Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2024

Ukigundua una dalili hizi 10 nenda ukapimwe maradhi ya Kisukari

Picha
CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES Afroza Akhtar hakuelewa kwamba alikuwa na kisukari kwa muda mrefu. Hakujua kwamba sababu za kujihisi kiu, uchovu na mwili kuishiwa nguvu huenda ni baadhi ya dalili za maradhi hayo. ''Nilikwenda kwa daktari na kumueleza baada ya kujisikia vibaya kwa muda mrefu.Alinifanyia vipimo vya kisukari na magonjwa mengine. Ni pale ndipo niligundulika kuwa nina ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu '' Tangu hapo alianza matibabu katika hospitali maalum ya ugonjwa wa kisukari. Si yeye pekee, kwa mujibu wa wataalamu wa kisukari, zaidi ya asilimia 50 ya watu wenye maradhi ya kisukari hawafahamu kuwa wana ugonjwa huo MATANGAZO Ugonjwa huo uligunduliwa wakati wa alipokuwa akipimwa maradhi mengine. Unaweza pia kusoma Ni rahisi kuepuka ugonjwa wa kisukari? 14 Novemba 2021 Ugonjwa wa kisukari unaweza kutibika na kuzuiwa kirahisi - Daktari anaeleza 7 Machi 2024 Wataalamu wanasema kutokana na hali hiyo ndiyo maana ni muhimu sana kutoa hamasa kwa jamii kuhusu ugonjw...

Israel ina mpango wa kutaka kuitwaa Gaza kaskazini

Picha
CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES Magazeti kadhaa ya Kiarabu, Uingereza na Marekani yaliangazia matokeo ya kurejea kwa Donald Trump katika kiti cha urais nchini Marekani kwa eneo la Mashariki ya Kati. Katika muktadha huu, Makala haya yanaangazia kuhusu hofu ya Israel kunyakua ardhi ya Palestina, na kwa upande mwingine kuhusu safu ya viongozi wapya wa Trump. Pia utafahamu kuhusu mwelekeo wa uhusiano kati ya Trump na Iran katika siku za usoni. Tunaanza na gazeti la Uingereza The Guardian na makala iliyoandikwa na Ben Reeve, ambapo aliangazia matamshi, harakati za kijeshi, na hatua za kisiasa ambazo zinaonyesha kuwa Israeli inapambana kunyakua Ukanda wa kaskazini mwa Gaza. MATANGAZO Mwandishi wa gazeti la Uingereza alirejelea matamshi ya Itzik Cohen, afisa mkuu wa jeshi la Israel, aliyoyaona kama "ukiri" kwamba Israel inatekeleza "maangamizi kwa jamii hiyo ya kaskazini mwa Gaza, na kuuhadaa ulimwengu kuhusu malengo yake halisi katika eneo ililodhibiti. Makala hiyo ilieleza kwa...

Kutoka Vietnam hadi Iran: Nani na kwa namna gani Korea Kaskazini ilisaidia Kupambana

Picha
CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES Bunge la Urusi lililofahamika kama State Duma limeidhinisha mkataba wa "ushirikiano wa kimkakati wa kina" na Korea Kaskazini. Hati hii ina kifungu cha kutoa usaidizi wa kijeshi wa pande zote katika shambulio la moja ya nchi, ambapo Wall Street Journal iliandika kwamba mkataba huo pia una kifungu cha siri juu ya kutumwa wanajeshi wa Korea Kaskazini Kwenda vitani na Ukraine. Siku ya Jumatano, Oktoba 23, Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lloyd Austin alisema Pentagon ina ushahidi wa wanajeshi wa Korea Kaskazini kutumwa Urusi. Taarifa za kijasusi za Korea Kusini imeripoti kwamba DPRK imeipatia Moscow askari elfu tatu, na kufanya jumla ya askari 10,000. Hapo awali, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alizungumza juu ya brigedi mbili za askari 6,000 kila moja. Ikiwa data hizi zitathibitishwa, ya kwamba DPRK kweli ilituma maelfu ya askari wake kusaidia jeshi la Urusi, basi kampeni hii itakuwa kesi ya kwanza ya ushiriki mkubwa wa wanajeshi wa Korea Kaskazini ...