwa siku lakini kwa sasa zitakuwa chini ya nakala 10. Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kuwa wabunge wote leo wameingia bungeni na Tablet. Spika wa bunge hilo Job Ndugai a

Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu 04.11.2019: Emery, Lallana, Mourinho, Allegri, Haaland, Saliba, Alena.

Picha
Unai Emery amepewa mwezi mmoja kuokoa kazi yake kama mkufunzi wa Arsenal. (Mirror) Kiungo wa kati wa England Adam Lallana, 31, analengwa na vilabu vya China na ligi kuu ya soka, huku mkataba wake na Liverpool ukielekea kumalizika. (Telegraph) Arsenal imejitenga na tetesi kuwa huenda ikamuajiri Jose Mourinho kama kocha wao mpya. (ESPN) Mkuu wa soka wa Arsenal, Raul Sanllehi, ameripotiwa kuonekana akila chakula cha jioni na Mourinho lakini wawili hao hawajazungumza kwa miaka kadhaa.(London Evening Standard) Kocha wa zamani wa Juventus Max Allegri, ambaye aliwahi kuhusishwa na Arsenal, anapigiwa upatu kujiunga na Bayern Munich baada ya Niko Kovac kuondoka. (Bild, via Football Italia) Meneja wa Leipzig Ralf Rangnick pia amehusishwa na nafasi ya ukufunzi iliyoachwa wazi Bayern Munich - naye Jose Mourinho akiwa mmoja wa wale wanaopigiwa upatu kuchukua nafasi hiyo. (London Evening Standard) Salzburg bado haijapokea ofa kutoka usajili wa mshmbuliaji wa Leeds-mzaliwa wa Norway, Erling Braut Haa