Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Papua New Guinea: Waziri ajiuzulu kwa kusafiri kifahari kuhudhuria kutawazwa kwa Mfalme Charles III


Waziri wa mambo ya nje wa Papua New Guinea amejiuzulu baada ya kashfa ya matumizi ya fedha ya ujumbe rasmi wa nchi hiyo uliohudhuria kutawazwa kwa Mfalme Charles III. 

Justin Tkatchenko alisafiri na binti yake Savannah, ambaye alichapisha kwenye mtandao wa TikTok kuonyesha safari yake kwenye ndege ya daraja la kwanza pamoja na kuonekana akifanya manunuzi mengi nchini Singapore. 

Siku ya Jumatano, aliwataja wakosoaji wake kuwa "wanyama waliopitwa na wakati". Maoni ya Bw Tkatchenko yalizua maandamano katika mji mkuu wa Port Morseby siku ya Ijumaa nje ya Ikulu ya Bunge. 

Papua New Guinea ni taifa la Jumuiya ya Madola huko Pasifiki ambalo Mfalme Charles ni mkuu wake wa serikali. 

Bw Tkatchenko alisema katika taarifa Ijumaa kwamba "amejiweka kando" baada ya kushauriana na Waziri Mkuu James Marape.

Aliongeza kuwa anataka kuhakikisha matukio ya hivi majuzi hayaingiliani na ziara rasmi za Rais wa Marekani Joe Biden na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi.

Bw Tkatchenko na bintiye walikosolewa kwa kusafiri na maafisa wasiopungua 10 kushuhudia kutawazwa kwa Mfalme Charles, kwa gharama ya karibu dola 900,000, kwa mujibu wa gazeti la Post-Courier. 

Msemaji wa serikali Bill Toraso alilithibitishia shirika la habari la Reuters kuwa wafanyakazi wake 10 walikuwa wamesafiri kwenda London, pamoja na wageni 10. Katika video hiyo ambayo imefutwa, Savannah alirekodi ziara yake katika maduka ya kifahari ya Singapore na mlo wake katika mgahawa wa daraja la kwanza alipokuwa njiani kuelekea London.

  • Turkey

    Rais Erdogan wa Uturuki anakabiliwa na upinzani mkali zaidi katika maisha yake ya siasa baada ya upinzani kuungana dhidi yake katika uchaguzi wa Jumapili. 

    Mpinzani wake mkuu Kemal Kilicdaroglu alifika mbele ya umati wa wafuasi wake siku ya Ijumaa, akiwa na washirika kutoka katika vyama vingine kuonyesha kuungana pamoja. 

    Huku mvua ikinyesha mjini Ankara, aliapa kurejesha "amani na demokrasia". Mtu huyo anataka wapiga kura kumuondoa madarakani Rais Recep Tayyip Erdogan aliyedumu kwa miaka 20.

    Alisema ameiingiza Uturuki katika changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na uchumi na mfumuko wa bei uliokithiri na janga la tetemeko la ardhi la Februari.

    Masuala haya yametawala kampeni hii kali ya urais na bunge. Akiwa na umri wa miaka 74, kiongozi huyo wa upinzani mara nyingi anatajwa kuwa mzungumzaji mpole, lakini alitoa hotuba yenye nguvu kwa hadhira inayoamini kuwa hili ndilo tumaini lao bora hadi sasa la kurudisha madaraka kutoka kwa rais ambaye ameyaondoa bungeni na kujiongezea kwakwe kwa kiasi kikubwa. .

  • Russia

    Wizara ya mambo ya nje ya Afrika Kusini inasema balozi wa Marekani "ameomba radhi" kwa kudai kuwa nchi hiyo iliiuzia Urusi silaha.

    Siku ya Alhamisi Reuben Brigety alidai meli ya Urusi ilikuwa imesheheni risasi na silaha huko mjini Cape Town Disemba mwaka jana.

    Afrika Kusini inasema haina rekodi ya mauzo ya silaha na Rais Cyril Ramaphosa ameagiza uchunguzi ufanyike.

    Siku ya Ijumaa msemaji wa masuala ya usalama wa taifa wa Ikulu ya White House hakusema lolote kuhusu maelezo ya madai hayo.

    Lakini John Kirby alisema ni "suala zito" na Marekani imekuwa ikizitaka nchi mara kwa mara kutounga mkono vita vya Urusi nchini Ukraine.

    Akiandika kwenye mitandao ya kijamii baada ya kukutana na wizara ya mambo ya nje, Bw Brigety alisema "anashukuru kwa fursa ya... kurekebisha maoni yoyote potofu yaliyotokana na matamshi yangu hadharani".

    Alisema katika mazungumzo hayo "uwepo wa ushirikiano mkubwa kati ya nchi zetu mbili na ajenda muhimu ambayo marais wetu wametupa".

    Wakati huo huo waziri wa baraza la mawaziri la Afrika Kusini alikosoa "diplomasia ya aina hiyo, akisema Afrika Kusini haiwezi "kuonewa na Marekani".

  • Maoni

    Machapisho maarufu kutoka blogu hii

    Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

    Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?