Marekani yazingirwa na virusi wakati ikisherehekea uhuru

Rekodi mpya ya idadi ya virusi vya corona imeweka kiwingu mwanzoni mwa  herehe za uhuru nchini Marekani wakati ongezeko la  maambukizi lailazimisha Uingereza kuwaweka wasafiri kutoka Marekani kwenye orodha mbaya.
Wakati fukwe zimefungwa  kutoka  eneo  moja  la  pwani  hadi  jingine  na  maafisa wakiwataka  Wamarekani  kubakia  majumbani  mwao, hali isiyokuwa  ya  furaha  kuelekea katika  kile  ambacho  kwa  kawaida  ni  mwishoni  mwa  juma kunakochomwa  nyama  na hali  ya  hewa ya  jua  imelemea  mapambano  ya  kudhibiti ugonjwa  wa  COVID-19  katika kitovu  cha  janga  hilo  duniani.
Ni idadi  usiyoweza  kuamini,"  amesema  Faisal Masud , mkurugenzi wa  matibabu  katika hospitali  ya  Methodist mjini  Texas, ambayo  maafisa  wamesema  inakaribia  kabisa kuzidiwa  na  wagonjwa.
Ukigusa  karibu  kila  nchi  duniani  tangu  kujitokeza  nchini  China  mwishoni  mwa  mwaka jana, virusi  vya  corona  vimewaambukiza  kiasi  ya  watu  milioni  10.9  na  kuwauwa  watu 522,000 duniani, na  kuzima  uchumi  uliokuwa  hapo  kabla  ukikua  kwa  kasi na kusababisha  maisha  ya  watu  kuzimika.
Lakini  wakati  Ulaya  na  sehemu  nyingi  za  Asia  kwa  kiasi  kikubwa  zimeweza  kudhibiti virusi  hivyo  vya  corona , kwa  kiasi  kikubwa Uingereza  inajitayarisha  kufungua  biashara zake, mikahawa  na  cinema,  lakini  nchini  Marekani  ugonjwa  huo  umewauwa  karibu watu 130,000 huku  kukiwa  na  ongezeko  kubwa  la  kesi  mpya  za  maambukizi  ambapo mtaalamu  wa  ngazi  ya  juu  wa  magonjwa  ya  kuambukiza Anthony Fauci  amesema "unaiweka  nchi  nzima  katika  hatari."

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?