​Ndege 4 za Urusi zaangushwa Ukraine huku baadhi ya wanajeshi wakikataa kutekeleza amri


Post update

Baadhi ya wanajeshi wa Urusi wakataa amri , ndege  nne zaangushwa - vimesema vikosi vya Wanajeshi wa Ukraine

Wakati Ukraine ikielekea katika siku ya ishirini ya uvamizi wa Urusi katika ardhi yake, Maafisa wakuu wa jeshi la Ukraine wametoa taarifa yao kila alfajiri

Vikosi vya Urusi vinasalia kushambulia maeneo kadhaa nchini Ukraine , na vimeshindwa kupiga hatua zaidi

Hata hivyo wanajeshi wa Urusi wameendelea kufanya mashambulizi ya makombora na mabomu kwenye miundombinu muhimu 

Wanajeshi wa Urusi wamekuwa wakitumia vituo vya afya katika maeneo yanayokaliwa kuwatibu waliojeruhiwa

Helikopta nne za Urusi ziliangushwa na vikosi vya Ukraine

Vikosi vya Ukraine vimefanikiwa kuzuia majaribio ya Urusi ya kuuteka mji wa bandari wa kusini wa Mariupol uliokuwa na ushindani mkubwa na hakujawa na dalili zozote za kutua kwa jeshi la Urusi katika eneo la Bahari Nyeusi.

Baadhi ya wanajeshi wa Urusi wanakataa kutekeleza amri.


Newsday Swahili


Follow us on Facebook

Follow us on Instagram

Follow us on Twitter

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?