Marekani yaionya India dhidi ya kuungana na Ukrane.

Newsday Swahili

Mshauri mkuu wa Rais Joe Biden wa masuala ya kiuchumi amesema kuwa Marekani iliionya India dhidi ya kushirikiana kwa karibu sana na Urusi kufuatia uvamizi wa Ukraine.


"Ujumbe wetu kwa serikali ya India ni kwamba gharama na matokeo kwao ya kuhamia katika upatanishi wa kimkakati ulio wazi zaidi na Urusi itakuwa muhimu na ya muda mrefu," Mkurugenzi wa Baraza la Kitaifa la Uchumi la White House Brian Deese aliwaambia waandishi wa habari Jumatano.


"Kwa hakika kuna maeneo ambayo tumekatishwa tamaa na maamuzi ya China na India, katika muktadha wa uvamizi," aliongeza.India imekataa kuweka vikwazo dhidi ya Urusi, kama nchi zingine zilivyofanya.


Nchi hiyo, ambayo Marekani inaiona kuwa ni kinzani dhidi ya uwezo wa China barani Asia, ndiyo nchi inayoagiza zaidi silaha za Urusi kutoka nje ya nchi, kulingana na Bloomberg.Inakuja baada ya Naibu Mshauri wa Usalama wa Kitaifa wa Marekani Daleep Singh kufanya ziara rasmi nchini India wiki iliyopita.


"Kile ambacho Daleep aliweka wazi kwa wenzake wakati wa ziara hii ni kwamba hatuamini ni kwa manufaa ya India kuharakisha au kuongeza uagizaji wa nishati ya Urusi na bidhaa nyingine," msemaji wa White House Jen Psaki alisema baada ya Bw Singh kurejea wiki hii.


Follow us on Facebook

Follow us on Instagram

Follow us on Twitter

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?