Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2023

Tetesi za soka Ulaya Jumanne 30.05.2023

Picha
​ CHANZO CHA PICHA,  GETTY IMAGES Dakika 30 zilizopita Tottenham wamedhamiria kuzima majaribio ya Manchester United ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa England Harry Kane, 29, msimu huu wa joto, huku mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy akigoma kumuuza Kane kwa timu pinzani ya Ligi kuu England. (Mirror) Erik ten Hag ana imani kuwa anaweza kumshawishi kiungo wa kati wa Chelsea Mason Mount mwenye umri wa miaka 24 ajiunge na Manchester United kama sehemu ya maboresho ya kikosi chake kwenye usajili wa majira ya joto. (Telegraph) Bayern Munich wako tayari kulipa pauni milioni 95 kumnunua kiungo wa kati wa West Ham na England Declan Rice, huku timu hiyo ya Ujerumani ikiwa na nia ya kuipiku Arsenal katika kuinasa saini ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Mirror) Paris St-Germain wana nia ya kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Arsenal na Norway Martin Odegaard mwenye umri wa miaka 24. (Mail) CHANZO CHA PICHA,  GETTY IMAGES Maelezo ya picha,  Martin Odegaard Tottenham, Newcastle na Arsenal ni m

KUELEKEA FAINAL YA SHIRIKISHO JUMAPILI….IBENGE AWAKABIDHI YANGA KOMBE LA CAF…

Picha
​ Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Young Africans wanaendelea kupata Baraka za kutoboa Fainali ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu huu, kufuatia uwezo na kiwango walichokionesha kwenye michuano hiyo. Young Africans itacheza mchezo wa Mkondo wa Kwanza wa Fainali, Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya USMA Jumapili (Mei 28), kisha itakwenda Algeria kwa mchezo wa Mkondo wa Pili utakaopigwa Juni 03. Baraka za safari hii kwa Young Africans zimetolewa na Kocha Mkuu wa Mabingwa wa Sudan Al Hilal Omdurman ya nchini Sudan, Florent Ibenge ambaye anaamini Wananchi wana kila sababu za kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho na kuweka historia ya kipekee kwa Tanzania. Ibenge ambaye msimu uliopita alitwaa Ubingwa wa Michuano hiyo akiwa na RS Berkane ya Morocco, amesema anaipa nafasi kubwa Young Africans kutwaa Kombe la Shirikisho Afrika msimu huu, kutokana na aina ya wachezaji waliokuwepo hivi sasa, ambao wengi wao anawafahamu. Ibenge amesema wachezaji hao baadhi wamepita katika mikono yake

Teknolojia ya kupunguza kasi ya kuzeeka kwa binadamu

Picha
​ CHANZO CHA PICHA,  BRAIN JOHNSON 29 Aprili 2023 Katika miaka 150 iliyopita, umri wa kuishi wa wanadamu unaweza kuwa umeongezeka maradufu. Hata hivyo, watu wengi wanakatishwa tamaa sana na mabadiliko yanayotokea katika Maisha yao wanapoanza kuzeeka. Lakni Teknolojia mpya inaibuka ili kupunguza hali hii ya kuwakatisha watu tamaa. Wanasayansi wanasema kwamba teknolijia hii itawasaidia watu kuishi Maisha yenye afya tele na muda mrefu pia. Wanasayasani wanafanya kila juhudi ili kupunguza hatari na mateso wanayopitia watu kutokana na ugonjwa unaovamia mwili, kupitia matibabu mengi ya kisasa. Mara nyingi Matibabu hutolewa ili kupunguza kudhoofika kwa seli za mwili, na ili kufanikisha jambo hilo vidogo hutolewa kwa wagonjwa. CHANZO CHA PICHA,  BRAIN JOHNSON Maelezo ya picha,  Brain Johnson akiwa na mwandishi wa BBC Laura Levinington Fursa za biashara katika sekta hii kupitia matibabu haya pia zimekuwa zikiongezeka katika siku za hivi karibuni. "Nilienda California ili kujua kama masomo

Virusi vinavyosaidia kukufanya kuwa mwanadamu

Picha
​ CHANZO CHA PICHA,  GETTY IMAGES Dakika 58 zilizopita Ingawa mara nyingi virusi huhusishwa na kusababisha magonjwa na wakati mwingine, milipuko yenye maafa , virusi pia zimekuwa na jukumu muhimu katika kukua kwa binadamu. Mijusi wa Mabuya wanaoishi katika milima ya Andes ya Kolombia si kama wanyama wengine watambaao. Wakati wanyama wengi watambaao hutaga mayai yenye magamba magumu, baadhi ya spishi wanaopatikana Mubuya huzaa. Muhimu zaidi, na cha kushangaza Zaidi Wanyama hao wana kondo la nyuma linalotumika kuwasaidai Watoto kupata chakula na hewa wakiwa tumboni kwa mama yao. Kondo la nyuma huhusishwa zaidi na mamalia kama vile panya na binadamu ,hawa ndio viumbe wanaotambulika sana kuwa na kondo la nyuma. Lakini kwa sasa wanyama wengine nao wanagundulika kuwa na kondo la nyuma kama binadamu. Mwaka 2001 wataalam wa wanyama Martha Patricia Ramírez-Pinilla na Adriana Jerez wa Chuo Kikuu cha Viwanda cha Santander huko Bucaramanga, Kolombia, walifichua kwamba mijusi wa Mabuya wana kondo l