Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2020

Virusi vya corona: Dkt Anthony Fauci atahadharisha kuwa Marekani itakuwa na visa 100,000 kwa siku

Picha
Mtafiti mkuu wa magonjwa Dkt Anthony Fauci ameliambia bunge la seneti nchini Marekani kuwa ''hatashangazwa'' ikiwa maambukizi mapya yatafikia 100,000 kwa siku. ''Ni wazi hatujaudhibiti kwa sasa,'' alikiri, akitoa tahadhari kuwa haitoshi kwa Wamarekani kuvaa barakoa na kutochangamana Katika hotuba yake, alisema kuwa karibu nusu ya watu wote wapya walioambukizwa wanatoka katika majimbo manne. Awali, Gavana wa New York alisema karibu nusu ya Wamarekani wote lazima wajiweke karantini ikiwa watatembelea jimbo hilo. Siku ya Jumanne, idadi ya watu walioambukizwa iliongezeka kwa zaidi ya 40,000 kwa siku moja kwa mara ya nne katika kipindi cha siku tano. Ongezeko- ambalo limekuwa kubwa katika majimbo ya Kusini na Magharibi limelazimu majimbo karibu 16 kusitisha na kutazama upya mipango yao ya kuyafungulia majimbo hayo, kwa mujibu wa shirika la habari la CNN. Florida, Arizona,Texas na California ni majimbo manne yaliyotolewa mfano na Dkt

Virusi vya corona: China yatumia dawa ya asili huku virusi vikichacha

Picha
Wakati wanasayansi wakipambana kutengeneza chanjo ya virusi vya corona, China ambayo imekuwa kinara katika utengenezaji wa dawa za asili imetengeneza dawa ya asili inayojulikana kama 'Traditional Chinese medicine (TCM)' ili kutibu ugonjwa wa corona. Gazeti moja lilizinduliwa na serikali ya China lilidai kuwa 92% ya wagonjwa wa corona wa nchi hiyo walitibiwa na dawa hiyo. TCM ni dawa ya kale zaidi duniani ambayo imetengenezwa kwa mitishamba. Dawa hiyo ni maarufu sana nchini China licha ya kwamba ilizua mjadala kuhusu matumizi yake mtandaoni. Wataalamu wanasema China inajaribu kuisambaza dawa hiyo ya TCM ndani ya nchi na nje ya nchi lakini wataalamu wa afya bado hawaamini uwezo wake wa kutibu. Ufanisi wake kwa ujumla Wizara ya afya ya China imeweka kitengo maalum cha TCM pamoja na muongozo wa kukabiliana na virusi vya corona, wakati televisheni ya taifa ilidai kuw adawa hiyo ilifanya kazi katika mlipuko wa miaka ya nyuma kama Sars mwaka 2003. Kuna da

Kiongozi wa upinzani Malawi Lazarus Chakwera ashinda uchaguzi

Picha
Kiongozi wa upinzani nchini Malawi Lazarus Chakwera ameshinda duru ya pili ya uchguzi wa urais, maafisa wanasema. Alimshinda aliyekuwa rais wa nchi hiyo Peter Mutharika kwa asilimia 58.57 ya kura katika uchaguzi wa Jumanne, tume ya uchaguzi ilitangaza usiku wa Jumamosi. Mwezi Februari, Mahakama ya katiba nchini Malawi ilifutilia mbali ushindi wa Mutharika katika uchaguzi wa Mei 2019, kutokana na dosari zilizokumba uchaguzi huo. Nchi iligawanyika vikali wiki kadhaa kuelekea uchaguzi wa marudio. Malawi ni nchi ya kwanza Afrika kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais na kuandaa duru ya pili ambayo upinzani ukanyakua ushinda. Bw. Chakwera anatarajiwa kuapishwa leo Jumapili. Kama ilivyotokea Malawi nchini Kenya upinzani ulipinga matokeo ya uchaguzi wa urais mwaka 2017 na kushinda mahakamani. Hata hivyo mgombea wa upinzani Raila Odinga alisusia duru ya pili ya uchaguzi. Baada ya matokeo rasmi kutangazwa usiku wa Jumamosi, Bw. Chakwera alisema ushindi wake ni &quo

Afrika Kusini yalegeza zaidi marufuku za COVID-19

Picha
Katika hatua nyingine Afrika Kusini imesema itaruhusu kufunguliwa tena kwa mikahawa na kumbi za starehe kuanzia Jumatatu inayokuja katika hatua ya hivi karibuni kabisa ya kulegeza vizuizi vya kukabiliana na virusi vya corona licha ya kuongezeka visa vya maambukizi nchini humo. Taarifa iliyotolewa na waziri wa Utalii Mmamoloko Ngubane imesema uamuzi huo umefikiwa ili kunusuru sekta ya utalii na biashara baada ya takwimu mpya kuonesha kiasi nafasi 600, 000 za ajira zinaweza kupotea iwapo vizuizi vilivyopo vitaendeela hadi mwezi Septemba. Ngubane amesema kumbi zote za starehe zitaruhusiwa kufanya kazi kwa asilimia 50 ya uwezo wake huku mikahawa na vituo vya kuuza chakula itaruhusiwa kupokea wateja lakini uuzaji wa pombe bado umepigwa marufuku. Hadi sasa Afrika Kusini imerikodi zaidi ya visa 118,000 vya maambukizi ya virusi vya corona pamoja na vifo 2,200 huku idadi ya maambukizi mapya ilipanda ghafla siku ya Alhamisi na kufikia visa 6500 kwa siku kutoka visa 1000 mwezi Aprili.

