Siku ya Wanawake Duniani: Ina maana gani Afrika?


Farmer in Malawi supported by UN Women.

CHANZO CHA PICHA, UN WOMEN/BENNIE KHANYIZIRA

Kila mwaka Machi 08, Umoja wa Mataifa husheherekea haki zilizopatikana kwa bidii za wanawake- na kuangazia changamoto ambazo bado ziko mbele katika kukomesha ubaguzi wa kijinsia katika karibu nyanja zote za maisha.

"Usawa wa kijinsia wa leo, kesho na endelevu" ndio kauli mbiu ambayo Umoja wa Mataifa umeichagua mwaka huu kuadhimisha kile kinachojulikana rasmi kama Siku ya Kimataifa ya Wanawake.

Kwa nini imechagua mada hii?

Dkt Maxime Houinato, mkurugenzi wa Umoja wa Mataifa wa Wanawake katika kanda ya Afrika Mashariki na Kusini, aliiambia  kwamba "kukuza usawa wa kijinsia katika mazingira ya mzozo wa mabadiliko ya tabia nchi na upunguzaji wa hatari ya majanga ni mojawapo ya changamoto kubwa duniani kwa karne ya 21".

"Wanawake na wasichana wanapitia athari kubwa zaidi za mabadiliko ya tabia nchi," aliongeza.

Kwa kweli, utafiti wa Umoja wa Mataifa unaonesha kuwa wanawake na wasichana hufa kwa idadi kubwa katika majanga ya asili.

"Kwa mfano, asilimia 95 ya waliofariki katika mafuriko ya visiwa vya Solomon 2014 walikuwa wanawake, 55% ya waliofariki katika tetemeko la ardhi la 2015 nchini Nepal walikuwa wanawake na 59% ya waliokimbia makazi yao kufuatia Kimbunga Idai mwaka 2019 nchini Malawi walikuwa wanawake," UN Women imesema kwenye tovuti yake

People walk on the flooded street of Buzi, central Mozambique, on March 20, 2019 after the passage of the cyclone Idai

CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, 

Vimbunga vimesababisha athari kubwa kusini mwa Afrika

Zaidi ya hayo, majanga yanayohusiana na hali ya hewa yamezidisha matatizo ya kijamii na kiuchumi.

"Nchini Uganda, kwa mfano, upotevu wa mifugo, upungufu wa mazao, na ukosefu wa chakula kutokana na ukame uliokithiri, na uvamizi wa nzige ulibainika kuongeza idadi ya wanafunzi walioacha shule, kulazimisha wasichana kufanya kazi zaidi , na kuongeza matukio ya ndoa za utotoni kwa kubadilishana kwa chakula," makala katika wakala wa habari unaolenga maendeleo, Inter Press Service, inaeleza.

Siku ya Kimataifa ya Wanawake ilianzaje?

Siku ya wanawake ilikuja kutokana na vuguvugu la wafanyakazi mnamo mwaka 1908, na ikatambuliwa rasmi kama hafla ya kila mwaka na miongo kadhaa baadaye, mnamo 1975.

Mnamo mwaka 1908, zaidi ya wanawake 15,000 waliandamana katika jiji la New York kudai muda mfupi wa kufanya kazi, malipo bora na haki ya kupiga kura.

Chama cha Kisoshalisti cha Marekani kilitangaza Siku ya Kitaifa ya Wanawake ya kwanza nchini Marekani mwaka mmoja baadaye.

Mjerumani Marxist na mwanaharakati Clara Zetkin alikuwa mmoja wa waasisi wa utambuzi wa toleo la kimataifa la Siku ya Kitaifa ya Wanawake ya Marekani.

RUSSIA - CIRCA 1900: Clara Zetkin (1857-1933), German politician, in Moscow during a military parade.

CHANZO CHA PICHA, HARLINGUE

Maelezo ya picha, 

Clara Zetkin alikuwa anaongoza mapambano ya haki za wanawake

Zetkin alijumuika na wanawake 100 kutoka nchi 17 katika Kongamano la Kimataifa la Wanawake Wanaofanya Kazi katika mji mkuu wa Denmark Copenhagen mwaka 1910.

Mkutano huo kwa kauli moja ulikubaliana na pendekezo la Zetkin kwamba kuanzia mwaka unaofuata Siku ya Wanawake itaadhimishwa nchini Austria, Denmark, Ujerumani na Uswizi.

Wazo la Zetkin la Siku ya Kimataifa ya Wanawake halikuwa na tarehe maalum.

Ilirasimishwa baada ya mgomo wa baada ya vita, wanawake nchini Urusi mwaka 1917. Wanawake walidai "mkate na amani" - na siku nne za mgomo wa wanawake, Tsar alilazimika kujiuzulu na serikali ya muda hiyo iliwapa wanawake haki ya kupiga kura.

Tarehe ambayo mgomo wa wanawake ulianza kwa kalenda ya Juliana, ambayo wakati huo ilikuwa ikitumika nchini Urusi, ilikuwa Jumapili Februari, 23.

Siku hii katika kalenda ya Gregori ilikuwa Machi 8. Huu ndio wakati ambapo sasa inaadhimishwa kama siku ya mapumziko nchini Urusi na nchi zingine takribani dazeni mbili.

Follow us on Facebook

Follow us on Instagram

Follow us on Twitter

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?