Bill Gates: Bilionea wa Microsoft atalakiana na mkewe Melinda Gates

Bill na Melinda Gates wametangaza talaka yao baada ya miaka 27 ya ndoa, wakisema "hatuamini tena tunaweza kuwa pamoja kama wanandoa".

"Baada ya kufikiria sana na kufanya kazi nyingi juu ya uhusiano wetu, tumefanya uamuzi wa kumaliza ndoa yetu," wawili hao walisema katika ujumbe wa twitter .

Walikutana kwa mara ya kwanza miaka ya 1980 wakati Melinda alipojiunga na kampuni ya Bill ya Microsoft.

Wanandoa hao mabilionea wana watoto watatu na kwa pamoja wanaendesha Wakfu wa Bill & Melinda Gates.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?