Umoja wa Ulaya wakosa mwafaka wa kufungua mipaka kwa wageni

Picha
Mataifa ya Umoja wa Ulaya jana yameshindwa kufikia makubaliano juu ya orodha ya nchi zilizo salama ambazo raia wake wangeweza kuruhusiwa kuanza kusafiri ndani na nje ya kanda hiyo kuanzia mwezi Julai. Mabalozi wa nchi 27 wanachama wa Umoja wa Ulaya walikutana m jini Brussels jana kutayarisha mwongozo wa kuruhusu baadhi ya raia wa mataifa kadhaa duniani kuanza kuingia tena kwenye mataifa ya kanda hiyo bila ya masharti ya kukaa karantini. Hata hivyo wanadiplomasia hao wameomba muda zaidi wa kushauriana na serikali za mataifa yao kabla ya kufikia uamuzi wa orodha ya nchi 10 hadi 20 zilizopendekezwa  na uamuzi unatarajiwa kutolewa baadae hii leo. Duru kutoka mjini Brussels zimesema orodha ya mataifa iliyowasilishwa kwa mabalozi hao haikuzujumuisha Marekani, Brazil wala Urusi, nchi ambazo bado zina kiwango kikubwa cha maambukizi ya virusi vya corona. Kulingana na maafisa wawili wa Marekani abiria kutoka Marekani wataruhusiwa kusafiri ikiwa watatimiza masharti kadhaa ikiwemo

Burundi: Pierre Nkurunziza kuzikwa leo

Picha
Mwili wa aliyekuwa rais wa Burundi hayati Pierre Nkurunziza unazikwa leo kwenye makaburi ya mji wa Gitega ,mji mkuu wa kisiasa ulioko katikati mwa Burundi Hafla ya mazishi zinatarajiwa kuongozwa na rais mpya jenerali Evariste Ndayishimiye na wakuu wengine wa serikali. Hayati Nkurunziza alifariki dunia tarehe 8 mwezi huu ,miezi miwili kabla ya kukabidhi madaraka kwa mrithi wake kufwatia uchaguzi uliofanyika mwezi wa tano. Kwa mjibu wa tangazo lililotolewa na serikali ya Burundi, hafla itaanzia kwenye 'hospital du Cenquantenaire Twese Turashoboye' iliyoko kwenye mkoa wa Karusi ambako maiti yake imehifadhiwa. Mlolongo wa magari yatakayosindikiza maiti yake utatoka kwenye hospitali hiyo utatoka Karusi na kuelekea katika mji wa Gitega ambao ni mji mkuu wa kisiasa katikati mwa Burundi. Wananchi wameomba kusimama kwenye barabara kumuaga marehemu. Kunatarajiwa hafla fupi ya jeshi kumtolea heshma za mwisho kwenye uwanja wa mpira wa Ingoma mjini Gitega,kabla ya

Uchaguzi wa Tanzania 2020: Nini mustakabali wa upinzani baada ya 'kifo' cha UKAWA?

Picha
Imesalia miezi mitatu kufanyika uchaguzi mkuu wa urais, ubunge na madiwani nchini Tanzania ifikapo mwezi Oktoba mwaka huu. Hekaheka za kisiasa zimepamba moto miongoni mwa wanasiasa, vyama vya upinzani na chama tawala CCM kuanza michakato ya kupata wawakilishi wao wa majimbo mbalimbali, huku hatima ya uliokuwa muungano wa vyama vya upinzani UKAWA (Umoja wa Katiba ya Wananchi) ikiwa haijulikani na kuonesha dalili zote 'ulishazikwa rasmi'. Uthibitisho wa 'kuzikwa' UKAWA uliotikisa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 umeoneshwa bayana baada ya hatua ya uongozi wa chama cha ACT-Wazalendo kuandika barua kuomba ushirikiano mpya na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), huku vyama vingine vikikaribishwa ikiwa maana hakuna umoja wowote kwa sasa, na haina uhakika kama vyama hivyo vitakubaliana kabla ya uchaguzi mkuu. Katibu Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu amemwambia mwandishi wa makala haya kuwa nia ya kukiondoa CCM madarakani iko pale pale, hivyo wanahit

Sudan, Ethiopia na Misri bado zavutana kuhusu mto Nile

Picha
Sudan imetahadharisha juu ya kuongezeka kwa mivutano baina yake Ethiopia na Misri kuhusu mradi wa Ethiopia wa bwawa la kuzalisha umeme kwenye mto Nile. Mivutano inazidi kuongezeka kati ya nchi hizo tatu baada ya mazungumzo ya hivi karibuni kushindwa kufikia makubaliano kuhusiana na mpango wa kulijaza maji na kuanza kazi kwa Bwawa la umeme nchini Ethiopia. Waziri wa rasilimali za maji na umwagiliaji wa Sudan, Yasser Abbas amesema nchi yake haitaki malumbano bali inaamini kuwa mazungumzo ndiyo suluhisho la pekee. Abbas amesema kutiliana saini makubaliano ni sharti linalopasa kutiliwa maanani kabla ya kulijaza maji bwawa hilo na kwamba nchi yake Sudan ina haki ya kudai hilo. Ethiopia  imetangaza mipango ya kuanza kulijaza bwawa hilo kubwa la kuzalisha umeme mwezi ujao, bila kujali iwapo makubalino juu ya mpango huo yamefikiwa au la. Misiri, ambayo inauchukulia mradi wa umeme wa Ethiopia kama tishio kubwa kwa maslahi yake mnamo siku ya Ijumaa ilitoa mwito kwa Baraza la Usalama la