Zimbabwe kuwafidia wazungu waliopokonywa mashamba yao

Serikali ya Zimbabwe imesema kwamba wakulima wazungu ambao walipokonywa ardhi zao kati ya mwaka 2000 na 2001 wanaweza kutoa maombi ya kurudishiwa ardhi hizo chini ya mpango mpya wa mageuzi ya sera ya ardhi.
Ikiwa ardhi haitaweza kurudishwa, wakulima hao watapewa ardhi sehemu nyingine, kwa mujibu wa taarifa ya pamoja iliyotolewa na Mawaziri wa Fedha Mthuli Ncube na wa Ardhi Anxious Masuka.
Mawaziri hao wamesema watafutilia mbali barua zilizowapa idhini wakulima weusi kuchukua ardhi hizo.
Walisema wakilima wazungu ambao ardhi zao zilichukuliwa na serikali na ambazo hazijatolewa wanaweza kutoa maombi ya kuzikodisha kwa miaka 99.
Wakulima wazungu 3,500 walifurushwa kutoka kwa mashamba yao wakati wa marekebisho tata ya sera ya ardhi.
Serikali ya Zimbabwe mwezi Mei ilikubali kuwafidia dola bilioni 3.5 wakulima wazungu ambao ardhi zao zilichukuliwa enzi za utawala wa rais wa zamani wa nchi hiyo marehemu Robert Mugabe.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?