Raheem Sterling: Kwanini mashabiki wa Man City hawamkubali sana’ Sterling? Uchambuzi wa Micah Richards

Nilikuwa katika uwanja wa Etihad siku ya Jumamosi wakati Raheem Sterling alipopoteza nafasi nzuri dhidi ya Watford. Ungewasikia mashabiki walionizunguka walivyokuwa wakigugunia na kupiga kelele 'hafai' au 'mtoe'.

Manchester City walikuwa wanaongoza mabao 3-1 wakati huo na Sterling alikuwa akicheza vizuri sana. Hilo lilikuwa shuti lake la kwanza katika mchezo huo na, ingawa sikusema chochote kwa watu walio karibu nami, nilikuwa nikifikiria tu kwamba walihitaji kutulia na kuwa na subra.

Hata hivyo hilo sio jambo jipya. Sterling anaonekana kushambuliwa zaidi kuliko mchezaji mwingine yeyote wa City. Haijalishi ni mabao mangapi anayofunga au mambo mazuri anayofanya katika mchezo - ikiwa atakosa, ni kawaida kwa Sterling sivyo?

Manchester City forward Raheem Sterling

CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, 

Sterling amefunga mabao 10 katika ligi kuu England katika michezo 26 msimu huu, goli moja nyuma ya wachezaji wanaoongoza kwa mabao msimu kwenye timu ya City, Riyad Mahrez and Kevin de Bruyne wenye mabao 11 kila mmoja.

Bila shaka ninaelewa kwa nini anabebeshwa lawama na mashabiki wakati anapofunga mabao magumu lakini anakosa nafasi za wazi na rahisi kufunga. 

Mashabiki wanakosea, pengine pia hatothaminiwa vizuri bila kujali ni mabao mangapi anayofunga au kufanya - au ni mataji mangapi anayoisaidia City kushinda.

Takwimu zake ni za kushangaza. Tangu alipojiunga na City mwaka 2015 amefunga mabao 112 katika mechi 286 alizocheza katika Ligi Kuu na Ligi ya Mabingwa, na kutoa pasi 55. Hilo ni jambo kubwa kwa kwa mtu ambaye mara nyingi hutumiwa kama mshambualji wa pembeni .

Ana majukumu makubwa kwa timu, kutokana na kasi na mikimbio yake inayoweza kuleta madhara uwanjani. 

Raheem Sterling has won three Premier League titles

CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, 

Raheem Sterling ametwaa mataji matatu ya ligi kuu England akiwa na City, mwaka 2018, 2019 na 2021, pamoja na taji moja la FA Cup na manne ya League Cups.

Kama ilivyo kwa Gabriel Jesus, Sterling ana mkataba unaomalizika mwaka 2023 na mpaka sasa wachezaji hao ambao hawajaongeza mikataba yao, wanahusishwa kuhamia vilabu vingine.

Arsenal wanadaiwa kukaribia kumnasa Jesus na nilisoma habari wiki iliyopita kuhusu Sterling kutakiwa na AC Milan, lakini kwangu mimi ni suala rahisi - City wanapaswa kujaribu kuwabakiza wote wawili kama wanaweza.

Wachezaji wote hawa wawili ni hodari na wanafanya kazi kwa bidii, na wanaweza kucheza kwenye wing azote katikati.

Sterling kuendelea kuimarika

Bado ana umri wa miaka 27 tu. Hakika, kutakuwa na wakati ambapo anapaswa kufunga zaidi, lakini napenda kusema hilo linaweza kuwa hoja kwa wachezaji wengine wachache wa City kutokana na idadi ya nafasi za kufunga ambazo timu inatengeneza.

Sterling aliigharimu City kitita cha £49m alipojiunga kutoka Liverpool mwaka 2015. Unaweza kuona ni gharama kiasi gani kumleta mchezaji mwingine ambaye angeweza kuwa msaada kama anavyofanya Sterling sasa.

Raheem Sterling

CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, 

Sterling alifunga mabao matatu kwenye Euro 2020, dhidi ya Croatia, Czech Republic na Ujerumani, na kuisaidia England kufika fainali

Sterling kucheza dhidi ya Real Madrid leo?

Real Madrid ni wageni wa City leo katika uwanja wa Etihad, katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Pep Guardiola na ana maamuzi magumu ya kufanya. Mara nyingi hulazimika kuacha washambuliaji wake wengi nje.

Mara ya mwisho kwa City kucheza na Real katika uwanja wa Etihad ilikuwa ni msimu wa 2019-20. Katika mechi ya mkondo wa pili katika uwanja wa Etihad, Guardiola aliamua kutumia washambuliaji watatu mbele, Jesus, Foden na Sterling, kasi yao na kukaba kuanzia mbele kuliwafanya Real Madrid kuwa na kibarua kigumu, City ilishinda 2-1.

Graphic showing Man City's starting XI v Real Madrid in the second leg of their Champions League last-16 tie on 7 August 2020: Ederson, Walker, Fernandinho, Laporte, Cancelo, De Bruyne, Rodri, Gundogan, Sterling, Foden, Jesus

CHANZO CHA PICHA, BBC SPORT

Wakati huu, kama City wangekuwa imara katika safu ya ulinzi nadhani Guardiola angemwacha Sterling nje ya kikosi cha kwanza, aanze safu ya ushambuliaji yenye Foden, Jesus na Rihad Mahrez, na kuangalia namna ya kumtumia akitokea benchi.

Lakini kutokana kutokuwepo kwa mlinzi tegemeo wa pembeni, Joao Cancelo, mwenye kadi na mwingine, Kyle Walker, mwenye majeraha huenda asicheze, City inaweza kuwa na udhaifu wa kujihami kwenye eneo lake la ulinzi kila upande, kulia na kushoto.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?