Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2020

Mbwa aliyewaokoa wanajeshi wa Uingereza waliokuwa wakishambuliwa na al-Qaeda Afghanistan

Picha
Mbwa wa jeshi aliyekimbia na bila kuogopa risasi zilizokuwa zikifyatuliwa na adui ili kuokoa maisha ya wanajeshi wa Uingereza waliokuwa wakipigana na al-Qaeda nchini Afghanistan anatarajiwa kutuzwa tuzo ya juu zaidi ya wanyama. Wakati wa uvamizi , mbwa huyo aina ya Malinois kutoka Ubelgiji kwa Jina Kuno alimkabili mpiganaji mmoja aliyekuwa na bunduki na alipigwa risasi katika miguu yake yote miwili. Baada ya kupoteza mguu wake mmoja kutokana na shambulio hilo la risasi , alikuwa mbwa wa kwanza wa Uingereza kuwekwa miguu bandia. Mbwa huyo mwenye umri wa miaka minne atapokea medali yake ya Dickin kutoka kwa shirika la hisani linaloshughulikia wanyama wagonjwa PDSA. Akiwa mwanajeshi mstaafu na kupelekwa nyumbani Uingereza, Kuno ambaye alifunzwa kufichua vilipuzi , silaha na kuwakabili maadui atatuzwa medali hiyo katika sherehe mwezi Novemba. Kuno na wamiliki wake walikuwa wamepelekwa nchini Afghanistan kusaidia vikosi maalum wakati wa shambulio la usiku lililokuw

Hong Kong: China yawakamata watu 10 baada ya kulizuia boti lililokuwa likitoroka Hong Kong

Picha
Mamlaka nchini China imewakamata takriban watu 10 baada ya kuzuia boti inayoaminika ilikuwa inaelekea Taiwan kutoka Hong Kong kulingana na ripoti. Walinzi wa pwani ya China wamesema kuwa ukamataji huo ulifanyika siku ya Jumapili alfajiri katika mkoa wa kusini wa Guangdong, karibu na Hong Kong. Vyombo vya habari mjini Hong Kong vilisema kwamba wale waliokuwa wakiabiri chombo hicho walikuwa wakijaribu kuingia Taiwan ili kuchukua hifadhi ya kisiasa. Ripoti hiyo imesema kwamba mwanaharakati wa Hong Kong Andy Li alikuwa miongoni mwa wale waliokamatwa . Bwana Li , ambaye alikamatwa mapema mwezi huu kwa madai ya kujihusisha na viongozi wa mataifa ya kigeni na utapeli wa fedha , alikamatwa kwa tuhuma za kuvuka mpaka bila kufuata sheria kulingana na gazeti la kusini mwa China la Morning Post likinukuu vyanzo tofauti. Haijulikani waliokamatwa watafunguliwa mashtaka gani. Majaribio ya watu Hong Kong kutoroka eneo hilo kwa kutumia boti sio ya kawaida. Hong Kong imer

Uchaguzi Tanzania 2020: Pingamizi la Tundu Lissu dhidi ya rais Magufuli na professa Lipumba lashindwa kufurukuta

Picha
Mgombea wa urais nchini Tanzania kupitia chama cha upinzani cha CHADEMA Tundu Lissu ameshindwa kuwazuia wapinzani wake katika uchaguzi mkuu wa urais wa mwaka huu kuondolewa katika orodha ya watakaogombea wadhfa huo. Tundu Lissu alikuwa amewasilisha pingamizi dhidi ya rais John Pombe Magufuli na profesa Ibrahim Harun Lipumba kuondolewa katika orodha ya kuwania urais kwa sababu za kutokamilisha matakwa ya kisheria katika kujaza fomu za uteuzi wa kiti hicho. Katika pingamizi hilo alilolowasilisha kwa tume ya uchaguzi nchini Tanzania NEC , bwana Lissu pia alidai kwamba rais John Pombe Magufuli hakuambatanisha picha katika fomu zake za uteuzi. Lakini ikitoa uamuzi wake, tume ya uchaguzi nchini humo NEC imesema kwamba baada ya kupitia pingamizi zote mbili na utetezi uliotolewa, imejiridhisha kuwa rais John Pombe Magufuli ambaye ni mgombea wa kiti cha Urais kupitia CCM alirejesha fomu zake ambazo ziliambatanishwa na picha kwa mujibu wa sheria za tume ya taifa ya uchaguzi.

