Bill Gates: Bilionea wa Microsoft atalakiana na mkewe Melinda Gates
Pata kiungo
Facebook
Twitter
Pinterest
Barua pepe
Programu Nyingine
Bill na Melinda Gates wametangaza talaka yao baada ya miaka 27 ya ndoa, wakisema "hatuamini tena tunaweza kuwa pamoja kama wanandoa".
"Baada ya kufikiria sana na kufanya kazi nyingi juu ya uhusiano wetu, tumefanya uamuzi wa kumaliza ndoa yetu," wawili hao walisema katika ujumbe wa twitter .
Walikutana kwa mara ya kwanza miaka ya 1980 wakati Melinda alipojiunga na kampuni ya Bill ya Microsoft.
Wanandoa hao mabilionea wana watoto watatu na kwa pamoja wanaendesha Wakfu wa Bill & Melinda Gates.
Shirika hilo limetumia mabilioni kufadhili kampeni mbalimbali ikiwemo magonjwa ya kuambukizana na kuhamasisha chanjo kwa watoto.
Wawili hao - pamoja na mwekezaji Warren Buffett - wanahusika na mpango wa Ahadi ya Kutoa, ambao unawataka mabilionea kujitolea kutoa utajiri wao mwingi kwa malengo ya kuwafaidi watu .
Bill Gates ndiye mtu wa nne tajiri zaidi ulimwenguni, kulingana na Forbes, na ana mali ya thamani ya $ 124bn (£ 89bn).
Alipata pesa kupitia kampuni aliyoianzisha miaka ya 1970, Microsoft, kampuni kubwa ya programu ulimwenguni.
Wawili hao walichapisha taarifa hiyo wakitangaza talaka yao kwenye Twitter.
"Katika kipindi cha miaka 27 iliyopita, tumewalea watoto watatu wa ajabu na kujenga wakfu ambao unafanya kazi ulimwenguni kote kuwezesha watu wote kuishi maisha yenye afya, yenye tija," ujumbe huo ulisema
"Tunaendelea kuwa na imani ya pamoja katika lengo hilo na tutaendelea kufanya kazi pamoja kwenye wakfu wetu , lakini hatuamini tena tunaweza kukua pamoja kama wanandoa katika sehemu inayofuata ya maisha yetu.
"Tunaomba nafasi na faragha kwa familia yetu tunapoanza maisha haya mapya."
Walikutanaje ?
Melinda alijiunga na Microsoft kama msimamizi wa bidhaa mnamo 1987, na hao wawili walikaa pamoja kwenye dhifa ya chakula cha jioni cha biashara mwaka huo huko New York.
Walianza kuchumbiana, lakini kama Bill alivyokiambia kipindi kimoja cha Netflix: "Tulijaliana sana na kulikuwa na uwezekano wa mawili kutokea : ama, tungeachana au tungeoana."
Melinda alisema alimpata Bill - akiwa mtu wa kawaida inaonekana hata katika maswala ya moyo - akiandika orodha kwenye ubao mweupe na "faida na hasara za kuoa".
Walioana mnamo 1994 katika kisiwa cha Lanai cha Hawaii,wakikiripotiwa kukodi helikopta zote za eneo hilo kuwazuia wageni wasiohitajika kupaa na kuja harusini mwao bila kualikwa.
Bill Gates alijiuzulu kutoka bodi ya Microsoft mwaka jana ili kuzingatia shughuli zake za uhisani.
Viongozi wa nchi za Umoja wa Ulaya hatimaye Jumanne asubuhi walifikia makubaliano ya yuro bilioni 750 za kuufufua uchumi wao. Pesa hizi ni za kukabiliana na athari zilizotokana na janga la virusi vya corona. Viongozi hao walioonekana wenye uchovu wamekubaliana bajeti ya yuro trilioni 1.82 pia pamoja na hizo pesa za kufufua uchumi baada ya janga la virusi vya corona. Hatua hii imefikiwa kufuatia majadiliano ya siku nne ya usiku na mchana yaliyojawa na makabiliano na ubishi mkali kuhusiana na pesa na nguvu katika mojawapa ya mkutano wao mrefu zaidi wa kilele kuwahi kushuhudiwa. Hizo bilioni 750 zitatolewa kama mkopo kwa nchi zilizoathirika vibaya zaidi na janga hilo huku makubaliano yakiafikiwa pia kuhusiana na bajeti hiyo ya miaka saba ya zaidi ya trilioni moja. Mkutano ulitarajiwa kuisha Jumamosi Charles Michel ni mwenyekiti wa mkutano huo wa kilele. "Tumeonyesha imani kwa mustakabali wetu na makubaliano haya yanaonyesha kuwa Ulaya ni nguvu ya vitendo. Tumejadiliana
Serikali ya Uganda imeaandaa maonyesho ya picha kuhusu raisi wa zamani Field Marshal Idi Amin Dada ambaye anadhaniwa kuwa ni mmoja wa madikteta hatari duniani. Hata ivyo maonyesho haya yanalenga kuonesha taswira tofauti na kuangazia mazuri aliyoyafanya. Je ni nini mtazamo wako kuusu hatua hii iliyochukuliwa na Serikali ya Uganda? Toa maoni yako Kuhusu hilii
Uganda imesaini makubaliano na Urusi kuisaidia kujenga uwezo wake wa kutumia teknolojia ya nyuklia kwa matumizi ya kutengeneza nishati, dawa na matumizi mengine ya amani. Hatua hii inafuata kusainiwa kwa makubaliano mnamo mei mwaka jana baina ya serikali ya rais Yoweri Museveni na shirika la kitaifa la nyuklia China CNNC, kulisaidia taifa hilo la Afrika mashariki kuendeleza matumizi ya nishati ya nyuklia kwa madhumuni ya amani. Katika ujumbe rasmi wa wizara ya nishati Uganda, makubalinao hayo na Urusi yalisainiwa hapo jana Jumatano huko Vienna kati ya waziri Irene Muloni na naibu mkurugenzi mkuu wa shirika la kitaifa la nishati ya atomiki ROSATOM, Nikolai Spasskiy. Urusi itaisaidia Uganda kujenga miundo mbinu ya nyuklia kwa matumizi katika viwanda sekta ya afya na pia ukulima. "Spasskiy ameeleza uwajibikaji na utayari wa ROSATOM kuisaidia Uganda kuidhinisha matumizi ya amani ya nishati ya nyuklia hususan katika ujenzi wa kinu cha nishati ya nyuklia," taarifa imeeleza. Kwa muj
Maoni
Chapisha Maoni