Tunachokifahamu kufikia sasa kuhusu shambulio la Alshabab dhidi ya wanajeshi wa Burundi.

Kundi la Kigaidi la al-Shabab limesema kuwa wao ndio wahusika kwenye mauaji makubwa katika shambulizi la katika kambi ya walinda amani wa Umoja wa Afrika nchini Somalia, hata hivyo pande zote mbili zimekuwa zikitoa taarifa zinazokidhana juu ya idadi za vifo.

Kundi hilo ambalo ni washirika wa al-Qaeda wamesema wamewaua wanajeshi wapatao 170 wa AU, wengi wao wakiwa wametokea nchini Burundi pia kuwaweka mateka wengine bila kutaja idadi yao. 

Hata hivyo jeshi la Burundi limesema kuwa wanajeshi wake 10 ndio waliopoteza maisha na wengine watano waliopotea.

Bado mpaka sasa hakuna taarifa za uhakika kuhusu shambulizi hili.

Kitu gani kilitokea kwenye shambulio hilo?

Mashambulizi hayo katika eneo la Shabelle ya Kati nchini humo yalishuhudia wapiganaji waliokuwa na silaha nzito wakivamia kambi ya al-Baraf kilomita 160 kaskazini-mashariki mwa mji mkuu, Mogadishu, ambako vikosi vya Burundi, vinavyohudumu chini ya AU, viliweka kambi.

Wananchi wa eneo hilo wanadai kusikia milio ya silaha nzito asubuhi.

"Shambulizi limetokea jana asubuhi,," Mjumbe wa AU, ambaye hakutaka kutambulika akiiambia BBC. "Magari mawili yaliyokuwa na mabomu na silaha yaliingia kwenye eneo na hapo ndio milio ya risasi ikaanza kusikika. Sifahamu idadi kamili ya waliopoteza maisha kwenye shambulizi lilitokea."

AU Inasemaje?

Umoja wa Afrika umelaani tukio hilo la kigaidi.

Mwenyekiti wa AU Moussa Faki Mahamat amesikitishwa na shambulizi hilo pia ametoa pole zake kwa askari waliofariki na kusema kuwa "Waliopoteza maisha hawatasahaulika kamwe".

Burundian peacekeepers in attention as Somali police officers go on parade

CHANZO CHA PICHA, AFP

Maelezo ya picha, 

Baada ya Uganda, Burundi pia ina washiriki wengi wa jeshi la Umoja wa Afrika nchini Somalia

Katika taarifa iliyotolewa na AU inasema kuwa umoja huo hautarudishwa nyuma harakati za umoja ho katika kulinda amani nchini Somalia bali itaendelea mpaka itakapofanikisha lengo lake la kulinda amani.

Bwana Faki amesema kuwa amezungumza na Rais wa Burundi Évariste Ndayishimiye na kutoa rambi rambi zake. 

Hatahivyo Rais Ndayishimiye amesema hakuna neno lenye nguvu zaidi ya kulaani mauaji ya wanajeshi walinda amani wa Burundi.

Takwimu

Aftermath of bomb blast in Mogadishu

CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES

Maelezo ya picha, 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Umoja wa Ulaya hatimaye wakubaliana kuufufua uchumi wao

Urusi kuisadia Uganda kujenga uwezo wake wa nyuklia, ni mataifa gani ya Afrika yanatumia nishati ya nyuklia na kwanini?