Bill Gates: Bilionea wa Microsoft atalakiana na mkewe Melinda Gates
Pata kiungo
Facebook
X
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
Bill na Melinda Gates wametangaza talaka yao baada ya miaka 27 ya ndoa, wakisema "hatuamini tena tunaweza kuwa pamoja kama wanandoa".
"Baada ya kufikiria sana na kufanya kazi nyingi juu ya uhusiano wetu, tumefanya uamuzi wa kumaliza ndoa yetu," wawili hao walisema katika ujumbe wa twitter .
Walikutana kwa mara ya kwanza miaka ya 1980 wakati Melinda alipojiunga na kampuni ya Bill ya Microsoft.
Wanandoa hao mabilionea wana watoto watatu na kwa pamoja wanaendesha Wakfu wa Bill & Melinda Gates.
Shirika hilo limetumia mabilioni kufadhili kampeni mbalimbali ikiwemo magonjwa ya kuambukizana na kuhamasisha chanjo kwa watoto.
Wawili hao - pamoja na mwekezaji Warren Buffett - wanahusika na mpango wa Ahadi ya Kutoa, ambao unawataka mabilionea kujitolea kutoa utajiri wao mwingi kwa malengo ya kuwafaidi watu .
Bill Gates ndiye mtu wa nne tajiri zaidi ulimwenguni, kulingana na Forbes, na ana mali ya thamani ya $ 124bn (£ 89bn).
Alipata pesa kupitia kampuni aliyoianzisha miaka ya 1970, Microsoft, kampuni kubwa ya programu ulimwenguni.
Wawili hao walichapisha taarifa hiyo wakitangaza talaka yao kwenye Twitter.
"Katika kipindi cha miaka 27 iliyopita, tumewalea watoto watatu wa ajabu na kujenga wakfu ambao unafanya kazi ulimwenguni kote kuwezesha watu wote kuishi maisha yenye afya, yenye tija," ujumbe huo ulisema
"Tunaendelea kuwa na imani ya pamoja katika lengo hilo na tutaendelea kufanya kazi pamoja kwenye wakfu wetu , lakini hatuamini tena tunaweza kukua pamoja kama wanandoa katika sehemu inayofuata ya maisha yetu.
"Tunaomba nafasi na faragha kwa familia yetu tunapoanza maisha haya mapya."
Walikutanaje ?
Melinda alijiunga na Microsoft kama msimamizi wa bidhaa mnamo 1987, na hao wawili walikaa pamoja kwenye dhifa ya chakula cha jioni cha biashara mwaka huo huko New York.
Walianza kuchumbiana, lakini kama Bill alivyokiambia kipindi kimoja cha Netflix: "Tulijaliana sana na kulikuwa na uwezekano wa mawili kutokea : ama, tungeachana au tungeoana."
Melinda alisema alimpata Bill - akiwa mtu wa kawaida inaonekana hata katika maswala ya moyo - akiandika orodha kwenye ubao mweupe na "faida na hasara za kuoa".
Walioana mnamo 1994 katika kisiwa cha Lanai cha Hawaii,wakikiripotiwa kukodi helikopta zote za eneo hilo kuwazuia wageni wasiohitajika kupaa na kuja harusini mwao bila kualikwa.
Bill Gates alijiuzulu kutoka bodi ya Microsoft mwaka jana ili kuzingatia shughuli zake za uhisani.
Serikali ya Uganda imeaandaa maonyesho ya picha kuhusu raisi wa zamani Field Marshal Idi Amin Dada ambaye anadhaniwa kuwa ni mmoja wa madikteta hatari duniani. Hata ivyo maonyesho haya yanalenga kuonesha taswira tofauti na kuangazia mazuri aliyoyafanya. Je ni nini mtazamo wako kuusu hatua hii iliyochukuliwa na Serikali ya Uganda? Toa maoni yako Kuhusu hilii
Wapenzi kutoka Ufaransa wamekamatwa na kilo 40 za mchanga wa Sardinian katika gari lao na wanaweza kukabiliana na kifungo cha miaka 6 jela. Walisema kuwa walitaka kuondoka na mchanga nyumbani kwao na hawakujua kama wamefanya makosa. Ni kosa la jinai kwa mtu kuhamisha mchanga kutoka katika kisiwa cha Sardinia, kwa sababu mchanga unatambulika kama mali ya umma. Kwa miaka mingi, wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakilalamikia wizi wa mali asili ikiwa ni pamoja na mchanga. Wapenzi hao wanaweza kuhukumiwa kati ya mwaka mmoja jela mpaka miaka sita kwa kosa la wizi wa mali ya umma. Chini ya sheria ya mwaka 2017, biashara ya mchanga na mapambo ya bahari ni kunyume cha sheria, na faini ya yuro 3000. Polisi walikuta mchanga umewekwa kwenye chupa 14 ambazo zilitoka katika ufukwe wa Chia , kusini mwa Sardinia katika buti ya gari la wapenzi hao. Mwaka 1994, ufukwe uliopo kisiwa cha Budeli kaskazini mashariki mwa Sardinia uliwekewa zuio kwa ajili ya siku siku za mbeleni. Mamlaka ina hofu ya tani kadhaa z...
WANACHAMA wa Yanga wamemuangukia mwenyekiti wao aliyejiuzulu Yusuf Manji baada ya kukataa ombi la kuachia ngazi la kiongozi huyo. Wanachama wa klabu hiyo kutoka matawi 65 ya mkoa wa Dar es Salaam walikutana jana na kumtaka makamu mwenyekiti wao, Clement Sanga kuhitisha haraka kmkutano wa dharura. Kikao hicho kiliongozwa na Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Mkwasa, ambapo kwa pamoja waliazimia kukataa ombi la kujiuzulu kwa Manji. “Wanachama hawataki Manji akae pembeni, wanataka mkutano wa dharura uitishwe siku 14 toka leo kwa mujibu wa katiba, kamati ya utendaji inakaa leo ( Jana) mchana itapitia maombi ya wanachama na kutoa maamuzi.” alisema Mkwasa. Naye Makamu Mwenyekiti wa matawi Bakili Makele alisema kuwa baada ya kutafakari barua ya Manji, ambayo inaeleza moja ya sababu ya kujiuzulu ni kutokana na afya yake, lakini wao wanasema bado wanamuhitaji. Naye Mwenyekiti wa Keko Ukombozi Joseph Kalindwa akizungumzia hilo alisema “ Manji alitukuta kipindi kigumu mno tukiwa tu...
Maoni
Chapisha Maoni