Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2020

Uchaguzi Tanzania 2020: Je, namna gani wapiga kura wanaweza kuepuka migogoro wakati wa kampeni?

Picha
  Matukio ya vurugu za kisiasa miongoni mwa wapiga kura wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa urais,ubunge na udiwani unaoendelea nchini Tanzania yameathiri mahusiano moja kwa moja kutokana na itikadi tofauti za vyama vya siasa licha ya Katiba ya nchi hiyo kusisitiza uhuru wa kila mwananchi katika kuchagua itikadi hizo pamwe na kudumisha misingi ya demokrasia na siasa za vyama vya vingi. Baadhi ya matukio hayo ni pamoja na matamko ya vitisho dhidi ya wafuasi na wanasiasa wa pande mbili tofauti, kujinyonga, kupigana kwa kutumia mapanga na silaha zingine za jadi hali ambayo inachochea uvunjaji wa sheria pamoja na kuibua taharuki miongoni mwa familia, ndugu, marafiki na taifa kwa ujumla. Duru za kisiasa zimetafsiri hali hiyo ni kiwango duni cha uvumilivu wa kisiasa miongoni mwa wapigakura, na kusababisha baadhi ya wapiga kura kuchukua uamuzi wa kukatisha uhai wao kwa sababu ya kutokukubaliana na wengine ndani ya familia, pamoja na viongozi kushindwa kuwa na lugha za ushawishi wafuasi wao

Carlo Acutis, atununikiwa utakatifu wa digitali

Picha
Kanisa Katoliki limepata baraka mpya Oktoba 10, kwa namna ya kipekee mno : Mshawishi ambaye mwili wake umeoneshwa kwenye laba,jeans na sweta. Leo hii Carlo Acutis anatangazwa kuwa mtakatifu katika mji wa Assisi, jimbo la Perugia, Italia. Acutis alifariki akiwa na umri wa miaka 15 kutokana na kansa ya damu mnamo Oktoba 12, 2006. Kijana huyo mdogo alijulikana sana katika jumuiya wa wakristo kutokana na kazi aliyoifanya katika kanisa kwa kutumia teknolojia mpya , kwa mujbu wa taarifa kutoka Vatican. Acutis alizaliwa mjini London mwaka 1991, ambako wazazi wake walihamia kwa ajili ya kazi lakini alikulia Milan. Acutis anatunukiwa utakatifu mapema sana tofauti na watakatifu wengine waliopita, ni baada ya miaka 14 tu tangu kifo cha kijana huyo. Acutis ni mwenye heri wa kwanza wa "millenia hii " aliyetumia mtandao kutumika katika kanisa, aliyeonesha mfano wa teknolojia inavyoweza kutumika vizuri sana katika kanisa. Hivi ndivyo Papa Pope Francis mwenyewe alivyomuelezea , kwa kusema ku

Ubalozi wa Marekani: Hatutasita kuwachukulia hatua watakaovuruga au kukwaza demokrasia Tanzania

Picha
Ubalozi wa Marekani umesema kwamba haumuungi mkono mgombea yeyote au chama chochote katika uchaguzi ujao wa Tanzania. ''Tunaunga mkono mchakato wa kweli wa uchaguzi huru, wa haki na wenye uwazi, kabla, wakati na baada ya siku ya uchaguzi. Hii ni pamoja na usalama wa wagombea wote, kuheshimiwa kwa utawala wa kisheria na hali ya mamlaka na vyombo vilivyopewa wajibu wa kusimamia na kuendesha uchaguzi kutokupendelea kabisa upande wowote'', ulisema ubalozi huo. Kupitia taarifa iliyochapishwa katika tovuti ya ubalozi wa taifa hilo nchini Tanzania, ubalozi huo hatahivyo umesema kwamba utafuatilia kwa karibu matendo ya watu wanaoingilia na kuvuruga mchakato wa kidemokrasia au kuchochea vurugu dhidi ya raia. Aidha ubalozi huo umesema kwamba unaunga mkono wito uliotolewa na wagombea wakuu wa kuwepo kwa mchakato wa uchaguzi wa amani na wenye uwazi. ''Tunatoa wito kwao na kwa wafuasi wao kuchukua hatua kutanzua hali ya usalama inayojengeka na kuepuka ma