Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2020

Coronavirus: Uganda yathibitisha kuwa na wagonjwa 44 wa Covid 19

Picha
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza visa vipya 11 vya ugonjwa wa Covid-19 nchini humo, wote wakiwa wanakwaya wa kwaya maarufu nchini humo 'Watoto Children's Choir. Kupitia matangazo ya televisheni, alisema kuwa wagonjwa wote wapya walikuwa karantini baada ya kurejea kutoa ughaibuni , ingawa hakueleza afya zao zikoje kwa sasa na walikuwa wametoka taifa gani. Mara nyingi kwaya hiyo huwa inatumbuiza katika nchi za ughaibuni kama Marekani, Canada na Uingereza. Mpaka sasa Uganda imethibitisha kuwa na wagonjwa wa Corona 44. Katika hatua za kukabiliana na maambukizi ya corona, tayari rais wa Uganda Yoweri Museveni ametagaza masharti zaidi ya kukabiliana na kuenea kwa virusi vya corona wiki mbili baada ya kupiga marufuku usafiri wa Umma. Katika hotuba yake kwa taifa iliyopeperushwa moja kwa moja kwenye televisheni usiku wa Jumatatu Bw. Museveni amepiga marufuku usafiri wa kutumia magari binafsi na boda boda kuanzia saa nne usiku. Mtu yeyote anayehitaji huduma za dha

maambukizi ya corona, anaweza kunyonyesha kwa kuzingatia haya

Picha
Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dk. John Jingu akizungumza na maafisa Maendeleo ya Jamii na Ustawi wa Jamii kutoka katika Kata za mkoa wa Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo kwa  wataalam hao juu ya mapambano dhidi ya Virusi vya Corona jijini Dar es Salaam jana.

Kairuki: Wanafunzi wa Tanzania wanaosoma China wasirejee nchini humo

Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki amewataka wanafunzi waliopo nje ya China kutorejea nchini humo hadi itakapotangazwa.

Coronavirus: Je agizo la kuwa umbali wa mita moja litatekelezwaje katika mitaa ya mabanda Afrika?

Picha
Kuna wagonjwa wachache wa Covid-19 barani Afrika ikilinganishwa na maeneo mengine duniani. Lakini Shirika la Afya Duniani limeonya bara hilo kujiandaa kwa hali mbaya zaidi. Serikali katika kanda tofauti za Afrika zimebuni masharti makali kama vile kufunga shule na kudhibiti matembezi. Hatahivyo katika makaazi ya mabanda ambayo yanakaliwa na mamilioni ya watu katika mazingira ya msongamano mkubwa, wengi wao wanahofia ni vigumu kukaa mbali na mwingine au kujitenga.

Coronavirus: Tofauti kati ya virusi vya corona, homa ya kawaida na mzio

Picha
Kuwasili kwa virusi vya corona kumezua mkanganyiko kuhusu tofauti ya dalili za ugonjwa huo na zile za homa ya kawaida. Katika programu ya Google, maneno kama vile 'kupiga chafya' yameongeza dalili za virusi vya corona katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita, suala ambalo linaleta shaka kutofautisha kati ya dalili za virusi hivyo vipya na dalili nyingine za magonjwa ya mapafu kama vile homa ya kawaida. ''Watu wanapaswa kujua kwamba virusi vya corona au Covid 19 ni mojawapo ya homa, hivyobasi vina dalili nyingi zinazofanana na homa ya kawaida'', alisema Paulo Ramos mtaalam wa magonjwa ya kuambukizwa katika taasisi ya Fiocruz Recife, nchini Brazil. "Lazima uwe makini iwapo unahisi tatizo la kupumua. Hatua hiyo ina maana kwamba ugonjwa huo unatatiza, ni muhimu kutafuta msaada wa kimatibabu kwa haraka," anafafanua zaidi mtaalam huyo. ''Ukiwa na shaka, shauriana na fuata mwongozo uliotolewa na nchi yako''. Tofauti kati ya coronavi

Familia ya Marealle wapelekana kortini mazishi ya mama yao

Picha
Mfanyabiashara anayemiliki vitega uchumi mbalimbali ndani na nje ya mkoa Kilimanjaro, Frank Marealle amefungua shauri mahakamani akipinga bibi wa miaka 105 kuzikwa eneo analodai ni lake.

Coronavirus: Watanzania na Wakenya washinikiza serikali zao kutangaza 'lockdown'?

Picha
Baadhi ya raia wa Tanzania na Kenya wamekua wakizitaka serikali zao zitangaze amri ya watu kukaa nyumbani ili kudhibiti maambukizi ya coronavirus. Lakini je marufuku hii ya ''lockown'' ina maana gani? Nchini nyingi duniani zimelazimika kuweka amri ya kutokuwepo na mikusanyiko baina ya watu ''lockdown'', ili kudhibiti maambukizi zaidi ya virusi vya corona yaliyowapata karibu watu 250,000 kote duniani na kusababisha vifo 9,900. Amri ya kukaa nyumbani ''lockdown'' imekua ikiwekwa na nchi mbali mbali zilizokumbwa na mlipuko wa coronavirus duniani kwa kiwango tofauti kulingana na kiwango na mlipuko na kasi ya kusambaa kwa virus katika nchi husika. ''Lockdown'' imewafanya watu kubadili mtindo wao mzima wa maisha ili kuzingatia sheria. Swali ni je Watanzania na Wakenya watarajie nini iwapo serikali zao zitatangaza ''lockdown? Kuna aina mbili za ''lockdown' Moja ikiwa ni amri kamili ya kukaa nyumb

Simulizi ya mwanamke anayekabiliana na ugonjwa uliobadili muonekano wake

Picha
Farah Khalek ni mwanamke mwen ye miaka 33 kutoka nchini Kenya, kama wanawake mwingine wa umri wake mwenye ndoto kubwa katika maisha yake. Licha ya kuwa anakabiliana na ugonjwa wa ngozi ambao umebadilisha muonekano wake wa sura kabisa. Ugonjwa huu unajulikana kama Scleroderma. Farah Khalek hakuzaliwa akiwa na sura aliyo nayo kwa sasa, alikuwa ni mtoto mwenye muonekano wa kawaida kama wengine. Farah ni msichana wa pekee kati ya ndugu watatu kwa wazazi wake, hivyo anahisi kuwa alipata malezi ya kupendwa zaidi kaatika familia. "Wazazi wangu na ndugu zangu walinidekeza tangu nikiwa mtoto mdog , kwa hiyo mimi nilikuwa katika mazingira ambayo nilihisi upendo na kukubalika" alisema Farah. Farah anaeleza kuwa akiwa na miaka 17 hali yake ilianza kubadilika wakati akiwa katika masomo yake ya sekondari. Anasema kuwa ugonjwa huo ulianza na dalili za mikononi, ambapo mikono yake ilianza kuwa migumu sana huku kucha zake zikibadilika rangi na kuwa bluu inayokaribi