Aliyelipwa Fidia ya mamilioni ya fedha kimakosa akataa kurejesha fedha


Mfuko wa Marekani ambao ulijitwikwa jukumu la kuwalipa fidia waathiriwa wa shambulizi la kigaidi la 1998 jijini Nairobi umemshtaki mwanamke ambaye alipokea kimakosa mamilioni ya pesa ambayo inadaiwa alikataa kurejesha. 

Mfuko huo umeomba Mahakama Kuu itoe amri ya kurejeshewa fedha alizopokea Mary Ngunyi Muiruri, kiasi cha dola za Marekani 65,683.50 (Sh milioni 7.4 za Kenya) mnamo Novemba mwaka 2020, Gazeti la Nation la Kenya limeripoti.

Hazina hiyo ilinuia kumlipa Mary Njoki Muiruri pesa hizo, lakini mkanganyiko wa majina ya kati ulisababisha mtu ambaye hakukusudiwa akipokea pesa hizo. 

Bi Ngunyi hajajibu madai hayo. 

Mfuko huo wa fidia ulikuwa umeomba benki ya eneo hilo kurejesha pesa hizo. Benki ya Nairobi, hata hivyo, ilisema Bi Ngunyi alikataa kuridhia ombi hilo, hivyo kuwasilisha shauri la kisheria. 

Benki hiyo inaongeza kuwa mawasiliano kati ya Mfuko wa Udhibiti wa Mabomu wa Ubalozi wa Marekani wa 1998 na Ngunyi yalionesha kuwa kulikuwa na mzozo kuhusu ni nani mpokeaji halisi wa mamilioni hayo.

Bi. Ngunyi alisisitiza kuwa fedha hizo ni zake

Benki imeongeza kuwa Bi. Ngunyi ameshatumia kiasi kikubwa cha fedha.

Kufikia mwaka 1998, Mfuko wa Ubalozi wa Marekani ulipopata maagizo ya mahakama ya kufungia akaunti ya Ngunyi mnamo Februari 2021, Bi Ngunyi alikuwa ametoa pesa nyingi na alikuwa na $5,553 pekee (Sh633,319) kama salio la akaunti .

Benki hiyo inahoji kwenye karatasi za mahakama kwamba haikuwa mhusika katika kesi za mahakama nchini Marekani kuhusu fidia ya waathiriwa wa mashambulizi ya kigaidi na kwa hivyo haikuweza kuthibitisha kwa mamlaka ni nani alikuwa mpokeaji halisi wa pesa hizo. 

Wakenya kadhaa waliwasilisha kesi katika mahakama za Marekani dhidi ya Jamhuri ya Sudan na Iran kati ya 2008 na 2012 wakitaka walipwe fidia kwa majeraha na kupoteza jamaa zao katika shambulio la bomu la Agosti, 1998 katika Ubalozi wa Marekani jijini Nairobi.

Mashambulio ya mabomu ya 1998: Kenya imelipia gharama ya juu ya maisha katika vita dhidi ya Ugaidi?

Mashambulio ya mabomu ya 1998 : Washukiwa watatu wakuu waliohusika na mashambulizi dhidi ya Kenya na Tanzania


Follow us on Facebook

Follow us on Instagram

Follow us on Twitter

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?