Wakenya sasa ruksa kushiriki mazishi ya waliokufa na corona

Kuanzia sasa raia wa Kenya wataweza kushiriki shughuli za mazishi ya wapendwa wao waliofariki kutokana na virusi vya corona baada ya serikali kulegeza masharti tofauti na awali ambapo walipiga marufuku.
Awali ndugu wa karibu wa mtu aliyekufa kwa corona hakuruhusiwa kufanya chochote zaidi ya kuangalia kwa mbali wakati maafisa wa afya waliojihami kwa mavazi maalum wakifanya shughuli za mazishi.
Maafisa wa afya wamesema kuwa miili ya marehemu waliokufa kutokana na maambukizi ya virusi vya corona haiwezi kuambukiza virusi hivyo.
Shirika la afya duniani (WHO) na kituo cha kudhibiti magonjwa Afrika CDC hawajasema bado kama maiti haiweza kuambukiza Covid-19, lakini wamebadilisha utaratibu na kuruhusu familia kuaga wapendwa wao.
Nchini Kenya', maofisa wa afya watakuepo katika mazishi ili kutoa muongozo na kuhakikisha usalama unazingatiwa.
"Tutaruhusu shughuli zote za mazishi za kidini na kitamaduni kufuatwa kulingana na tamaduni za marehemu,"
Serikali imekiri kuwa zuio waliloliweka mwezi uliopita lilikuwa gumu kufuatwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?