Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2020

Kifo cha George Floyd: Wakili akiita 'mauaji yaliyopangwa'

Picha
Wakili wa familia ya George Floyd, ambaye kifo chake kiliibua maandamano ya hasira kote nchini Marekani , amemshutumu afisa wa polisi kwa "kupanga mauaji". Polisi wa Minneapolis Derek Chauvin ameshitakiwa kwa mauaji , lakini wakili Benjamin Crump amekiambia kituo cha habari cha CBS news kuwa yalikuwa ni mauaji ya kiwango cha kwanza. "Tunadhani kwamba alikua na nia … takriban dakika tisa aliendelea kushindilia goti lake kwenye shingo ya mwanaume ambaye alikua anamuomba amsamehe na kumwambia kuwa hawezi kupumua," alisema matukio ya uporaji yameripotiwa katika jimbo la Philadelphia. Video kutoka katika vituo viwili vya televisheni vya Philadelphia Jumapili zilionesha vijana wakivunja magari kadhaa ya polisi na kuiba katika duka moja . Ripoti ya Uchunguzi ya West Philadelphia, imesema kuwa magari ya polisi pia yalichomwa moto. Miji kadhaa ya Marekani imeweka amri ya kutotoka nje. Rais Donald Trump alituma ujumbe wake wa twitter uliosema: Sheria na amri v

Virusi vya corona: 'Sina mpango wa kuanzisha sindano za dawa ya mitishamba', asema Rajoelina

Picha
Rais wa Madagascar Andry Rajoelina amebadilisha msimamo wake kuhusu dawa ya nchi yake anayodai kuwa na uwezo wa kutibu corona. Mwezi uliopita bwana Rajoelina alizindua rasmi dawa ya mitishamba ambayo alisema kwamba ina uwezo kuzuia na kuponya wagonjwa walio na virusi vya corona. lakini hilo lilipingwa na shirika la afya duniani kwasababu hakuna thibitisho la kisayansi kuhusu dawa hiyo. Taasisi ya kitaifa ya matibabu nchini Madagascar pia ilitilia shaka uwezo wa dawa hiyo iliotengenezwa kutoka kwa mmea wa pakanga, ikisema huenda ikaathiri afya ya wanadamu. Lakini licha ya taarifa ya taasisi hiyo , siku ya Jumanne bwana Rajoelina alisema kwamba Madagascar itaanzisha sindano za dawa hiyo huku akiongezea kwamba majaribio yake tayari yameanza kufanywa nchini Marekani. Hatahivyo Michelle Sahondrarimalala, ambaye ni daktari na mkurugenzi wa tafiti za idara ya mahakama, amefafanua zaidi alichomaanisha rais huyo, akisema kwamba waandishi hawakumuelewa kile ambacho kiongozi huyo wa t

Virusi vya corona: Mashine ya kupima corona 'yakutwa na hitilafu Tanzania'

Picha
Wizara ya afya nchini Tanzania imetangaza kwamba uchunguzi wa serikali uliokuwa ukifanywa katika maabara kuu ya nchi hiyo umebaini kuwa moja ya mashime ya kupima corona ilikuwa na hitilafu. Waziri Ummy Mwalimu hii leo ametangaza matokeo ya uchunguzi aliyoagiza kufanyika baada ya Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli kutilia shaka ufanisi wa maabara hiyo. "Kamati imebaini kuwepo kwa mapungufu ya uendeshaji wa kitaaluma katika upimaji wa vipimo na uhakiki wa ubora wa majibu'' amesema Waziri Mwalimu. Pia kumebainika kuwepo kwa udhaifu katika uhifadhi wa vipimo vya covid-19, aidha imebainika kuwepo kwa upungufu wa Wataalamu"- Waziri Afya Ummy mwalimu amesema. Wizara ya afya nchini humo imeweka wazi kwamba sasa vipimo vitakuwa vinafanyika katika maabara iliyopo mabibo. "Kuanzia sasa shughuli zote za upimaji wa maabara ya taifa zitafanyika katika maabara mpya ya mabibo yenye vifaa vya kisasa vyenye ubora na uwezo wa kupima sampuli 1,800 ndani ya saa 24"

Virusi vya Corona: Vitu gani tunaweza kujifunza kwa nchi ambazo zimepambana mapema na corona?

