Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2023

Dini ya Kiislamu kuipiku ile ya Kikristo kwa ukubwa 2070

Picha
CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES Maelezo ya picha, Waislamu wakifanya ibada. Utafiti unasema kuwa dini ya Uislamu inatarajiwa kuipiku ile ya Wakristo ifikiapo 2070 Uislamu ni dini ya pili kwa ukubwa baada ya Ukristo kwa sasa lakini inakua kwa haraka sana. Hata hivyo hilo huenda likabadilika iwapo mwenendo wa watu wanaojiunga na dini hiyo utaendelea, kulingana na utafiti uliochapishwa na kituo cha utafiti cha Marekani Pew Research Center. Kulingana na utafiti huo Uislamu unakuwa kwa haraka ikilinganishwa na dini nyengine yoyote ile duniani. Itaipiku dini ya Kikristo ifikiapo 2070 kulingana na makadirio yake na hivyobasi kuwa dini yenye ufuasi mkubwa duniani. MATANGAZO Umoja wa Wakristo na Waislamu Kibera Mkahawa wakataa kuwahudumia wanawake Waislamu Ufaransa Msikiti mkubwa Afrika wajengwa Algeria Mwaka 2010 taifa la Indonesia ndilo taifa lililokuwa na idadi kubwa ya Waislamu duniani lakini sasa India huenda ikawa na wafuasi wengi zaidi duniani ifikiapo 2050. Hatahivyo taifa hilo litakuwa

Kisima kikubwa China kuwahi kutokea Duniani;

Picha
Kwa nini China inachimba kisima chenye kina cha kilomita 11 ardhini? CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES Maelezo ya picha, Kitakuwa kisima kirefu zaidi kilichotengenezwa na mwanadamu nchini Uchina 6 Juni 2023 China imeanza kuchimba kisima chenye kina cha zaidi ya kilomita 11 (futi 11,100) ndani ya jangwa la Taklamakan katika mkoa wake wa kaskazini-magharibi wa Xinjiang. Kazi ya mradi huu ilianza wiki iliyopita. Kulingana na ripoti ya shirika rasmi la habari la China "Xin Wa", kisima hiki chenye kina kirefu kitafikia tabaka za kipindi cha zamani zaidi cha Cretaceous duniani. Muda uliokadiriwa wa mradi ni siku 457 ambapo wanaofanya kazi hapa watakuwa na shughuli nyingi usiku na mchana na mashine nzito. Mradi wa kipekee CHANZO CHA PICHA, GETTY IMAGES Maelezo ya picha, Tayari kuna kisima cha mafuta kilicho umbali wa kilomita tisa ndani ya jangwa la Taklamakan Mradi huo unatajwa kuwa mradi mkubwa zaidi wa uchimbaji madini nchini China. Hapo awali, kisima kirefu zaidi cha aina yake nchi