Harry Maguire: Polisi wanadai kwamba nahodha wa Manchester United alijaribu kuwahonga

Picha
Nahodha wa Manchester United Harry Maguire aliuliza polisi waliomkamata katika visiwa vya Ugiriki vya Mykonos "Je unajua mimi ni nani?" na kutaka kuwapa pesa kulingana na kesi inayoendelea kusikilizwa. Mlinzi huyo wa Uingereza, 27, alikuwa miongoni mwa watu watatu waliokamatwa Alhamisi kwa madai ya mabishano na polisi. Wengine waliokuwepo ni kaka yake Maguire, 28 na rafiki yake Christopher Sharman, 29. Wote watatu wanashutumiwa kwa kuvamia polisi na kuzua vurugu. Harry na Joe Maguire pia wanashutumia kwa madai ya kujaribu kutoa rushwa, huku Harry Maguire na Christopher Sharman wakishtumiwa kwa kutoa cheche za matusi. Hata hivyo, watatu hao wamekanusha mashitaka dhidi yao. Harry Maguire, ambaye Jumanne alitajwa katika kikosi cha hivi karibuni cha Gareth Southgate timu ya Uingereza, haudhurii kesi hiyo huko Syros, lakini baba yake, Alan, anahudhuria. Anawakilishwa na Alexis Anagnostakis, wakili maarufu anayetetea haki za binadamu huko Ugiriki amb

Bayern Munich wailaza PSG na kushinda kombe la ligi ya mabingwa Ulaya

Picha
Bayern Munich iliizidia Paris St-Germain katika fainali kali ya kombe la ligi ya mabingwa Ulaya ili kutawazwa mabingwa kwa mara ya sita katika mechi iliochezwa Lisbon. Kingsley Coman ambaye alianza soka yake katika klabu ya PSG alifunga goli la pekee kunako dakika ya 59 kupitia kichwa kufuatia krosi iliopigwa na Joshua Kimmich na kuwawacha mabingwa hao wa Ufaransa wakisalia kutafuta ushindi wa kombe hilo. Ulikuwa usiku wa furaha kwa mkufunzi wa Bayern Hansi Flick , ambaye aliisaidia timu hiyo kupata kombe lake la pili msimu huu baada ya lile la ligi, alipochukua ukufunzi wa timu hiyo kufuatia kufutwa kwa Niko Kovac mwezi Novemba. Ulikuwa usiku mrefu kwa nyota wawili wa mabingwa hao wa Ufaransa Neymar na Mbappe ambao walishindwa kuonesha umahiri wao na kujipata wakifadhaishwa na kipa wa Bayern Manuel Neuer aliepewa tuzo la mchezaji bora wa mechi wakati walipopoteza fursa za wazi. Uchungu wa Mbappe uliongezeka katika kipindi cha pili wakati alipoonekana kuchezewa vi

Choo unachoweza kuona kinachoendelea ndani Japani

Picha
Moja ya maeneo maarufu nchini Japani umeongeza kivutio kisicho cha kawaida ambacho ni vyoo vya umma angavu. Mbunifu wa vyoo hivyo ambaye pia ni mhandisi Shigeru Ban, amesema vyoo hivyo ambavyo unaweza kuona mwenzio anachofanya upande wa pili au akiwa ndani vimewekwa mji wa Shibuya wenye watu wengi. Ingawa hilo linaonekana kama kuvuka mipaka ya utamaduni hivi, lengo ni kubadilisha mitazamo ya watu kuhusu vyoo vya umma. Mbunifu Shigeru ambaye pia ni mshindi wa tuzo ya Pritzker amesema katika taarifa "Vyoo angavu vimewekwa katika bustani mbili za Shibuya, ya - Yoyogi Fukamachi na Haru-no-Ogawa. "Kuna mawili yanayotutia wasiwasi, wakati unaingia choo cha umma, hasa vilivyo maeneo ya bustani," amesema kwenye tovuti rasmi ya mradi huo, "Kwanza ni usafi, na pili ni ikiwa kuna mtu ndani au la." Ubunifu wa Shigeru Ban unatoa ufumbuzi wa matatizo hayo mawili baada ya utengenezaji wake wa vyoo ambayo ukuta wake ni kioo - kwanza mtu anaweza kuona k

