Paul Makonda apigwa marufuku kuingia Marekani

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, apigwa marufuku kuingia Marekani.

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani leo Ijumaa, Januari 31 2020 marufuku hiyo pia inamhusisha mke wa Makonda Bi Mary Felix Massenge.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Makonda anashutumiwa kwa kushiriki katika ukandamizaji wa haki za binaadamu.

Ukandamizaji wa haki ambao Makonda anashutumiwa kuutenda ni pamoja na kunyima watu haki ya kuishi, haki ya uhuru wa kujiamulia mambo na usalama wa watu.

"Wizara ina taarifa za uhakika kuwa Makonda amehusika katika uvunjifu huo wa haki kupitia nafasi yake kama mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam. Katika nafasi yake hiyo, pia amelaumiwa kwa kukandamiza upinzani wa kisiasa, kukandamiza haki ya kujieleza, na kushambulia makundi yasiyo na sauti," imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Maoni

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?