Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2021

Kombe la dunia : Afrika haina viwanja vya mechi za kombe la dunia

Picha
Saa 2 zilizopita CHANZO CHA PICHA,  GETTY IMAGES Kupigwa marufuku kwa viwanja kadhaa vya soka barani Afrika huenda kutaathiri mechi za ufunguzi za kufuzu kwa Kombe la Dunia la Afrika mnamo Juni. Jumla ya mataifa 10 kati ya 40 yanayoshiriki katika kampeni ya kufuzu yanakabiliwa na tishio la kushiriki mechi nje ya mipaka yao . Hii ni baada ya Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) kutuma barua kwa mashirikisho wanachama wiki hii iliyokuwa na orodha ya viwanja vilivyoidhinishwa kwa raundi mbili za kwanza za mechi za makundi. Nchi zilizoathiriwa ni pamoja na Senegal, ambao walishiriki kwenye Kombe la Dunia lililopita huko Urusi mnamo 2018, na Mali, ambao walikuwa miongoni mwa timu zilizoshinda nafasi ya kwanza. MATANGAZO Tetesi za soka Ulaya Jumatano 05.05.2021 Burkina Faso, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Liberia, Malawi, Mali, Namibia, Niger na Sierra Leone zote hazijaidhinishiwa viwanja vyao vya nyumbani wakati Caf inapokabiliana na miundombinu mibovu kote barani. Sasa timu hizo zina muda mfupi

Bill Gates: Bilionea wa Microsoft atalakiana na mkewe Melinda Gates

Picha
Bill na Melinda Gates wametangaza talaka yao baada ya miaka 27 ya ndoa, wakisema "hatuamini tena tunaweza kuwa pamoja kama wanandoa". "Baada ya kufikiria sana na kufanya kazi nyingi juu ya uhusiano wetu, tumefanya uamuzi wa kumaliza ndoa yetu," wawili hao walisema katika ujumbe wa twitter . Walikutana kwa mara ya kwanza miaka ya 1980 wakati Melinda alipojiunga na kampuni ya Bill ya Microsoft. Wanandoa hao mabilionea wana watoto watatu na kwa pamoja wanaendesha Wakfu wa Bill & Melinda Gates. Shirika hilo limetumia mabilioni kufadhili kampeni mbalimbali ikiwemo magonjwa ya kuambukizana na kuhamasisha chanjo kwa watoto. Wawili hao - pamoja na mwekezaji Warren Buffett - wanahusika na mpango wa Ahadi ya Kutoa, ambao unawataka mabilionea kujitolea kutoa utajiri wao mwingi kwa malengo ya kuwafaidi watu . CHANZO CHA PICHA,  GETTY IMAGES Bill Gates ndiye mtu wa nne tajiri zaidi ulimwenguni, kulingana na Forbes, na ana mali ya thamani ya $ 124bn (£ 89bn). Alipata pesa kup