Uamuzi kuhusu kesi ya mauaji ya Waziri Mkuu wa zamani wa Lebanon Rafik Hariri kutolewa

Picha
Uamuzi uliokuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu utatolewa hii leo dhidi ya wanaume wanne wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Lebanon Rafik Hariri na watu wengine 21 katika shambulio la bomu mwaka 2005. Watuhumiwa wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kishia wa kundi la Hezbollah nchini Lebanon - walihukumiwa na mahakama maalum huko Uholanzi licha ya kutokuwepo mahakamani. Hasira iliyojitokeza baada ya shambulio la Beirut ililazimu Syria iliyokuwa inaunga mkono kundi la Hezbollah kuondoa vikosi vyake Lebanon miaka 29 iliyopita. Hezbollah na serikali ya Syria zilikanusha kuhusika na shambulio hilo. Zaidi ya watu 220 walijeruhiwa pale gari lililokuwa limejazwa vilipuzi lilipolipuka wakati msafara wa Bwana Hariri ulipokuwa unapita mbele ya ufuo wa Beirut. Mauaji hayo yalibadilisha Lebanon na kuanza kuchipuka kwa makundi ya upinzani ambayo miaka kadhaa baadae yalibadilisha siasa za nchi hiyo. Kijana wa Bwana Hariri, Saad, aliongoza chama kilichokuwa

Israel na UAE kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia

Picha
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anatumai mpango wa Israel na Umoja wa Falme za Kiarabu unaweza kusaidia kufikiwa suluhisho la mataifa mawili na Wapalestina kwa ajili ya amani katika Mashariki ya Kati.  Israel na UAE zimekubaliana kurejesha mahusiano katika muafaka wa kihistoria, ambao ni wa tatu pekee wa aina hiyo ambao taifa hilo la Kiyahudi limewahi kusaini na taifa la Kiarabu, ambapo imeahidi kusitisha unyakuzi wa ardhi za Wapalestina. Guterres amesema unyakuzi unaweza "ukafunga kabisa mlango" wa mazungumzo kati ya Israel na viongiozi wa Palestina na "kuharibu matumaini" ya kupatikana taifa la Kipalestina chini ya suluhisho la mataifa mawili. Waziri Mkuu wa Israel Bwenjamin Netanyahu amesema ni "siku ya kihistoria" na muafaka huo utafungua enzi mpya kwa ulimwengu wa Kiarabu na Israel.  Makubaliano haya ni pamoja na mahusiano kamili ya kidiplomasia, kufunguliwa kwa balozi na kubadilishana mabalozi, uwekezaji mkubwa ambao uta

Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 13.08.2020: Thiago, Lacazette, Sarr, Grealish, Diawara, Pogba

Picha
Manchester City wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka kiungo wa kati wa Bayern Munich Muhispania Thiago Alcantara na wanaaminiwa kutoa ofa ya malipo zaidi ya Liverpool kwa ajili ya kumpata kijana huyo mwenye umri wa miaka 29. (SportBild - via Star) Manchester United wamesitisha kwa muda biashara ya kuwahamisha wachezaji huku wakijaribu kusaini mkataba na winga wa Borussia Dortmund na England Jadon Sancho, 20. Watford wako tayari kudai rekodi ya garama ya zadi ya pauni milioni 40 kwa winga Msenegal Ismaila Sarr, 22, huku Liverpool na klabu nyingine za Ulaya zikitangaza nia yao ya kumchukua.  Sarr amewaambia waandishi wa habari nchini Senegal kwamba "kile mtu angependa " kuchezea Liverpool. (Sans Limites - via Goal) Roma wanaweza kumbadilisha kiungo wa kati Mguinea Amadou Diawara mwenye umri wa miaka 23 na kiungo wa kati Arsenal Lucas Torreira ambaye ni raia wa Uruguay mwenye umri wa miaka , 24. (Gazzetta dello Sport - via Mail) Valencia wamezi