WARIDI WA BBC: ‘Unene huu umenipa umaarufu na nimejikubali’


Janet Wambui ni mwanamke wa miaka 41, mzaliwa wa Kenya . Kutokana na muonekano wake wa kuwa na mwili mnene kupita kiasi tangu akiwa binti mdogo alipewa majina mengi ambayo ameendelea kuyatumia kama msanii nchini humo. Mwili wake umesaidia kuwa msanii kutokana na nafasi anazoigiza zinazohitaji mwanamke mwenye umbo kubwa.

Ni kwanini wananiita ‘momo au biggie’

Mama huyu wa watoto wawili anasema kuwa amekuwa na mwili mkubwa tangu alipokuwa mtoto mdogo, anapoulizwa iwapo unene huu ni kitu ambacho kiko kwenye familia yao anasema kuwa huenda alirithi muonekano huo kutoka kwa baba yake mzazi ambaye pia ni mnene wa mwili .

”Kwetu tumezaliwa tukiwa watoto sita, mmoja wetu alifariki kwa hiyo tumesalia watano, ila kwa wote mimi ndio mtoto pekee niliyezaliwa mnene nadhani kwamba nilirithi kwa baba yangu, ila halinisumbui kabisa ”anasema Wambui. 

Anasema kuwa jina lake maarufu la MOMO lilitokana na hatua yake ya kuingia kwenye sanaa ya kuigiza katika nyimbo za kiasili za jamii ya Agikuyu nchini Kenya. Video ya kwanza ambayo ilimpatia umaarufu aliigiza kama mwanamke mnene, wimbo wenyewe ukifahamika kama MOMO unaeleza pandashuka za kuwa mwanamke mnene, baada ya wimbo huo kuzinduliwa ndipo watu nchini Kenya walianza kumfuatilia kama msanii.


”Nadhani wengi walikuwa wanazuzuliwa na muonekano wangu , ni kitu ambacho nilikizoea tangu nikiwa binti mdogo .Nilizoea kutizamwa kila nilipokuwa ninatembea. Na kwa hiyo sijaona ugumu wa kuwa mnene bali nafurahi kwani ni muonekano ambao umenipa nafasi ya kutafuta riziki ”anasema Wambui. 

Baada ya wimbo huo wa Momo , alianza kupata nafasi kadha wa kadha za kuigiza ikiwemo kwenye baadhi ya tamthilia za Kenya, na pia kuigiza nafasi ambazo zinaangazia maisha ya watu wanene katika vipindi na wasanii mbalimbali nchini Kenya.

Maisha ya utotoni

Mwanadada huyu anazungumza kwa njia ya kujikubali anaposimulia maisha yake ya utotoni , alilelewa kama watoto wengine ila anakumbuka kuwa yeye alikuwa mnene tangu alipoingia shule ya chekechea, shule ya msingi na hata sekondari .

”Nakumbuka mama akiniwekea bakuli mbili za chakula, kwa kuwa shule yetu ilikuwa mbali nilikuwa natembea huku nikila chakula changu , bakuli ya pili ilikuwa ni chakula cha mchana na mama alihakikisha kuwa mwalimu alikuwa anakiweka nisije nikakila chote ”anakumbuka Wambui 

Shuleni anasema kuwa hakupata ugumu , kwani alikubalika na waalimu na hata wanafunzi. Aidha anasema kuwa hatua ya kwanza ya mtu kukubalika na wengine licha ya utofauti wake na watu wanaomzunguka ni pale yeye mwenyewe anapojikubali na kuishi bila wasiwasi wa muonekano wake .

Huku akitabasamu anaeleza kuwa mambo ambayo aliyafurahia katika shule ya sekondari ilikuwa pamoja na kuwa aliteuliwa kama kiranja wa bweni , anasema kuwa muonekano wa mwili mnene ulimuweka kwenye nafasi nzuri ya kuwa kiongozi ambaye alikuwa anahakikisha kuwa wanafunzi wenzake wanamfuatilia sheria za bweni na hata za shule kijumla. 

”Nikiwa sekondari , nilikuwa nafurahi kwa kuwa unene wangu ulizuia wanafunzi kuiba nguo zangu kwani hazingewatosha , nilikuwa mwanafunzi mnene zaidi shuleni sasa mwanafunzi akiiba nguo zangu au soksi atazivalia wapi ”anasema Wambui 

Maisha ya utu uzima

Janet

janet

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?