Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2022

Imam afungwa miaka Mitano kwa kuua nguruwe msikitini Rwanda.

Raheem Sterling: Kwanini mashabiki wa Man City hawamkubali sana’ Sterling? Uchambuzi wa Micah Richards

Picha
​ Nilikuwa katika uwanja wa Etihad siku ya Jumamosi wakati Raheem Sterling alipopoteza nafasi nzuri dhidi ya Watford. Ungewasikia mashabiki walionizunguka walivyokuwa wakigugunia na kupiga kelele 'hafai' au 'mtoe'. Manchester City walikuwa wanaongoza mabao 3-1 wakati huo na Sterling alikuwa akicheza vizuri sana. Hilo lilikuwa shuti lake la kwanza katika mchezo huo na, ingawa sikusema chochote kwa watu walio karibu nami, nilikuwa nikifikiria tu kwamba walihitaji kutulia na kuwa na subra. Hata hivyo hilo sio jambo jipya. Sterling anaonekana kushambuliwa zaidi kuliko mchezaji mwingine yeyote wa City. Haijalishi ni mabao mangapi anayofunga au mambo mazuri anayofanya katika mchezo - ikiwa atakosa, ni kawaida kwa Sterling sivyo? CHANZO CHA PICHA,  GETTY IMAGES Maelezo ya picha,  Sterling amefunga mabao 10 katika ligi kuu England katika michezo 26 msimu huu, goli moja nyuma ya wachezaji wanaoongoza kwa mabao msimu kwenye timu ya City, Riyad Mahrez and Kevin de Bruyne wenye mab

Kim Jong - Un aahidi kuimarisha mpango wa silaha za nyuklia

Ndege ya RwandaAir yapoteza mwelekeo baada ya kuteleza katika uwanja wa Entebbe.

Picha
​ Ndege ya abiria iliteleza na kutoka kwenye njia yake ilipokuwa ikitua katika uwanja wa ndege wa Entebbe nchini Uganda Jumatano asubuhi.  Katika taarifa, RwandAir ilisema tukio hilo "lilitokana na hali mbaya ya hewa". Abiria wote na wafanyakazi wa ndege walishuka salama bila majeraha yoyote, iliongeza. Mdhibiti wa anga alisema njia mbadala ya ndege kurukia inafanya kazi kwa ajili ya ndege ndogo na nyepesi. "Juhudi zote zinaendelea ili kuondoa ndege kwenye ukanda wa kuruka na kutua ndege ili njia kuu ya kuruka na kutua ndege irudi kutumika kikamilifu," ilisema. Gazeti la Daily Monitor nchini Uganda, limeripoti kuwa abiria 20 kati ya 60 waliokuwemo ndani ya ndege hiyo wameratibiwa kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa kwa mtoto wa Rais Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba. Inaripoti kuwa tafrija ya kuzaliwa kwa Jenerali Kainerugaba ya kutimiza miaka 48 imepangiwa kufanyika Jumapili. Jenerali Kainerugaba, ambaye pia ni kamanda wa majeshi ya nchi kavu, alichapisha ujumbe mtan