Picha
Mlipuko wa pili wa maambukizi ya virusi vya corona sio tena suala la ikiwa linaweza kutokea badala yake ni lini litatokea na athari yake itakuwaje," amesema mwanabaolojia Dkt. Jennifer Rohn, ambaye amekuwa akifuatilia vile janga hili linavyoedelea Asia na kusambaa kote duniani. Shirika la Afya Dunia (WHO) limesema maambukizi mapya huenda yakaendelea kuwepo kwa kipindi kirefu na kutahitaji juhudi za pamoja ili kuudhibiti. Hata nchi zenye mikakati inayofanyakazi kwa ufasaha kukabiliana na jaga hili kupitia upimaji, kutafuta walioathirika na hatua za kusalia ndani - kama vile Korea Kusii na Japani huko Asia, lakini pia Ujerumani na Ulaya - zimeshuhudia mlipuko wa pili wa maambukizi punde tu baada ya kulegezwa kwa masharti. Wiki hii, timu ya Umoja wa Ulaya yenye kupambana na ugonjwa wa Covid-19 ilipedekeza kwamba Ulaya inastahili kujiandaa kwa mlipuko wa pili - na swali lililopo ni lini utatokea na athari zake zitakuwa na ukubwa gani, amesema mkurugenzi wa timu hiyo Andrea Amm

Virusi vya corona: Je kuna ushahidi kuwa dawa za malaria zinatibu corona?

Picha
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa ametumia dawa ya malaria ya hydroxychloroquine ili kuzuia maambukizi ya virusi vya corona licha ya kwamba wanasayansi wametoa angalizo dhidi athari ambazo zinaweza kujitokeza. Utafiti unaendelea kuangalia kama dawa hiyo ya malaria ya hydroxychloroquine ambayo ni sawa na chloroquine zinaweza kukabiliana na virusi vya corona. Tumeangalia kile ambacho tunakifahamu kuhusu dawa hizi. Nani ametoa wazo la kutumia dawa hizo Shirika la afya duniani limesema kuwa linahofia ambao wanajitibu wenyewe kwa dawa hizo kupata madhara makubwa. Hofu ya usalama wao imeibuliwa na ofisa wa zamani wa afya. Dkt. Rick Bright, ambaye aliondolewa katika wadhifa wake mwezi Aprili kutokana na jitihada za serikali za kutengeneza chanjo mpya, alisema nia ya rais Trump katika dawa hizi inavuruga juhudi za wanasayansi wengi. Je, kuna ushaidi kuwa dawa hizo zinaweza kutibu ugonjwa wa Covid-19? Awali rais Trump alizungumzia kiufupi kuhusu dawa ya hydroxychloroq

Obam akosoa ushughulikiaji wa janga la virusi vya corona

Picha
Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama amewakosoa viongozi wa nchi hiyo wanaoshughulikia janga la virusi vya corona akisema  janga hilo linaonesha maafisa wengi "hata hawajidai tu kuwa wanawajibika." Obama  alizungumza  katika kile  kinachojulikana kama "Show Me Your Walk" toleo la HBCU," tukio la  masaa  mawili  kwa  wanafunzi wanaohitimu  kutoka  vyuo  ambavyo  kwa  kihistoria  ni  vya watu wenye  asili  ya  Afrika  na  vyuo vikuu  lililotangazwa katika  You Tube, Facebook na  Twitter. Matamshi  yake  yalikuwa  bila kutarajiwa  ya  kisiasa, kutokana  na  ene o lenyewe, na  kugusia kuhusu  matukio ya  hivi  sasa kupindukia  virusi  na  athari  zake  za kijamii  na  kiuchumi. "zaidi  ya  kila  kitu, janga  hili  hatimaye limetoboa tena pazia  kwa ukamilifu  wake kuhusu  wazo  kwamba  watu  wengi  wanaohusika madarakani wanajua  kile  wanachokifanya," Obama  alisema. "Wengi  wao  hata  wanaonekani  kujidai  kuwa wanawajibika.&qu